Hodi wana - JF?

WABHEJASANA

JF-Expert Member
Jun 22, 2011
4,225
869
Habarini za mchana wana JF?

Kiukweli na kwa moyo wa dhati kabisa nimeamua kujiunga humu ndani ili tuweze kuunganisha nguvu katika kuipigania nchi hii.

Nimekuwa nikichungulia tu mawazo yenu kama user wa kawaida lakini mwisho wa siku nimeona kuna haja na kila sababu ya mimi kuwa member ili tushirikiene kwa pamoja,kwanza niwapongeze wale wana CDM kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya humu ndani katika kuielemisha jamii,kiukweli na bila kipingamizi tunapaswa kusimama kidete kuhakikisha kwamba ushindi unapatikana pamoja na kwamba kuna watu wenye kukatisha tamaa.Lakini pia ni lazima tusimame kwenye ukweli mtupu ili Mwenyezi Mungu awe upande wetu.Nimeona ni vyema mwaka huu usipite ili niingine mwaka ujao kwa matumaini mapya na mawazo mapya.mchana mwema na chakula chema.Pipooooooooooz????!!!
 
Karibu Pipooooz!Humu kila unachokitaka utapata ni wewe tu na roho yako.
 
aiseeeeeeee babaangu mimi ndio mkuu rombo naripoti moja kwa moja kutoka mkuu rombo karibu sana janvin mkuu
 
Kwanza kabisa nikukatishe tamaa na hiyo slogan yenu ya pipoz pawa ingawa unaonekana unayo nia njema kabisa kuitakia nchi yetu yaliyo mema.Hiyo ni slogan iliyopitwa na wakati na ilikuwa na matumizi enzi za nyuma sana wakati dunia inatawaliwa na wafalme wababe na mabwana vita. Leo hii dunia iko kwenye enzi za kutawaliwa na uchumi na slogan muafaka hapa ni Money Power na sio Peoples' Power. Mwenye pesa ndiye mwenye nguvu na ndie atakaetawala. Yote mnayoyaona huko Syria, Misri, Libya, Tunisia, Bahrein, na yaliyopita kule Iraq na Afghanistan yote ni Money Power. Nguvu za kutawala mwenendo wa kuendesha tawala ulishatwaliwa mikononi mwa masses na hivi sasa upo mikononi mwa wachache wenye pesa na ndio mana kila mtu anakimbizana na pesa na ufisadi kwa maana hiyo ndiyo pekee yenye fursa ya kutawala katika zama hizi.
 
Back
Top Bottom