Companero
Platinum Member
- Jul 12, 2008
- 5,604
- 1,704
Katika tafakuri zangu za kujiandaa kurudi kubeba maboksi kwa wazungu nimejikuta tena nikiitafakari nadharia tata ya 'Miafrika Ndivyo Ilivyo'. Ila leo nimeiangalia kwenye upande wa pili wa thumni. Hivi hawa wazungu ambao mwananadharia wa 'Miafrika Ndivyo Ilivyo' anadai wamependelewa na Mungu kuwa na vichwa vya kuvumbua sana wao huwa wanajisikiaje?
Kwa mfano, yanapotamkwa majina ya Galileo Galilei, Isaac Newton, Abraham Lincoln, Marie Curie, William Shakespear, Albert Einstein, Bill Gates na wazungu wengineo je mzungu anajisikiaje? Je, anajisikia kuwa hayo ni mafanikio ya Kizungu tu? Au anakubaliana na Frantz Fanon kuwa mafanikio hayo ni ya watu wote duniani ikiwamo Miafrika/Mitanzania?
Kama kuna mzungu humu ndani au mtu anayewaelewa vizuri wazungu basi naomba anisaidie kuelewa hili suala maana nadhani lina jibu la matatizo yetu Miafrika. Ningependa kujua mtu kama Jim Sinclair anajisikiaje hasa anapotoa yale matangazo yake kuhusu jinsi wanavyochota madini ya Mitanzania. Je, na yeye anajisikia kama yule Paul Mooney wa Makuadi wa Soko Huria? Kwa ujumla, je, wanajisikiaje kuhusu 'Miafrika ndivyo Ilivyo'?
Kwa mfano, yanapotamkwa majina ya Galileo Galilei, Isaac Newton, Abraham Lincoln, Marie Curie, William Shakespear, Albert Einstein, Bill Gates na wazungu wengineo je mzungu anajisikiaje? Je, anajisikia kuwa hayo ni mafanikio ya Kizungu tu? Au anakubaliana na Frantz Fanon kuwa mafanikio hayo ni ya watu wote duniani ikiwamo Miafrika/Mitanzania?
Kama kuna mzungu humu ndani au mtu anayewaelewa vizuri wazungu basi naomba anisaidie kuelewa hili suala maana nadhani lina jibu la matatizo yetu Miafrika. Ningependa kujua mtu kama Jim Sinclair anajisikiaje hasa anapotoa yale matangazo yake kuhusu jinsi wanavyochota madini ya Mitanzania. Je, na yeye anajisikia kama yule Paul Mooney wa Makuadi wa Soko Huria? Kwa ujumla, je, wanajisikiaje kuhusu 'Miafrika ndivyo Ilivyo'?