Hodi hodi mpaka ndani

drrwgrant

New Member
May 26, 2014
3
1
Jamaani salamu zote! Baada ya kukurukukuru tu kwa muda mrefu nikaona bora nijiunge rasmi na nimefurahi sasa kuwa mwana-JF halisi.
 
Karibu mgeni ila humu hutakiwi kuwa na hasira

Ahsanteni sana kwa kunikaribisha. Vile naomba radhi kwa kukosea hapo juu, nilitaka kuandika "baada ya kulurku" na siyo "baada ya kukurukukuru". Lurku nimeibuni tu kutoka neno la kingereza lurk: kufuata mazungumzo ukiwa mwenyewe unakaa kimya na kutochangia lo lote. Hilo neno lengine kukurukukuru sijui limeingiaje, labda spellcheck hata maana yake sikufahamu. Kwa vyovyote tafadhali usifikiri kuwa nimejiunga hapa nikiwa na hasira bali nia yangu kupeana mawazo na haswa kujifunza. Naona hapa nimeshapata funzo la kwanza, nisiwe nachapisha haraka na kubonyeza post message bila kusoma tena kile nilichokiandika kwanza.
 
Ahsanteni sana kwa kunikaribisha. Vile naomba radhi kwa kukosea hapo juu, nilitaka kuandika "baada ya kulurku" na siyo "baada ya kukurukukuru". Lurku nimeibuni tu kutoka neno la kingereza lurk: kufuata mazungumzo ukiwa mwenyewe unakaa kimya na kutochangia lo lote. Hilo neno lengine kukurukukuru sijui limeingiaje, labda spellcheck hata maana yake sikufahamu. Kwa vyovyote tafadhali usifikiri kuwa nimejiunga hapa nikiwa na hasira bali nia yangu kupeana mawazo na haswa kujifunza. Naona hapa nimeshapata funzo la kwanza, nisiwe nachapisha haraka na kubonyeza post message bila kusoma tena kile nilichokiandika kwanza.

Hukunielewa mkuu sio hasira kwa sababu ya hilo neno ulilokosea Kuandika bali ni tahadhari tu kwa sababu humu kuna watu majibu yao yanaweza kukupandisha hasira ukajikuta unatukana unatakiwa ucheke na kumrekebisha ili siku ipite kwa usalama.
 
Back
Top Bottom