Hivi "Young" ni sawa na "Yanga"?

Sio kweli kwamba wazawa walishindwa kutamka au kujua maana halisi ya neno young. Ukweli ni kwamba kuna muda ulifika kukawa na vuguvugu la vijana kutaka kuwaondoa wazee kwa kigezo cha neno "Young" . wazee wakawa wanalififisha neno hilo kwa kuliingiza yanga kama aka hivi na mpaka likazoeleka.
Faida ya kufanya hivyo team sasa ni ya wote wazee na hao "young africans"

nangu Mandokwa
 
Kule MPWAPWA kuna kilima wazungu wa kikoloni waliishi... VIEW HIGH... wagogo mpk leo wanatamka VING'AWE!
 
KAWE imetokana na COW WAY.... palipokuwa na TANGANYIKA PACKERS.... YOUNG kuwa YANGA.... sawa tu
 
Young sio yanga hata siku moja bora wangesema yang. Hapo sawa sio yanga labda tuulize wazee waseme maana ya yanga ni nini maana haliingii kwenye tafsiri sahihii

Young African (youngA) labda walifupisha na kulitamka Yanga
 
Nami nikuulize hivi Barcelona ni sawa na Barca?
Barca ni nick name kwao wala huwezi kulikuta kwenye vitu official kama time-table fixtures wala popote. Lakini Yanga linatumika kama official name kwenye taratibu nyingi za nchi, BMT na TFF
 
KAWE imetokana na COW WAY.... palipokuwa na TANGANYIKA PACKERS.... YOUNG kuwa YANGA.... sawa tu
Hapo sio penyewe, kwasababu kawe imebaki kuwa kawe sio cow way tena, yaani cow way haipo tena wala kawe haitwi cow way tena, hata carrier corps haipo tena ipo kariakoo, lakini Yanga na Young zote zipo kwenye makabrasha mbalimbali kwenye club, BMT na TFF. Tulitarajia Dar es Salaam Young African iwe DAYA kama kifupisho lakini sio Yanga
 
Yanga timu ya wananchi,kama wewe ni mwananchi na haupo yanga jitafakari. La sivyo katafute nchi yako
 
Yanga siyo jina rasmi,jina lililosajiliwa ni Young African Sports Club. Ukipenda unaongezea mwenyewe "Ze Citizen Team" na ukinogewa zaidi ongeza "mabingwa wa kihistoria"
Mbona nawasikia wakianza na neno Dar es Salaam, unataka kusema Dar es salaam haimo kwenye urasimi wa jina?
 
Mifano yako kama barca, the blues, the gunners haifani na Yanga kwa Young, ni heri wangeita greens, yellows, au vijana. Maana Yanga sio sio kifupi cha Young na wala sio Vijana. Yanga ni jina ambalo halina maana yoyote. The blues kwakuwa jezi yao ni Rangi ya blue, the gunners wanatunza ghala la silaha, Barca ni kifupi cha Barcelona, Yanga ni nini?
Mbona huelewi pamoja na jamaa kukujibu hapo kwamba yanga lilikuja kutokana na watu kushindwa kutamka Young?
 
Mbona huelewi pamoja na jamaa kukujibu hapo kwamba yanga lilikuja kutokana na watu kushindwa kutamka Young?
sawa, kama "watu" wameshindwa kutamka young je, na viongozi wa young, BMT, TFF wameshindwa kutamka young hivyo wakaamua kuwafuata walioshindwa kutamka?. kama ni hivyo ingebidi young itoweke kama zilivyotoweka cow way, carrier corps, follow on line = foleni, nk. Lakini huwezi kutumia both kilichokosewa na kisichokosewa kwenye documents na mawasiliano rasmi ya club. Hata bank, mahakamani, nk huwezi kutumia majina yaliyokosewa 9nicks) na yaliyosahihi interchangeably, huko ni kukiuka sheria.

Tunategemea hata ratiba ikipangwa TFF itamke Young African vs Mtibwa Sugar sio Yanga vs Mtimbwa. Tuache wananchi na vyombo vya udaku viandike Yanga, Barca, nk kwa sababu zao.

Utamsikia Katibu wa TFF akisema klabu ya Yanga imetozwa faini ya sh. 3,000,000 kwa kosa la kutokuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo. Kiuhalisia iliyotozwa hiyo faini sio Young African ni yanga ambayo haipo kisheria.
 
Mbona nawasikia wakianza na neno Dar es Salaam, unataka kusema Dar es salaam haimo kwenye urasimi wa jina?

Haipo. Unaiona Dar hapo?
 

Attachments

  • IMG_20190504_123255.jpg
    IMG_20190504_123255.jpg
    53.8 KB · Views: 15
Dar Young Africans ndiyo jina rasmi sio hili la Yanga. Ni sawa na the Blues, the Gunners, the Reds, Cosmo kwa iliyokuwa Cosmospolitans. Ilianza kwa sababu wapenzi hawakuweza kutamka kwa ufasaha Young Africans wakawa wanasema Yanga Afrika. Umekataa Barca kwa Barcelona bure tu. Hata simba ilipokuwa Sunderland tuliita "Sanda." Vitabu vya hiyo Yanga yako hata Klabuni ubao sharti uandikwe Dar Young Africans. Zamani akina Mshindo Mkeyenge, Abdul Masoud walikuwa wakitangaza mpira Yanga walikuwa wakiita Dar Young Africans. "Wasikilizaji mpira unapigwa kuelekea goli la Dar Young Africans!!!" Muulize mwanachama wa "Yanga" yoyote kwa msajili jina gani limeandikwa. Kama ni Yanga basi wamebadili majuzi tu.
Hilo ulilosema ndilo hasa linalotakiwa kutendwa. haya majina ya the blues, the Gunners, Reds sio majina yaliyokosewa lakini Yanga ni jina lililokosewa kabisa kwa kushindwa kutamka Young Africans. Hata viongozi wa Arsenal, Chelsea, Man EPL, hawawezi kupanga ratiba zao kwa kuandika The Blues vs Everton kama ilivyo kwa Yanga vs Green worriers
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom