Hizi smartphone zimeleta kizungumkuti, ndiyo chanzo kikubwa cha matatizo

Black BackUp

JF-Expert Member
Aug 5, 2019
683
618
Habari wana JF, Niende straight to the point.

Unakuta mgeni amekuja kukutembelea nyumbani kwako/kwenu wote mnakuwa bize na simu kwenye mtandao kati yenu panakuwa hakuna stori zaidi ya salamu na kuitikiana tu ehee.

Mwingine anajibu hata kisichoulizwa/ambiwa,dereva naye anachati mpaka anasimama katikati ya zebra ama foleni inaenda hana habari.

Kilichonikumbusha niandike uzi yaani kwenye daladala jana mdada amemdondosha mtoto chini ya siti baada ya kukonsetreti kwenye simu mpaka akasahau kwamba kashika mtoto.

Jamani inabidi tubadilike, simu hizi (smartphone) ndiyo chanzo sana cha matatizo.
 
Zamani ilikua unaenda eneo la kusubiri huduma mfano benki unakuta magazeti au kama si magazeti unakuta wateja wenzako mtapiga stori za hapa na pale mpaka mnahudumiwa na kuondoka.

Magazeti na wateja wenzako wamekua replaced na smartphones. Ni mbaya ila ndiyo ukweli. Hii imepelekea kuharibu namna ya kuwasiliana, kusocialize na hata kushughulika na maswala madogo madogo yanayoweza kutatuliwa na maongezi.

Huwezi ikimbia teknolojia. Kaza mwendo.
 
1572497925433.png

Unakuta mgeni amekuja kukutembelea nyumbani kwako/kwenu wote mnakuwa bize na simu kwenye mtandao kati yenu panakuwa hakuna stori zaidi ya salamu na kuitikiana tu ehee.
Na hata wakiwa kwenye faragha zao simu haiachi
1572497700465.png


1572497801450.png

Mbona Ulaya wazungu hawana hii tabia
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom