Hizi zilikuwa wiki mbaya kwa Nape na Zitto, au ndiyo mwanzo wa mwisho wao?

mpk

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
3,115
3,862
Nape tangu amekuwa mwenezi wa CCM hakuwahi kukutana na ziara ngumu kama hii anayoendelea nayo kanda ya ziwa. Ugumu wa ziara si kukosa watu kwenye mikutano tu, bali zomea zomea iliyoikumba ziara yake na katibu mkuu wa Ccm ndg Kinana. Ilianzia pale Bukoba Nape aliposema meli iliyohaidiwa na Kikwete si kipaumble, wananchi wakamzomea. Kule Mleba alipojaribu kumpamba Prof Tibaijuka wananchi wakamzomea, aliposhuka tu Nkwenda wilaya ya Kyerwa boda boda wakazomea Nape akashika shati lake na kusema "ZOMEENI TU LAKINI HATA KWA DAMU SHATI HILI NDO LINAINGIA IKULU" haikuishia hapo jana akazomewa mpaka akwaambia watu wamekunywa viroba vya Chadema.

Kwingineko Zitto naye ameonja joto ya jiwe kule Geita, Momba na Mbeya mjini, Zitto kwa upande wake anakutana na kasheshe hiyo pale anapojaribu kukikosoa chama chake cha zamani au viongozi wake. Mfano Mbeya mjini alikumbana na dhahama pale alipomkosoa Mbowe kutembelea shangingi la kiongozi wa kambi ya upinzani. Zitto alilazimika kujitetea kwamba wanaozomea ni wale wanaoamini wanasiasa kupindukia kiasi cha kuaminshwa kwamba yeye ni MSALITI.

Kwa ujumla hizi zilikuwa wiki mbaya kwa vijana hawa, lakini je siku mbaya kwao zimepita? Kwa kuwa mara nyingi Zitto huzomewa kila anapojaribu kuisema Chadema, atafanyaje siasa bila kusema alifukuzwa Chadema kwa nini? Kuhusu Nape siku zake zinaweza kuwa zinahesabika kwa vile mara nyingi mwenyekiti mpya wa Ccm huja na sekeritarieti yake, lakini je kwa muda aliyobaki nao ajipambanue namna gani? asiiguse Chadema wakati ndiye mpizani wake mkuu?
 
wanachoshindwa ni kujua shida za wananchi hivi mbowe akirudisha shangingi then maisha ya mtanzania yanakuwaje? kwanini mnashindwa kujua chanzo halisi cha matatizo ya watz? watu wanathamini mda wao si unawaita huna hoja.


Hawa wengine wanaishia kusema ufisadi upo vyama vyote ni upuuzi umekabidhiwa serekali miaka hamsini unakusanya watu unatoa pumba za namna hiyo watu watachukia tu kikubwa wawe tayari kubadilika
 
wanachoshindwa ni kujua shida za wananchi hivi mbowe akirudisha shangingi then maisha ya mtanzania yanakuwaje? kwanini mnashindwa kujua chanzo halisi cha matatizo ya watz? watu wanathamini mda wao si unawaita huna hoja.


Hawa wengine wanaishia kusema ufisadi upo vyama vyote ni upuuzi umekabidhiwa serekali miaka hamsini unakusanya watu unatoa pumba za namna hiyo watu watachukia tu kikubwa wawe tayari kubadilika

wanafanya siasa za mtu badala ya siasa za masuala ndio maana wanazomewa ......Supreme leader badala ya kuongelea azimio lake la Tabora aka Arusha .....anaongelea shangingi la Mbowe what a shame ?
 
wanafanya siasa za mtu badala ya siasa za masuala ndio maana wanazomewa ......Supreme leader badala ya kuongelea azimio lake la Tabora aka Arusha .....anaongelea shangingi la Mbowe what a shame ?

Naona hoja ktk mchango wako, lakini kumbuka kuna kulewa sifa baada ya mafanikio ya muda kisiasa.
 
wanafanya siasa za mtu badala ya siasa za masuala ndio maana wanazomewa ......Supreme leader badala ya kuongelea azimio lake la Tabora aka Arusha .....anaongelea shangingi la Mbowe what a shame ?

Issue sio ngumu kiivyo kwamfano unafika unawasalimu wananchi unawaeleza lengo la chama na kuwa wapizani bado hawajawa na resources za kutosha hivyo kuna maeneo mengi hayajafikiwa kikamilifu, pia wananchi wanapaswa kukumbushwa kila wakati wasisahau mapambano dhidi ya mfumo wa kinyonyaji wa CCM. Waelezee ulivoshirikiana na wenzako kwenye hoja ya escrow. Ricmond na mengine. Eleza kuwa hauna tofauti nao ila ni mitizamo ya kisera kisha mwaga azimio la wapi sijui-utajikuta umewavuta na watakukubali. Sasa unakoroma tu Mbowe .shangingi what for?
 
wanachoshindwa ni kujua shida za wananchi hivi mbowe akirudisha shangingi then maisha ya mtanzania yanakuwaje? kwanini mnashindwa kujua chanzo halisi cha matatizo ya watz? watu wanathamini mda wao si unawaita huna hoja.


Hawa wengine wanaishia kusema ufisadi upo vyama vyote ni upuuzi umekabidhiwa serekali miaka hamsini unakusanya watu unatoa pumba za namna hiyo watu watachukia tu kikubwa wawe tayari kubadilika

Alichishindwa ZZK ni kufanya siasa za kuvuta watu wapya ambao hawako kwenye vyama na ambao ndiyo wengi na badala yake anaendelea na siasa zilizomfanya kufukuzwa. Watu wana vyama vyao na wanawaamini viongozi wao ndiyo maana wako kwenye vyama hivyo, kujaribu kuoondoa imani yao kwao ni kujiletea matatizo.
 
