Hazard CFC
JF-Expert Member
- Apr 7, 2015
- 16,615
- 38,588
Habari zinazosambaa hadi hivi mjini Morogoro ni hofu ya kupotea kwa bondia maarufu nchini mkazi wa Morogoro Francis Cheka.
Kwa mujibu wa watoa habari na marafiki wa karibu wa Bondia huyo ni kwamba eneo ilipotokea ajali ya lori la mafuta hapo msamvu ni jirani kabisa na “ofisi” yake iliyokuwa ikijihusisha na ununuzi wa chupa na madumu ya plastics yaliyokwisha tumika!
Habari zaidi zinasema bondia huyo alionekana katika eneo la ajali wakati wananchi wakipigania kuchota na kuzoa mafuta yaliyomwagika kutoka kwenye tanker hilo la mafuta ya petrol; Baada ya kutokea mlipuko wa moto kufuatia mafuta kushika moto hakuna aliyemuona Francis Cheka tena!!!
Mpaka sasa hivi ninapoandika taarifa hii Bondia Francis Cheka hapatikani nyumbani kwake, wala simu yake au mwili wake!! Huku marafiki zake wakiwa katika majonzi makubwa sana kwani inasemekana alienda katika koki iliokuwa ikitoa mafuta ili kuwazuia watu wasihatarishe maisha yao kabla Moto haujalipuka.
Sisi wapenzi wa Bondia huyu tunaliomba jeshi la polisi kusaidia kupata ukweli wa taarifa hii ya kusikitisha sana!!!
Kwa mujibu wa watoa habari na marafiki wa karibu wa Bondia huyo ni kwamba eneo ilipotokea ajali ya lori la mafuta hapo msamvu ni jirani kabisa na “ofisi” yake iliyokuwa ikijihusisha na ununuzi wa chupa na madumu ya plastics yaliyokwisha tumika!
Habari zaidi zinasema bondia huyo alionekana katika eneo la ajali wakati wananchi wakipigania kuchota na kuzoa mafuta yaliyomwagika kutoka kwenye tanker hilo la mafuta ya petrol; Baada ya kutokea mlipuko wa moto kufuatia mafuta kushika moto hakuna aliyemuona Francis Cheka tena!!!
Mpaka sasa hivi ninapoandika taarifa hii Bondia Francis Cheka hapatikani nyumbani kwake, wala simu yake au mwili wake!! Huku marafiki zake wakiwa katika majonzi makubwa sana kwani inasemekana alienda katika koki iliokuwa ikitoa mafuta ili kuwazuia watu wasihatarishe maisha yao kabla Moto haujalipuka.
Sisi wapenzi wa Bondia huyu tunaliomba jeshi la polisi kusaidia kupata ukweli wa taarifa hii ya kusikitisha sana!!!