Shark
JF-Expert Member
- Jan 25, 2010
- 29,459
- 29,152
Habari Wana jamvi na JF Kwa ujumla, natumai kama unaweza soma na kupitia Uzi huu hapa leo tarehe 06 mwezi wa 04, 2022 ina maana upo hai na unapumua kwa kudra za Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema.
Wakati wa awamu ya Serikali ya Tano chini ya JPM tuliona, kusikia na kusoma mengi jinsi wale waliosemwa Mafisadi wa nchi hii namna walivyokuwa wanakiona cha moto. Kuanzia wale waliojiuzia viwanda vya Serikali, biashara za zamani za Serikali mpaka wale ambao walikuWa na majengo Kila mkoa wakiamriwa kusalimisha Serikalini. Ni kweli awamu ile ilikuwa na mapungufu mengi lakini pia ilikuwa na mazuri vilevile.
Ila sasa kwa awamu hii ya sita tumeona wakija na madai mbalimbali pamoja na kupanda holela kwa vitu ambapo huku mtaani inasemwa ni wale Mafisadi wanarudisha hela zao zilizochukuliwa. Kwa mfano mdau mmoja kijiweni anasema yule Kanali ambae ni makamu mwenyekiti wa chama alisalimisha 3 trilioni kati ya 4 kwa Serikali ya awamu ya 5 ya JPM. Pia mtoto wa msoga wanasema yupo pale kwenye Wizara ya Ardhi kimkakati na siyo bahati mbaya.
Kama hayo yasemwayo ni kweli chondechonde awamu hii acheni mnayofanya maana watu wa sasa wapo macho na wanajua.
Wakati wa awamu ya Serikali ya Tano chini ya JPM tuliona, kusikia na kusoma mengi jinsi wale waliosemwa Mafisadi wa nchi hii namna walivyokuwa wanakiona cha moto. Kuanzia wale waliojiuzia viwanda vya Serikali, biashara za zamani za Serikali mpaka wale ambao walikuWa na majengo Kila mkoa wakiamriwa kusalimisha Serikalini. Ni kweli awamu ile ilikuwa na mapungufu mengi lakini pia ilikuwa na mazuri vilevile.
Ila sasa kwa awamu hii ya sita tumeona wakija na madai mbalimbali pamoja na kupanda holela kwa vitu ambapo huku mtaani inasemwa ni wale Mafisadi wanarudisha hela zao zilizochukuliwa. Kwa mfano mdau mmoja kijiweni anasema yule Kanali ambae ni makamu mwenyekiti wa chama alisalimisha 3 trilioni kati ya 4 kwa Serikali ya awamu ya 5 ya JPM. Pia mtoto wa msoga wanasema yupo pale kwenye Wizara ya Ardhi kimkakati na siyo bahati mbaya.
Kama hayo yasemwayo ni kweli chondechonde awamu hii acheni mnayofanya maana watu wa sasa wapo macho na wanajua.