Hizi kumbukizi za Mwl Nyerere kila mchangiaji anakosoa utawala huu, Kwanini sasa?

Wewe ungeweza kuyasema haya uliyoyaandika mbele ya Magufuli?! Inaonekana anatisha sana.

Kuna wakati aliwaita viongozi wastaafu woote ikulu, akawaambia WAMUACHE AFANYE ATAKAVYO , KAMA WAO WALIVYOFANYA WAKATI WAO.
Na aliwakumbusha WAACHE KUWASHWA WASHWA.

Tangu siku hiyo kimyaaaa, tunawasikia kwenye kumbukizi za Mwl Nyerere wanapumua utadhani wana pumu, vifua vimewajaa wanagombea mic.

Kwanini wasiite press waka sema tu,, wanaogopa nini?! Au nao wanashughulikiana au kushughulikiwa?!
Wana madudu mengi anayoyafahamu Magufuli. Na wanajua hana staha, atayatangaza madudu hayo mbele za wananchi.

Mwalimu aliweza kusema chochote bila ya hofu kwa sababu hakuwa na 'kabati lililojaa mifupa.'
 
Wana madudu mengi anayoyafahamu Magufuli. Na wanajua hana staha, atayatangaza madudu hayo mbele za wananchi.

Mwalimu aliweza kusema chochote bila ya hofu kwa sababu hakuwa na 'kabati lililojaa mifupa.'
Hahaha hivyo ni ukweli wanamuogopa, na hawawezi kusema ukweli dhidi ya yanayoendelea.

Basi kama makabati yao yamejaa mafupi na nyama, waache kujidai wao ni akina mr clean, na waache kukosoa wakae kimya.

Hivyo hakuna anayeweza kusema Magufuli kinaga ubaga, nje ya kumbukizi za Mwl Nyerere, wamebaki kujikinga huko na kutafuta hadhara kujitutumua kumbe Magufuli kawashika wote, na mauchafu yao.
Bora hata Mkapa aliyeamua kutokusema chochote kwenye kumbukizi, nimeona na kuwasikia wengi, kumbe wanafiki na watafuta cheap popularity.
 
MKWERE is very smart. Kukanusha kule Ni kutupa signal kuwa ujumbe umefika na mzee wa kujimwambafai kachukia hivyo points zote tatu kachukua MKWERE.
Kwa mimi bila kujali uchama wa mtu yeyote ile hotuba ya Mkwere inabaki kuwa ni Kati ya hotuba Bora za mwaka 2019 ambayo itadumu na kutumika kama reference katika mambo ya siasa zetu huko mbeleni Kama vile wanasiasa wa Sasa wanavyotumia hotuba za Mwalimu JKN
 
Akosolewe na nani wakati wa kumkosoa wote ni mbumbu!!!!!!HV hao wanaojiita wakosoaji wakati taifa letu linaporomoko kiuchumi nyakati zilizopita hawakuwepo?mbona nchi iliharibikia mikononi mwao Leo hii wanataka kimshauri nn Rais au ndo wanataka kumpa mbinu za kushindwa kama wao?JPM omba ushauri hata kwa Kagame lkn sio watanzania hatujiwezi kifikira.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom