Ukienda kwenye mabaa , shoo za promotions mbalimbali , disco , pubs ..kila mahali ni nyyegezi kwenda mbele.. mitaani watoto wanauimba kama wote......hata waheshimiwa wakiusikia huwa wanatingisha vichwa kwa furaha kama siyo kuruka ruka mfano Mhe. Naibu Spika , naona hata BASATA wenyewe huko mtaani watakuwa wanaukubali....sasa najiuliza huu mwimbo umepigwa marufuku kwenye matamasha ya Wasafi Festival tu au?? nimekumbuka hii ishu sababu niko hapa Nyerere square Dodoma kuna promotions ya Tigo inaendelea..wanashindana kucheza Nyegezi...Hongereni WCB kwa kutoka video chap chap kabala ya ban manake duh iko hewani sana kila mahali...ifike mahali tuache unafiki wadau