KalamuTena
JF-Expert Member
- Jul 7, 2018
- 13,189
- 17,157
Wajamaica hawakufika huko kwa utashi wao.Hizo ndivo akili za kiafrica zilivo na ndio mana tuna fail sana, mbona watu weusi wa Jamaica na Haiti hawajavamiwa kwenye visiwa vyao wakaambiwa kwamba kule si pao kwa vile wao sio asilia?
Waafrica tunatakiwa tuache ubaguzi na ubinafsi.
Kwa kifupi tu, Zanzibar ipo kabla ya Tanganyika, Taifa la Zanzibar lilikuepo kabla ya Taifa La Tanganyika, Sasa watanganyika sijui wanapata wapi fikra kuwa Zanzibar ni milki yao. Na hilo ndio tatizo halisi la huu Muungano wetu, Watanganyika wanahisi Zanzibar ni milki yao, Kwanini wasiingie na Burundi na Rwanda wakasema zao pia? Kwanini wasiende Mauritius pia wakasema pao?
Hawakwenda kuvamia sehemu ya mtu yeyote, wao ni wahanga wa yaliyowatokea bila ya matakwa yao.
Unaposema Tanganyika haikuwepo una maana ardhi inayoitwa Tanganyika ilisombwa na kuletwa hapo na nani. Na hiyo ardhi ya Zanzibar hao walioikalia waliitoa wapi na kuisogeza karibu na ardhi inayojulikana sasa kama Tanganyika?
Mtatafuta kila njia ya kuhalalisha uvamizi wa eneo ambalo hamkupashwa kulivamia, lakini ukweli ni kuwa uvamizi ulifanyika na mliowavamia sasa hawataki muendelee kuwanyanyasa kwenye eneo mlilovamia.
Kama mnataka kukaa kwa amani, tulieni hakuna atakayewabughudhi, lakini kutaka kudai haki mahali ambapo hamkutumia haki kupakalia hapo sio sawa.
Burundi na Rwanda zingekuwa chini ya wahamiaji haramu toka mbali waliojitangazia eneo hilo kuwa mali yao, maeneo hayo yangekuwa halali ya Tanganyika kuyachukua kama wenyeji wa huko waliondolewa na wageni wavamizi wasijulikane waliishia wapi.
Wavamizi wa Zanzibar hawana tofauti yoyote na wale settlers wa kiingereza hapo Kenya na kule Rhodesia, ambayo sasa ni Zimbabwe.