Mukuru
Member
- Apr 14, 2009
- 40
- 0
Komba amzimia Waziri Nagu
Mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba amemsifu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Mary Nagu, kuwa ana sura nzuri na anauzika.
Mbunge huyo amelieleza Bunge leo kwamba, yupo tayari kutunga wimbo wa kumsifu Waziri huyo.
Kabla ya kutoa sifa hizo, Kapteni Komba alisema bungeni mjini Dodoma kwamba, Dk Nagu leo kapendeza kuliko siku nyingine zote.
Mbunge huyo ametoa sifa hizo wakati anachangia bajeti ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko iliyowasilishwa leo bungeni.
Komba amesema, pamoja na sifa za uzuri wa sura na kuuzika, kwa kuwa Waziri Nagu ni mwanamke ana uwezo wa kutekeleza ombi lake la kuwasafirisha wawekezaji kwa ndege hadi Songea ili wafike Ziwa Nyasa.
Amesema, si rahisi kwa mwekezaji kusafiri kwa gari umbali wa kilomita 1,200 hadi Ziwa Nyasa lakini wakienda kwa ndege hadi Songea, wataweza kuwekeza huko kwa sababu watasafiri kwa gari kilomita 80.
Komba amesema, uwanja wa ndege wa Songea ni mzuri kama wa Mwanza lakini hakuna ndege zinazokwenda huko.
Amewakaribisha Dk Nagu na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dk Cyril Chami, Songea, Ruvuma na Ziwa Nyasa.
Mbunge wa Kwela, Chrisant Mzindakaya, amesema, Dk Nagu, Dk Chami na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, Joyce Mapunjo, wanastahili kuiongoza Wizara hiyo.
Kwa mujibu wa Mzindakaya, Mapunjo ana uwezo mkubwa wa kusimamia mambo hivyo Wizara hiyo imepata kiongozi mzuri. Mbunge huyo ameyasema hayo leo wakati anachangia bajeti ya Wizara hiyo.
Mzindakaya amesema, amefanya utafiti wa uhakika na kubaini kwamba, Tanzania na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC) ndiyo nchi tajiri zaidi kwa rasilimali miongoni wa nchi za maziwa makuu.
Sasa uamuzi ni matumizi, mnavyoamua wenyewe kutumia amesema Mzindakaya na kusisitiza kwamba,Tanzania isiendelee kufanya kosa la kuuza bidhaa ghafi nje, iuze bidhaa zilizosindikwa.
Mbunge huyo amesema, Wizara za Viwanda,Biashara na Masoko, Maliasili na Utalii, Kilimo, Chakula na Ushirika, Fedha na Uchumi zinapaswa kuandaa mfumo wa kufanya kazi pamoja ili programu ya Kilimo Kwanza iwe na manufaa kwa Taifa.
Mzindakaya amesema, utekelezaji wa programu ya Kilimo Kwanza uende sanjari na kasi ya kuiimarisha sekta ya viwanda, na pia hamasa ya kukuza usindikaji iendane sambamba na kasi ya kuimarisha masoko ya bidhaa.
Kama halifanyiki hivyo tutaendelea kuwa watumwa kwa mambo mengine ambayo tunayaweza amesema Mbunge huyo.
Mbunge wa Mbinga Magharibi, Kapteni John Komba amemsifu Waziri wa Viwanda, Biashara na Masoko, Dk Mary Nagu, kuwa ana sura nzuri na anauzika.
Mbunge huyo amelieleza Bunge leo kwamba, yupo tayari kutunga wimbo wa kumsifu Waziri huyo.
Kabla ya kutoa sifa hizo, Kapteni Komba alisema bungeni mjini Dodoma kwamba, Dk Nagu leo kapendeza kuliko siku nyingine zote.
Mbunge huyo ametoa sifa hizo wakati anachangia bajeti ya Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko iliyowasilishwa leo bungeni.
Komba amesema, pamoja na sifa za uzuri wa sura na kuuzika, kwa kuwa Waziri Nagu ni mwanamke ana uwezo wa kutekeleza ombi lake la kuwasafirisha wawekezaji kwa ndege hadi Songea ili wafike Ziwa Nyasa.
Amesema, si rahisi kwa mwekezaji kusafiri kwa gari umbali wa kilomita 1,200 hadi Ziwa Nyasa lakini wakienda kwa ndege hadi Songea, wataweza kuwekeza huko kwa sababu watasafiri kwa gari kilomita 80.
Komba amesema, uwanja wa ndege wa Songea ni mzuri kama wa Mwanza lakini hakuna ndege zinazokwenda huko.
Amewakaribisha Dk Nagu na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Dk Cyril Chami, Songea, Ruvuma na Ziwa Nyasa.
Mbunge wa Kwela, Chrisant Mzindakaya, amesema, Dk Nagu, Dk Chami na Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Masoko, Joyce Mapunjo, wanastahili kuiongoza Wizara hiyo.
Kwa mujibu wa Mzindakaya, Mapunjo ana uwezo mkubwa wa kusimamia mambo hivyo Wizara hiyo imepata kiongozi mzuri. Mbunge huyo ameyasema hayo leo wakati anachangia bajeti ya Wizara hiyo.
Mzindakaya amesema, amefanya utafiti wa uhakika na kubaini kwamba, Tanzania na Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Watu wa Kongo (DRC) ndiyo nchi tajiri zaidi kwa rasilimali miongoni wa nchi za maziwa makuu.
Sasa uamuzi ni matumizi, mnavyoamua wenyewe kutumia amesema Mzindakaya na kusisitiza kwamba,Tanzania isiendelee kufanya kosa la kuuza bidhaa ghafi nje, iuze bidhaa zilizosindikwa.
Mbunge huyo amesema, Wizara za Viwanda,Biashara na Masoko, Maliasili na Utalii, Kilimo, Chakula na Ushirika, Fedha na Uchumi zinapaswa kuandaa mfumo wa kufanya kazi pamoja ili programu ya Kilimo Kwanza iwe na manufaa kwa Taifa.
Mzindakaya amesema, utekelezaji wa programu ya Kilimo Kwanza uende sanjari na kasi ya kuiimarisha sekta ya viwanda, na pia hamasa ya kukuza usindikaji iendane sambamba na kasi ya kuimarisha masoko ya bidhaa.
Kama halifanyiki hivyo tutaendelea kuwa watumwa kwa mambo mengine ambayo tunayaweza amesema Mbunge huyo.