Hizi kauli za mkoa wangu, wilaya yangu, halmashauri yangu, manispaa yangu, zimekaaje?

wwww

JF-Expert Member
Mar 20, 2012
350
252
Ndugu wanaJF,

Kumekuwa na kauli mbalimbali za baadhi ya viongozi kutoa matamko mfano; Wakuu wa Mikoa, Wilaya au Wenyeviti/ Mameya wa Halmashauri/Manispaa kwamba ni Marufuku kufanya kitu fulani kwenye eneo lake la utawala kwa kuita, MKOA WANGU, WILAYA YANGU, HALMSHAURI YANGU, MANISPAA YANGU n.k.

Hii kauli imekuwa ikinisikitisha sana mimi hasa ninapomsikia kiongozi kama Mkuu wa Mkoa anaita Mkoa ni wake eti kisa tu kapewa dhamana ya kuuongoza. Hivi hawa wanajua maana ya dhamana? Hivi mtu kama Paul Makonda anaweza kuumiliki mkoa wa Dar-es-salaam ukawa wake kweli, au nikutojitambua?

Nimewasikia watawala wengi tu kama Morogoro, Iringa na kwingineko na leo mkuu wa Mkoa mwingine kule Kigoma mwanajeshi mstaafu wa JWTZ naye eti anaumikili mkoa wa Kigoma hivyo anapiga marufufu shughuli za kisiasa kwenye mkoa wake. KWELI?

Inawezekana naye Rais wetu mpendwa sana JPM akajimilikisha nchi yetu ya Tanzania na kuanza kupiga marufuku mtu yeyote kufanya kitu chochote kwenye nchi yake mpaka pale yeye atakapoamue vinginevyo.

Wanajf naomba tujadili maana hawa jamaa wananitia kichefuchefu sana mimi kwa kujimilikishwa himaya zetu kirahisi rahisi tu.
 
"Tanzania ya Magufuli itakuwa ni Tanzania ya viwanda"

Kiongozi ni mtumishi. Hana umiliki wowote zaidi ya madaraka aliyopewa kwa muda tu.

Nakuomba kauli zisikupe shida ili mradi wanatekeleza utawala wa sheria.
 
Ndugu wanaJF,

Kumekuwa na kauli mbalimbali za baadhi ya viongozi kutoa matamko mfano; Wakuu wa Mikoa, Wilaya au Wenyeviti/ Mameya wa Halmashauri/Manispaa kwamba ni Marufuku kufanya kitu fulani kwenye eneo lake la utawala kwa kuita, MKOA WANGU, WILAYA YANGU, HALMSHAURI YANGU, MANISPAA YANGU n.k.

Hii kauli imekuwa ikinisikitisha sana mimi hasa ninapomsikia kiongozi kama Mkuu wa Mkoa anaita Mkoa ni wake eti kisa tu kapewa dhamana ya kuuongoza. Hivi hawa wanajua maana ya dhamana? Hivi mtu kama Paul Makonda anaweza kuumiliki mkoa wa Dar-es-salaam ukawa wake kweli, au nikutojitambua?

Nimewasikia watawala wengi tu kama Morogoro, Iringa na kwingineko na leo mkuu wa Mkoa mwingine kule Kigoma mwanajeshi mstaafu wa JWTZ naye eti anaumikili mkoa wa Kigoma hivyo anapiga marufufu shughuli za kisiasa kwenye mkoa wake. KWELI?

Inawezekana naye Rais wetu mpendwa sana JPM akajimilikisha nchi yetu ya Tanzania na kuanza kupiga marufuku mtu yeyote kufanya kitu chochote kwenye nchi yake mpaka pale yeye atakapoamue vinginevyo.

Wanajf naomba tujadili maana hawa jamaa wananitia kichefuchefu sana mimi kwa kujimilikishwa himaya zetu kirahisi rahisi tu.


