Hizi picha zinatoa ujumbe gani wakati huu wa kampeni?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,335
217,362
@mlinga_goodluck mapema siku ya leo akiwa Tarime Vijini, kata ya Sirari akijiliw ( 655 X 640 ).jpg


Instagram media - CFfKDBZnqeG ( 800 X 640 ).jpg


Hawa ndo Raia wa Kagera.. . . Naomba mnisaidie kuwatag ndugu zangu wa Kagera ( 640 X 640 ).jpg


Mara kadhaa nimesikia kwamba ili mambo yako yasikwame katika awamu hii na hasa kwenye kipindi hiki cha kampeni basi kazi ni ndogo tu , chukua sare za ccm hata kama hazikuenei wewe zivae halafu fanya lolote , iwe magendo au uharamu wowote hutaguswa na yeyote , si polisi wala mgambo wa jiji .
 
wewe eww
View attachment 1581746

View attachment 1581747

View attachment 1581751

Mara kadhaa nimesikia kwamba ili mambo yako yasikwame katika awamu hii na hasa kwenye kipindi hiki cha kampeni basi kazi ni ndogo tu , chukua sare za ccm hata kama hazikuenei wewe zivae halafu fanya lolote , iwe magendo au uharamu wowote hutaguswa na yeyote , si polisi wala mgambo wa jiji .
Magu kaharibu nchi yetu sana,nikiangalia alivyo jaza bajaji kwenye barabara za Dar yaani nikiona picha yake napata kichefuchefu
 
View attachment 1581746

View attachment 1581747

View attachment 1581751

Mara kadhaa nimesikia kwamba ili mambo yako yasikwame katika awamu hii na hasa kwenye kipindi hiki cha kampeni basi kazi ni ndogo tu , chukua sare za ccm hata kama hazikuenei wewe zivae halafu fanya lolote , iwe magendo au uharamu wowote hutaguswa na yeyote , si polisi wala mgambo wa jiji .
Hao wapwa wanapiga spana za kimya kimya. Ndio hawa wakienda kwenye mikutano ya maccm wanamuuzia Magufuli kuku , kumbe mifukoni wana kadi za Chadema.
 
Ccm inapita wakati mgumu sana.. karibia wanagawana mbao

Pongezi kwa chadema.. hakuna wakati ambao chadema imekua na nguvu kama wakati huu.

Hata wakiiba kura zote bado chadema imeitangazia dunia kwamba ni chama makini.
 
Makonda, Ndugai, Chalamila, Gambo, Musiba, ni kati ya watu waliochangia sana CCM kuchukiwa.

Kwa miaka hii mitano, Tanzania imegeuzwa na kuonekana nchi ya ajabu. Rais amefanya mambo.mengi ya ajabu, mambo yanayodhalilisha utu, mambo yanayotweza utu wa watu, amefanya mambo mengi ya kuwafukarisha watu, amefanya mambo mengi ya kuwaondolea watu ajira, amefanya mambo ya kuua future za watu.

Uongozi wa Magufuli haujui top priorities za wanadamu. Top priorities za wanadamu, ni mambo yanayogusa maisha yao ya kila siku. Ni kweli ndege, barabara, reli ni muhimu lakini binadamu ana uwezo wa kuvumilia kuishi bila ya hivyo vitu. Lakini hawezi kuishi bila akira, hawezi kuishi bila chakula. Kuna vitu vinaweza kusubiri, kuna vitu mwanadamu hawezi kusubiri.

Unaweza kuwaambia wananchi wasubiri kununuliwa ndege lakini huwezi kumwambia mtu asubiri kula, au mahali pa kulala, au mavazi au mwanae kwenda kusoma, n.k.

Lakini kitu kingine cha ajabu, watu wale wenye upeo mdogo, wasio na busara wala utu, watu katili waliokosa utu, na huenda hawana malezi bora, kama Makonda, Gambo, Sabaya, Chalamila, n.k, Rais Magufuli, hao ndio best eleven yake!! Watu wengi wanajiuliza, kwa nini iwe hivyo? Ndiyo maana wengine wanaenda mbali na kusema, huenda hawa watu wamemshika kwa nguvu za giza!! Siamini kama ni kweli lakini nadhani wanataka kumpelekea ujumbe Rais kuwa wanashangaa kwa nini watu wa hovyo kwake wamekuwa nyota.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umeandika vizuri sana
Makonda, Ndugai, Chalamila, Gambo, Musiba, ni kati ya watu waliochangia sana CCM kuchukiwa.

Kwa miaka hii mitano, Tanzania imegeuzwa na kuonekana nchi ya ajabu. Rais amefanya mambo.mengi ya ajabu, mambo yanayodhalilisha utu, mambo yanayotweza utu wa watu, amefanya mambo mengi ya kuwafukarisha watu, amefanya mambo mengi ya kuwaondolea watu ajira, amefanya mambo ya kuua future za watu.

Uongozi wa Magufuli haujui top priorities za wanadamu. Top priorities za wanadamu, ni mambo yanayogusa maisha yao ya kila siku. Ni kweli ndege, barabara, reli ni muhimu lakini binadamu ana uwezo wa kuvumilia kuishi bila ya hivyo vitu. Lakini hawezi kuishi bila akira, hawezi kuishi bila chakula. Kuna vitu vinaweza kusubiri, kuna vitu mwanadamu hawezi kusubiri.

Unaweza kuwaambia wananchi wasubiri kununuliwa ndege lakini huwezi kumwambia mtu asubiri kula, au mahali pa kulala, au mavazi au mwanae kwenda kusoma, n.k.

Lakini kitu kingine cha ajabu, watu wale wenye upeo mdogo, wasio na busara wala utu, watu katili waliokosa utu, na huenda hawana malezi bora, kama Makonda, Gambo, Sabaya, Chalamila, n.k, Rais Magufuli, hao ndio best eleven yake!! Watu wengi wanajiuliza, kwa nini iwe hivyo? Ndiyo maana wengine wanaenda mbali na kusema, huenda hawa watu wamemshika kwa nguvu za giza!! Siamini kama ni kweli lakini nadhani wanataka kumpelekea ujumbe Rais kuwa wanashangaa kwa nini watu wa hovyo kwake wamekuwa nyota.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nyerere aliwahi kkusema madui wakuu wa maendeleo ni MARRADHI, UJINGA NA UMASIKINI nadhani alimsahau adui mmoja ambae ni UCHAWI. Nyinyiemu ya safari hii umejaza uchawi mwingi mno
 
Back
Top Bottom