Hizi Adhabu kumbe bado zipo!

Power G

JF-Expert Member
Apr 20, 2011
3,886
1,193
Wana JF, kuna adhabu ambazo kwa muda nimekuwa nikizisikia katika msimulizi ya watu kama vile za kukatwa mikono, kukatwa vichwa na kupigwa mawe hadi kufa. Mara zote nimekuwa nikizichukuliwa kama hadithi, kumbe ni kweli zipo mpaka leo na kesho. Tafadhali fuatana nami nikuhabarishe.

Jana tarehe 12/10/2011 nilikuwa shughuli kidogo katika mji wa Jeddah nchini Saudia. Mnamo saa 5 asubuhi nikiwa kwenye gari nikielekea wizara ya mambo ya nchi za njema wakati tunakaribia eneo moja linaloitwa Balad (historic town) magari yote yalisimamishwa kukawa kunapita msafara mkubwa sana wa magari ya polisi yakiwa na vimulimuli na ving'ora na moja lililoonekana kama la kiraia aina ya Jeep nyekundu. Kwa mawazo yangu nilidhani ule msafara ungekuwa wa "kikwete" wa nchi hii. Msafara ulitangulia na siye tukawa kwenye msululu wa magari kwa nyuma.

Msafara uliishia kwenye Msikiti mkubwa sana ambao uko opposite na wizara ya mambo ya nje. Watu maelfu kwa maelfu toka pande zote walikuwa wakimiminika kuelekea kwenye eneo hilo huku kukiwa na ulinzi mkali wa magari mengine yakiwa mounted na machine guns. Katika ile Jeep nyekundu alishuka askari mmoja mwenye nyota 3 akiandamana na kijana mmoja mwenye umri kama wa miaka 30 hivi akiwa amevaa kanzu. Kijana alipelekwa moja kwa moja mpaka kwenye kijukwaa ambacho kinaonekana kipo siku zote kwa ajili ya shughuli maalum.

Saa 5 na dk 5, yule askari alimfunga kitambaa yule kijana kwenye macho kisha akaamuliwa apige magoti. Baada kama ya dak 2 aliongezeka mtu mwingine kwenye jukwaa ambaye anaonekana ana umbo la kushiba hasa naye akiwa amevaa kanzu nyeupe. Askari mwingine alitokea akiwa na jambia lenye umbo la mwezi mchanga lililokuwa kwenye ala nyeupe akamkabidhi yule jamaa mwenye kanzu aliyekuwa jukwaani. Huyu jamaa alichomoa jambia akalinyanyua kwa mkono wake wa kushoto na kulishusha mara moja sawia katika shingo ya huyo kijana na kichwa kikaruka mbali na kiwiliwili huku watu wakishangilia ikiwamo na watoto wadogo. Kutokana na ulinzi uliokuwapo sikuweza hata kuweza kupiga picha walao kwa simu.

Katika mazungumzo niliwasikia watu wakisema ni mharifu, lakini sikuweza hata kufuatilia kosa lake lilikuwa lipi. Ila adhabu ndiyo niliyoishuhudia. Kwa kweli hiyo picha imenisumbua sana kwenye mawazo hadi sasa.
 
Wana JF, kuna adhabu ambazo kwa muda nimekuwa nikizisikia katika msimulizi ya watu kama vile za kukatwa mikono, kukatwa vichwa na kupigwa mawe hadi kufa. Mara zote nimekuwa nikizichukuliwa kama hadithi, kumbe ni kweli zipo mpaka leo na kesho. Tafadhali fuatana nami nikuhabarishe.

Jana tarehe 12/10/2011 nilikuwa shughuli kidogo katika mji wa Jeddah nchini Saudia. Mnamo saa 5 asubuhi nikiwa kwenye gari nikielekea wizara ya mambo ya nchi za njema wakati tunakaribia eneo moja linaloitwa Balad (historic town) magari yote yalisimamishwa kukawa kunapita msafara mkubwa sana wa magari ya polisi yakiwa na vimulimuli na ving'ora na moja lililoonekana kama la kiraia aina ya Jeep nyekundu. Kwa mawazo yangu nilidhani ule msafara ungekuwa wa "kikwete" wa nchi hii. Msafara ulitangulia na siye tukawa kwenye msululu wa magari kwa nyuma.

Msafara uliishia kwenye Msikiti mkubwa sana ambao uko opposite na wizara ya mambo ya nje. Watu maelfu kwa maelfu toka pande zote walikuwa wakimiminika kuelekea kwenye eneo hilo huku kukiwa na ulinzi mkali wa magari mengine yakiwa mounted na machine guns. Katika ile Jeep nyekundu alishuka askari mmoja mwenye nyota 3 akiandamana na kijana mmoja mwenye umri kama wa miaka 30 hivi akiwa amevaa kanzu. Kijana alipelekwa moja kwa moja mpaka kwenye kijukwaa ambacho kinaonekana kipo siku zote kwa ajili ya shughuli maalum.

Saa 5 na dk 5, yule askari alimfunga kitambaa yule kijana kwenye macho kisha akaamuliwa apige magoti. Baada kama ya dak 2 aliongezeka mtu mwingine kwenye jukwaa ambaye anaonekana ana umbo la kushiba hasa naye akiwa amevaa kanzu nyeupe. Askari mwingine alitokea akiwa na jambia lenye umbo la mwezi mchanga lililokuwa kwenye ala nyeupe akamkabidhi yule jamaa mwenye kanzu aliyekuwa jukwaani. Huyu jamaa alichomoa jambia akalinyanyua kwa mkono wake wa kushoto na kulishusha mara moja sawia katika shingo ya huyo kijana na kichwa kikaruka mbali na kiwiliwili huku watu wakishangilia ikiwamo na watoto wadogo. Kutokana na ulinzi uliokuwapo sikuweza hata kuweza kupiga picha walao kwa simu.

Katika mazungumzo niliwasikia watu wakisema ni mharifu, lakini sikuweza hata kufuatilia kosa lake lilikuwa lipi. Ila adhabu ndiyo niliyoishuhudia. Kwa kweli hiyo picha imenisumbua sana kwenye mawazo hadi sasa.

Hicho ndicho kitu wenzetu wanakililia kwenye mahakama ya kadhi.
 
Adhabu kama hizo zinamfaa Rostam na kundi lake.

Nataman tungekuwa na mahakama ya kadhi.
 
Ni sawa na adhabu nyengine za kifo,,

Hata US si wanafanya kila siku!??
Hizo adhabu nyingine za kifo zinazofanywa katika nchi nyingine, sidhani kama zinatolewa hadharani hata mbele ya macho ya watoto wadogo.
 
Back
Top Bottom