Kama unataka kumpima Makonda anaumiliki mkoa Dar na watu wake kaidi amri zake na utangaze wazi wazi. Mfano vuta sigara sehemu za wazi aswa ukiwa mbele ya Ofisi yake walau akuone ama pinga kufurushwa kwa mashoga. Usikilizie ndani ya saa 24 utakuwa wapi na uone kama kuna mtu mwingine atatoa amri ya kukutoa.
 
sasa aah ata mie hilo nshalizoea maana kule zenj watawala wametuambia tuhame hasa km tumeshindwa kuishi kwa watawala hawa viburi tutayaona mengi
 
Kuna mkuu wa Mkoa amekuja na kauli ya kusema hii ni sheria ya Mkoa wangu.
Tanzania kama taifa moja sheria zinazofuatwa ni kwa nchi nzima lakini hakuna sheria inayotekelezwa kwa Mkoa mmoja
Tumeona tamasha la Fiesta likifanyika katika mikoa yote nchini kwa huru na ushirikiano kutoka kwenye viongozi na idara za usalama za mikoa hizo.
Kwanini Mkuu wa Mkoa wa Dar Paul Makonda kusema kwenye Mkoa wake mwisho wa tamasha ni saa sita usiku. Mwaka Jana tuliona Tamasha la Fiesta likifanyika bila masharti yeyote.
 
Huwa nawaza tu hivi ndio anakuwa mkuu wa mkoa maisha yake yote au yaan sipati picha tu ni mawazo yangu tu lakini
 
Tujadili hoja,Madaraka mikoani yanatofautiana na mtazamo wako.mfano baadhi ya miji kama Moshi ukitupa taka ovyo ni makosa kisheria ingawa morogpro haiko hivyo. Zinaitwa by law aka sheria Mahalia.
 
Lakini huyu brother neno wangu limemkaa sana kichwani na haipendezi kiongozi kuwa mbinafsi, suala la uongozi ni jambo shirikishi ndio maana watu wenye hekima utawasikia wakisema ktk kipindi chetu tumefanya haya na yale. Kamwe hasemi ktk kipindi changu. Yani hata ukiangalia video fupi ktk account yake ya instagram anasema madaktari wangu kutoka China. Yani nimecheka mpaka basi
 
Kwakuwa yupo DSM anahaki ya kusema Mkoa wangu., unafikiri angekuwa Mkoa mpya wa Simiyu angesema Mkoa wangu?
 
Lakini huyu brother neno wangu limemkaa sana kichwani na haipendezi kiongozi kuwa mbinafsi, suala la uongozi ni jambo shirikishi ndio maana watu wenye hekima utawasikia wakisema ktk kipindi chetu tumefanya haya na yale. Kamwe hasemi ktk kipindi changu. Yani hata ukiangalia video fupi ktk account yake ya instagram anasema madaktari wangu kutoka China. Yani nimecheka mpaka basi
Wizara ya Afya imekuwa kimya kwenye kusimamia na kuratibu ugeni wa hawa madaktari
 
walimu wangu, madaktari wangu, wakuu wangu wa wilaya... Baada ya siku zake za uongozi kuisha atapata shida sana bashite..
 
Kuna mkuu wa Mkoa amekuja na kauli ya kusema hii ni sheria ya Mkoa wangu.
Tanzania kama taifa moja sheria zinazofuatwa ni kwa nchi nzima lakini hakuna sheria inayotekelezwa kwa Mkoa mmoja
Tumeona tamasha la Fiesta likifanyika katika mikoa yote nchini kwa huru na ushirikiano kutoka kwenye viongozi na idara za usalama za mikoa hizo.
Kwanini Mkuu wa Mkoa wa Dar Paul Makonda kusema kwenye Mkoa wake mwisho wa tamasha ni saa sita usiku. Mwaka Jana tuliona Tamasha la Fiesta likifanyika bila masharti yeyote.
Nyumbani kwangu
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom