Hizi tabia za wake zetu wakiwa wajawazito ni tabia zao, maigizo, visasi ama malipizi?

Billie

JF-Expert Member
Aug 13, 2011
12,666
19,674
Poleni na majukumu na COVID 19 ambayo sisi kama taifa ya JMT tumeamua kukana kuwa kinachotusumbua sio COVID bali na tatizo la upumuaji almaarufu kizungu kama pneumonia.Anyway tuachane na hilo twende kwenye mada.

MADA: Wifi yenu ni mjamzito wa miezi 6 ila cha kushangaza amekuwa na matabia ya ajabu kama mzimu ambapo anapelekea nitamani kumzaba mikofi ama nihame nyumba au nishinde bar. Unakuta ananifanyia matendo yanayoashiria hanipendi hata kuniona ambazo tabia hizo ni ngeni kabisa kwake ukifananisha na enzi zile hana mimba, mbaya zaidi mwenzenu nanyimwa uch.i leo ni siku ya 29 na hii imepelekea kurundikana kwa nye.ge mwilini mwangu ambazo zimezalisha hasira kali mno haswa ukijumLisha na kabila langu la kikurya yaani natamani hata nijambe ili nirelax. Mke wangu imefika point nikitoka kazini narudi home yeye anahama hata chumba analala kwenye chumba cha mtoto wetu wa kiume JUNIOR ambapo nye.ge zinanipelekea kumkufuru MUNGU mpaka naanza kumuonea wivu mwanangu Junior wa miaka 7

ANYWAY,Naomba niulize JE hivi visa vinavyoendelea kwa wake zetu wajawazito ni maigizo,FUTUHI,visasi au ni nini? nauliza hivi kwa sababu enzi za mimba ya JUNIOR mke wangu hakuwa hivi nakumbuka alikuwa anapenda niwe nimelala mapajani mwake huku tunaangalia movie chumbani kwetu leo hii nashangaa mimba hii imeniletea uhasama mpaka shetani wa kuchepuka anashinda masikioni mwangu akininong'oneza ma vitu ya ajabu ajabu.

ANGALIZO: Uzi huu ningependa uchangiwe na wenye wake au wanawake wenyewe ambao wapo kwenye ndoa au wenye experience na ujauzito tena ikibidi zaidi ya mmoja.Na wale wazee wa kutoona siku ndani ya mwezi mbio mpaka kwenye DUKA LA DAWA kwenda kununua MISOPROSAL naombeni mtoe like kwenye uzi na comments za wadau tajwa hapo juu

KARIBUNI TUJIFUKIZE KWENYE HUU UZI.
 
Hahahhahaa hayo yako madogo aisee kuna wengine wanaagizwa utumbo wa ng'ombe dume(sasa ujiulize mhusika atajuaje kama ni utumbo wa ng'ombe dume), wapo walioagizwa miwa usiku wa manane, wapo walioendea mishikaki umbali wa kilomita tano kwaajiri ya kunusa tu na sio kula na mengine mengi sanaaa.

Nadhani yangekutokea hayo ndo ungejiaminisha kwamba unakomolewa, ila ni mambo ya kawaida tu
 
Hapa naona tifauti kubwa saba kati yetu na wewe. Hizi habari huwa hatuzitoi, sababu tunajua kunata na biti.

Jahazi likielekea kusi badili upande elekea kule upepo unapo vuma. Ila siku 29 parefu sana aisee. Inaonekana umeishiwa mbinu, chukua hiyo mbinu ya juu. Sisi huwa tunapewa hata kama tunachukiwa kiasi gani.
 
Ukweli mara nyingi tabia hizo huchangiwa na mabadiliko ya mfumo wa homoni, mara nyingi hotokea bila wao kupenda, japo wapo wachache ambao huongezea na visasi ndani yake.

Ila mara nyingi ni sababu za homoni tu kwa wengi wao
 
Hahahhahaa hayo yako madogo aisee kuna wengine wanaagizwa utumbo wa ng'ombe dume(sasa ujiulize mhusika atajuaje kama ni utumbo wa ng'ombe dume), wapo walioagizwa miwa usiku wa manane, wapo walioendea mishikaki umbali wa kilomita tano kwaajiri ya kunusa tu na sio kula na mengine mengi sanaaa.

Nadhani yangekutokea hayo ndo ungejiaminisha kwamba unakomolewa, ila ni mambo ya kawaida tu
khaaaah
 
10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom