Wana nyumba zao+ za urithi wamepangisha.Wakuu habarini.
Mambo yanaendaje..
Wakuu awali ya yote natambua/mnatambua kuwa maisha ya mjini haswa ukiwa umepanga + ukiwa na watoto ni changamoto nzito.Hivyo inahitaji uchapakazi/utafutaji maisha yaende.
Wakuu jana asubuhi nikiwa naelekea kwenye harakati za utafutaji nikiangaza angaza macho huku na kule kuna wazee flani + vijana wamekaa kwenye kijiwe...nahisi walikuwa wakipata kahawa kama sio chai huku wakiendelea kuchambua hotuba ya juzi ya Mh Raisi.
Kilichonifanya mpaka nikaleta hii thread hapa niliporudi mida ya mchana... kwa sabbu nilipata emergence kidogo kuna kitu nilisahau....sasa ile kuangaza macho formation ni ile ile niliyoiacha asubuhi(wazee flani na kofia zao) huku wakicheza draft.
Ilinipa tafakari kidogo nikajiuliza hivi hawa jamaa hadi jioni watakuwepo?...Cha ajabu Ile niliporudi mida ya kumi na mbili hivi na alama formation ni ile ile,Ila nahisi kuna baadhi ambao ni wachache nahisi walipungua( japo formation ni ile ile) niliowakumbuka kuna wazee wanne hivi waliokuwa wamevalia kofia,rasi,big na wengine kama sita hiv.
Hao wazee wanne niliwamark toka asubuhi kwa sabbu ya kofia zao,ila hao wengine niliwamark mchana japo nahsi tangu asubuhi walikuwepo.
Ok.sasa wakuu lengo langu sio kutangaza life style ya mtu humu/kufuatilia na pia sitarajii kwa sabbu sipendi majungu + umbeya ila kwa sabbu humu ni jamii pana na hatutambuani nina imani may be kuna jinsi wenzetu wanarelax na maisha ilihali wengine tunasota.
Sasa Jee wanayaendesha vipi maisha ya hapa mjini? au wamewekeza? Na hata kama wamewekeza nahisi sio kwa idadi ile niliyo iona.
Kweli kweli..Muhimu sana.Mind your own business
Oooh sawa sawa..ndio maana asubuhi mpaka jioni wamejiachia.Wana nyumba zao+ za urithi wamepangisha.
Vile vile wengine madalali, na pia wake zao ndio wanaopambana kuuuza chakula usiku, na vitafunwa kama maandazi, mihogo, kalimati n.k
Tunakopa kimya kimya kikubwa tu survive
kiukweli hawajawahi.. na sitarajiiHata hapa jukwaani tuna soma, comments na ku-like 24/7...
Sasa sijui tunapataje bando na mambo mengine... Vipi hao wazee hapo mtaani walishakuja kuhemea kwako kwa kibaba cha Unga?
Ok Mkuu..Jiongeze, Hao ni wenye nyumba. Hata asipofanya kazi kwa mwezi lazima ashibe.
Hahahah..kweli mzee babaUkitoka mkoani utashangaa maisha ya watu wa pwani.Na wewe ukijifanya mtu wa pwani wakati ni wa mkoani umeisha.
Sent from my SM-G920F using JamiiForums mobile app
Mjini hapa mzee,Oooh sawa sawa..ndio maana asubuhi mpaka jioni wamejiachia.
Ok,Ahsante Mkuu ila kuna watu wanarizika mapema sana.
Ila Mkuu kwa upande wa pili kwa idadi niliyoiona nina wasiwasi sio wote wana nyumba za urithi kama unavyodai. Au unasemaje Chief
Tangu mwaka uanze leo hii point umeitoa bhana:;:; 100%Mind your own business
Maisha ya mjini ni rahisi sana. Ukishamiliki nyumba zako kadhaa, wewe ni kula tu mafao. Kodi miezi 3-6! Unapiga zako dili za udalali! Unakula cha juu, maisha yanaendelea.
Ole wako uwaige hao Maalwatan! Utalala na njaa.
Mjini hapa mzee,
Wengine wana miamvuli yao ile mikubwa wanakodisha kwa siju 1,000
Wengine walinzi, mchana stori nyingi usiku wanapotea.
Wengine ni wazee wa kuunganishia machinga wenye mabanda barabarani umeme. Ukiwa machinga na banda lako la mazaga akikuwekea taa, kwa buku.
So, mishe ni nyingi huku town mzee