Bonde la Baraka
JF-Expert Member
- Sep 22, 2016
- 4,580
- 7,938
Habari wadau!
Zifuatazo ni baadhi ya sera atakazotumia Mh. Rais kuomba ridhaa ya watanzania kuingia ikulu kwa mara nyingine tena;
1. "Ndugu zangu Watanzania nimetumia kipindi changu cha miaka 5 kutengeneza Tanzania iliyoibiwa, iliyoharibika , nchi hii ilioza sana na sasa kazi iliyobaki ni kuleta furaha na maisha mazuri , naomba mnipe kura nikamalizie kazi mliyonituma"
2. "Sakata la makinikia sasa nishalishughulikia na wapo katika hatua za kukamilisha malipo yetu ya matrilioni, naomba nipeni ruhusa ya kumalizia zoezi hili ili wasije watu wasio na uchungu na taifa hili wakaharibu kazi nzuri tuliyoifanya CCM awamu ya 5"
3. "Nimeondoa viongozi wazembe, mafisadi na wala rushwa, sasa nidhamu serikalini imerudi, nimeondoa wafanyakazi hewa maelfu kwa maelfu, nimeondoa wafanyakazi wasio na sifa wenye vyeti feki na sasa kazi iliyobaki ni kuwapa furaha watumishi wa umma nao waache kupanda daladala, waendeshe magari yao, walale kwenye nyumba nzuri."
4. "Tumeshaanza utekelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa ya standard gauge, ujenzi ulisuasua kwakuwa tulikuwa tunatafuta fedha za kukamilisha ujenzi haraka, na nimezipata na natarajia kuanza kujenga kutoka Dar es salaam mpaka Dodoma haraka mapema mwa mwakani , ndugu zangu nipeni nafasi nimalizie kazi hii "
Hii imekaa kama comedy hivi ila ndivyo itakavyokuwa kama tu Mungu akatupa uzima.
Zifuatazo ni baadhi ya sera atakazotumia Mh. Rais kuomba ridhaa ya watanzania kuingia ikulu kwa mara nyingine tena;
1. "Ndugu zangu Watanzania nimetumia kipindi changu cha miaka 5 kutengeneza Tanzania iliyoibiwa, iliyoharibika , nchi hii ilioza sana na sasa kazi iliyobaki ni kuleta furaha na maisha mazuri , naomba mnipe kura nikamalizie kazi mliyonituma"
2. "Sakata la makinikia sasa nishalishughulikia na wapo katika hatua za kukamilisha malipo yetu ya matrilioni, naomba nipeni ruhusa ya kumalizia zoezi hili ili wasije watu wasio na uchungu na taifa hili wakaharibu kazi nzuri tuliyoifanya CCM awamu ya 5"
3. "Nimeondoa viongozi wazembe, mafisadi na wala rushwa, sasa nidhamu serikalini imerudi, nimeondoa wafanyakazi hewa maelfu kwa maelfu, nimeondoa wafanyakazi wasio na sifa wenye vyeti feki na sasa kazi iliyobaki ni kuwapa furaha watumishi wa umma nao waache kupanda daladala, waendeshe magari yao, walale kwenye nyumba nzuri."
4. "Tumeshaanza utekelezaji wa ujenzi wa reli ya kisasa ya standard gauge, ujenzi ulisuasua kwakuwa tulikuwa tunatafuta fedha za kukamilisha ujenzi haraka, na nimezipata na natarajia kuanza kujenga kutoka Dar es salaam mpaka Dodoma haraka mapema mwa mwakani , ndugu zangu nipeni nafasi nimalizie kazi hii "
Hii imekaa kama comedy hivi ila ndivyo itakavyokuwa kama tu Mungu akatupa uzima.