Wakati ambapo zito ataacha kuikashifu chadema na kunadi sera za ACT ndipo atakapopata ahueni katika maisha yake, yeye kapotoka kwa kusema uongo kuikana ACT na kuing'ang'ania chadema kwa nguvu za mahakama, sasa chuki inamuumiza na ili awe na amani aache chuki asonge kujenga ACT yake kwanza yeye ni kiongozi mkubwa ambae hakuna chama chochote cha siasa wanacho hiko cheo kwa nini asifarijike?
 
wachunguzi wa mambo ya GUNDU , MIKOSI na LAANA wanadokeza kwamba haya mambo yakishaanza hayaishi mpaka uingie kaburini .
 
Alichishindwa ZZK ni kufanya siasa za kuvuta watu wapya ambao hawako kwenye vyama na ambao ndiyo wengi na badala yake anaendelea na siasa zilizomfanya kufukuzwa. Watu wana vyama vyao na wanawaamini viongozi wao ndiyo maana wako kwenye vyama hivyo, kujaribu kuoondoa imani yao kwao ni kujiletea matatizo.
umeandika kisomi sana ! Hongera !
 
wachunguzi wa mambo ya GUNDU , MIKOSI na LAANA wanadokeza kwamba haya mambo yakishaanza hayaishi mpaka uingie kaburini .

Naona umekuwa mungu watamani nyota ya zitto ififie lkn wapi ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu
 
wanafanya siasa za mtu badala ya siasa za masuala ndio maana wanazomewa ......Supreme leader badala ya kuongelea azimio lake la Tabora aka Arusha .....anaongelea shangingi la Mbowe what a shame ?
hizi ndio siasa wanazozipenda sana wapambe na washauri wake akina mchange na wachumia tumbo wengine , lakini huu ndio mwanzo wa mwisho wao .
 
wala sio mimi mkuu , hiyo ni kwa mujibu wa wabobezi wa mambo hayo .

Ukweli ni kuwa nyota ya zitto haizimiki labda allah atakapoamua yeye na kumfanyia fujo ndio munampa ujasiri zaidi sio kuwa mnamrudisha nyuma
 
Hakuna anayetaka kufifisha nyota ya mtu, ZZK anapata wakati mgumu kwa sababu ya kibri cha na kujiona bora kuliko binadamu yoyote nchi hii.
 
Hivi Zitto hawezi kuiongelea Ccm ambayo ndio inaongoza dola kutwa kucha chadema. Asubiri ukawa ikichukua nchi atakuwa na room nzuri kuisema.
 
Issue sio ngumu kiivyo kwamfano unafika unawasalimu wananchi unawaeleza lengo la chama na kuwa wapizani bado hawajawa na resources za kutosha hivyo kuna maeneo mengi hayajafikiwa kikamilifu, pia wananchi wanapaswa kukumbushwa kila wakati wasisahau mapambano dhidi ya mfumo wa kinyonyaji wa CCM. Waelezee ulivoshirikiana na wenzako kwenye hoja ya escrow. Ricmond na mengine. Eleza kuwa hauna tofauti nao ila ni mitizamo ya kisera kisha mwaga azimio la wapi sijui-utajikuta umewavuta na watakukubali. Sasa unakoroma tu Mbowe .shangingi what for?

Baba yangu aliniambia kuwa hata kama umesoma ukawa na elimu ya Chuo Kikuu kama huna busara ni kazi bure! Tunachohitaji sisi wananchi ni faraja kuu ya moyo, ambayo tumeikosa tangia Kikwete aingie madarakani! Sasa ukija na porojo sijui mimi ni mzalendo tunakuona na wewe ni sehemu ya tatizo, kilichobaki sasa tutawashusha jukwaani kwa mawe maana hatuna namna sasa tumechoka!
 
Naona matusi yoyote yakitupwa humu yanawashabiki sana tofauti na halihalisi. Lazima tutambue kuwa ZZK ameondoka na anajenga chama chake. Wanaokwenda kumsikiliza wana haki zaidi ya wewe unayeandika huku.
 
Issue sio ngumu kiivyo kwamfano unafika unawasalimu wananchi unawaeleza lengo la chama na kuwa wapizani bado hawajawa na resources za kutosha hivyo kuna maeneo mengi hayajafikiwa kikamilifu, pia wananchi wanapaswa kukumbushwa kila wakati wasisahau mapambano dhidi ya mfumo wa kinyonyaji wa CCM. Waelezee ulivoshirikiana na wenzako kwenye hoja ya escrow. Ricmond na mengine. Eleza kuwa hauna tofauti nao ila ni mitizamo ya kisera kisha mwaga azimio la wapi sijui-utajikuta umewavuta na watakukubali. Sasa unakoroma tu Mbowe .shangingi what for?

Ndugu yangu elewa kuwa anayemlipa mpiga zomari ndiye anayechagua wimbo gani uimbwe. Zitto hana lolote analoweza kuwaambia wananchi kwa sasa na ingewezekana angepumzika kabisa. Tatizo ni kuwa alikwishalipwa kwa kazi ambayo bado anatakiwa kuikamilisha nayo ni kusambaratisha upinzani. Anapokuwa katika mikutano yake analazimika kusema kile wanachopenda kukisikia wanaomlipa.
 
Back
Top Bottom