Hizi ndio sababu za kutofunga mipaka na kuweka movement restrictions

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,888
143,985
Hizi ndio baadhi ya sababu alizotaja Bwana mkubwa za kutofunga mipaka/kuwa na lockdown

1.Ambulance zitashindwa kusafirisha wagonjwa
2.Ujenzi wa SGD utakwama
3.Ujenzi wa Stieglers Gorge utakwama
4.Mizigo haitasafirishwa kupitia bandari ya Dar-es-salaam na hivyo tutakosa mapato
5.Nchi zinazotuzunguka na zinazotegemea bandari yetu kusafirisha mizigo zitaathirika na kwamba tungewaua kama tungefunga mipaka.
6.Vifaa vya kutengeneza mabarabara visingesafirishwa

Hayo ni baadhi niliyoyakumbuka baada ya kumsikia akiongea kupitia TBC1 katika kipindi cha "JAMBO" asubuhi hii na kasisitiza watu wachape kazi na kwamba corona isitumike kama kisingizio ila akasisitiza tuchukue tahadhari.

Sasa sijui ni kwanini ile Press release haijataja baadhi ya haya aliyoyatamka.
 
Hizi ndio baadhi ya sababu alizotaja Bwana mkubwa za kutofunga mipaka/kuwa na lockdown

1.Ambulance zitashindwa kusafirisha wagonjwa
2.Ujenzi wa SGD utakwama
3.Ujenzi wa Stieglers Gorge utakwama
4.Mizigo haitasafirishwa kupitia bandari ya Dar-es-salaam na hivyo tutakosa mapato
5.Nchi zinazotuzunguka na zinazotegemea bandari yetu kusafirisha mizigo zitaathirika na kwamba tungewaua kama tungefunga mipaka.
6.Vifaa vya kutengeneza mabarabara visingesafirishwa


Hayo ni baadhi niliyoyakumbuka baada ya kumsikia akiongea kupitia TBC1 katika kipindi cha "JAMBO" asubuhi hii na kasisitiza watu wachape kazi na corona isitumike kama kisingizio ila akasisitiza tuchukue tahadhari.

Sasa sijui ni kwanini ile Press realease haijataja baadhi ya haya aliyoyatamka.

Mods kama mtafuta au kuunganisha huu uzi,basi wawekeni watu clip ya alichosema.
Uhai wa watu ni bora kuliko hivyo alivyo vitaja
 
Uhai wa mwananchi ni muhimu kuliko vitu vyote hivyoo
Hao Marekani na Kenya na wengine waliojifungia ndani mbona rate ya maambukizi ndio inazidi kuongezeka?? US walivyoanza kujifungia zilikuwa cases chache sana, sasa hivi wako half a million na bado wameongeza mwezi zaidi
 
Nchi zinazojali raia wake zimetoa kipaumbele kwa uhai wa raia kuliko mapato ya nchi. Raia ndiyo uchumi wenyewe. Ukipoteza raia STandard gauge unamjengea nani?
Ng'ombe na mbuzi wasafiri salama bila shida wala mikwaruzo. Mabehewa yaliyoterekezwa mwanza, dodoma na kila mahali yatasafirisha ili tupate pesa za waarabu wakati tumeishatangulia kuzimu. Amuulize PM wa UK aliupataje.
 
12 Reactions
Reply
Back
Top Bottom