Hizi ndio adhabu mbili kubwa kama wasusiaji wataendelea kususia

state agent

JF-Expert Member
Jul 1, 2019
1,764
2,511
Wana ukumbi!

Baada ya vyma vya NCCR Mageuzi,Chama Cha ukombozi wa Umma(CHAUMA) Na kile cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kukaidi amri halali ya waziri wa TAMISEMI mh Suleiman Jafo ya kuwaruhusu wanachama wao waliomba ridhaa ya ugombezi imebainika kuwa hizi ndio adhabu mbili kuu ambazo vyama hivyo vyaweza kukumbana nazo:

1. Hukumu ya kiserkali

Kuzuiliwa ruzuku
Juzi mh rais amemuapisha CAG Mpya na moja ya kazi zake ni kupitia upya ufisadi mkubwa kwenye vyama vya siasa hasa baada ya vyama vingi kupata hati chafu kwa miaka mingi .Vyama vinapokea pesa nyingi lakini hazitumiki ipasavyo kwani moja ya matumizi ni kufanyia kampaini za chaguzi hii kuu mbili ule wa TAMISEMI na ule mkuu kwa maana hiyo CAG tamwandikia batua msajili wa vyama juu ya kadhia hii na msajili atasitisha ruzuku Mara moja .

2.
Hukumu ya wananchi 2020
Sisi tutakuwa tuanahudumiwa na makada wa chama tawala CCM mpaka 2020 hadi 2024 kimsingi tutakuwa tumesha waelewa CCM na hivyo kuwaona ndio watu wetu na kuwasahau kabisa upinzani maana hawatahusika na

a/barua za udhamini hasa mikopo,manunuzi kama viwanja na nyumba,udhamini wa kijinai,

b/wadau wa maendeleo mtaani na vijijini

c/ michezo na utamaduni

Huku ndiko kura hukea na sisi tutwaadhibu hawa walitusaliti


State agent
 
John Shibuda akiiasa CCM, nanukuu " Nyama ya kitimoto hata uitie viungo kibao bado itabaki kuwa haramu kwa wanaoamini" mwisho wa kumnukuu Mzee Shibuda. TAMISEMI na CCM ya awamu ya tano mjue hilo na linaonekana dhahiri ktk wananchi kususia uchaguzi haramu wa serikali za mitaa na vijiji.

Sheria mpya ya vyama vya siasa inaidhalilisha CCM - Shibuda
 
Nimekudharau saana na kama wewe ndiyo wana ccm wenzetu tulio wapa imani ya kukiongoza chama basi ni hasara kubwa saana . Juzi niliandika uzi humu ukajifanya unakosoa kijinga kumbe hata mwisho wako wa kuona ni mbura hati tuu. Daa pole saana.

 
Ile mihuri huwa inaandikwa serikali za mtaa wa CCM? Halafu muwaambie waache kudai dai buku tano za mihuri.

Ina maana kila tusiofungamana na upande wowote au hata hao wapinzani hawaruhusiwi kipewa huduma za kiserikali kwa kuwa sio CCM?

Na hvyo basi muache kupokea kodi za wasiokua CCM...mlipe wenyewe ili ziwanufaishe nyie...

Hovyo kabisa.
 
state agent usitishe watu, kama mna uwezo futeni kabisa hivi vyama, mbaki na vile 11 mvibebe bebe kuhadaa ulimwengu muone kama mtaweza. Mmefanya mlicho fanya mkazani mmeshinda lakini matokeo yake mnahaha humu kwa kuwa mmefumaniwa mkilawiti demokrasia. KAMA SIO KWELI KELELE HIZI za nini? Na leo utakesha humu mana tangu asubuhi nikichungulia humo tu,
 
Well said mkuu100%

Tatizo la nchi hii wanasiasa wengi wa upinzani wametokana na makundi makuu mawili.

1=waliokuwa ccm na kuhitilafiana huko na hatimae kuenguliwa na baada ya mfumo wa vyama vingi wakatumia fursa hiyo kurudi ulingoni lakini wakiwa na sumu zaidi ya uanasiasa safi.

2=wanafunzi wa kada mbalimbali waliokuwa wakaidi wakiongoza migomo katika taasisi mbalimbali za kielimu nchini.
Walipomaliza vyuo na kutokuwa material nzuri za kupata ajira wakatumia short cut kisiasa kuukwea ubunge kwenye hivyo vyama vyao.
Hivyo hawa sio leadership materials bali wahuni fulani hivi.

Mifano ni kama huyu halima mdee mama wa msuba yeye all the time kinywa kimejaa matusi iwe bungeni,mitandaoni na popote pale.

Wengine wote ukiorodhesha humu nadhani mnawajua na wananchi as the whole mnawaona kila siku.

Halafu genge hili ndio linataka kuongoza nchi ya watu milioni hamsini na tano?

NO ! TUACHENI UTANI,NAIPENDA NCHI YANGU KWA SANA.
 
masoudkipanya_B4o0u68j7Kl.jpeg
 
Kibajaji mbona ana matusi nje nje hana tofauti na huyo halima imekuaje mmempa uongozi.

We nae ndo wale wale...ikitokea unapoishi uongozi akapata asiyekua ccm na wewe pia usipewe huduma za kijamii??? Mbona akili zenu finyu sana.
 
Fanya hivi, wekeni na adhabu ya kuwapiga risasi viongozi wote wa upinzani watakaogoma kushiriki uchaguzi, zoezi hili mulifanyie hapo uwanja wa taifa kisha wananchi wote wazalendo waje kushuhudia. Tena safari hii muwatume wale wale mliowatuma kumpiga Lissu risasi. Ila muwape masharti wasikosee shabaha kama kwa Lissu, maana safari hii mtalifanya zoezi hilo kisheria.
 
Back
Top Bottom