Hizi ndo picha za jamaa aliyepofuliwa macho kwa kutembea na mke wa Polisi

LIKUD

JF-Expert Member
Dec 26, 2012
14,936
26,637
PO1.PNG



PO2.PNG


po3.PNG
 
Ndo akome
Usiseme hivyo wewe, punishment should fit the crime. hapa Ze Polisi ameenda mbali sana aisee.
Kama kila dhambi ingekuwa inatolewa adhabu hapa na kwa jinsi hiyo unafikiri tungekuwaje?
Haya hata useme shida ni mke wa mtu...Hao wasichana mnaolala nao daily na kuleta visa huku jukwaani kwani c wanakuja kuwa wake za watu?
Yani najua Mungu akituangalia jinsi tulivyopotea hasira zinaongezeka kila kukicha duniani, Ole wetu!!
 
Kuna jamaa nikepanga nae nyumba moja, anapenda sana wake za watu kuna kabinti mke wa mtu jamaa anatembea nako na mme wake hajui kutokana na ubize. Sasa mtu kama huyo anajua kabisa huyo ni mke wa mt u lakini hasikii inafikia wakati anapata hadi wivu jamaa akienda kuoga na mke wake. Nimemsihii sana lakini haelewi. Mtu kama huyu akibambwa si hata shingo akatwe. Mwenzaka kao kwa halali yeye badala atafuta walio single anatafuta walio double ili apate mseleleko wa maisha. Ajui kama mwenzake anagharamia.
 
heeh inawezekana huyu jamaa ni mzembe sana, hadi kutobolewa macho yote mawili?

Pole yake.
 
anastahili kifungo cha maisha huyo polisi, ukiona mke wako kalala na mtu sijui kwa nini unamfata msela, wa kumfata ni mke wako na kuamua unafanyaje kama ni hela inarudishwa afu asepe, sasa jamaa yeye kosa lake nini? inabidi ujichunguze mara mbili umekosa nini hadi mke wako aende nje, afu kwa nini hujui kuchagua hadi ukamchagua ambaye atakuja kukusaliti baadaye...
 
Ni adhabu kubwa sana aliyopmdwa ila ni uzembe wake kupewa adhabu hii. Mke anauma bhana.
 
Haya kashamtia upofu baba wa watu,na mkewe kampa adhabu gani?
 
anastahili kifungo cha maisha huyo polisi, ukiona mke wako kalala na mtu sijui kwa nini unamfata msela, wa kumfata ni mke wako na kuamua unafanyaje kama ni hela inarudishwa afu asepe, sasa jamaa yeye kosa lake nini? inabidi ujichunguze mara mbili umekosa nini hadi mke wako aende nje, afu kwa nini hujui kuchagua hadi ukamchagua ambaye atakuja kukusaliti baadaye...

lakini kwanini jamaa nae atembee na mke wa mtu, hata maandiko yanasema ' kwa ajili ya zinaa, kila mtu awe na mke wake'. Siungi alichofanyiwa jamaa wala sifurahii uzinzi aliokuwa anaufanya jamaa.
 
lakini kwanini jamaa nae atembee na mke wa mtu, hata maandiko yanasema ' kwa ajili ya zinaa, kila mtu awe na mke wake'. Siungi alichofanyiwa jamaa wala sifurahii uzinzi aliokuwa anaufanya jamaa.

Kwani mwanamke anatembea kaandikwa kua "mimi mke wa mtu"?? wanawake wanatoka nje ya geti tu pete wanaweka kwenye mkoba, Afu wa kujilinda ni nani? Mke wa mtu anastahili kua wa kwanza kusema NO maana anajijua yeye ni mke wa mtu tayari ana mume, ana sehemu ambapo akitaka muda wowote shida yake ya ngono inaweza ikatatuliwa kwa nini alale na mtu nje, siwezi kulaumu mtu anayelala na mke wa mtu mimi, sawa katenda dhambi ila hana tofauti na aliyelala na binti wa kawaida tu, wanawake wenyewe ndio wajiheshimu.
 
Simlaumu polisi... alifanya kwa kadri yake kuiridhisha nafsi yake, mshahara wa dhambi mara zote ni mauti ingawa pia hakuna aliye msafi..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom