Hivi watumishi watafanya nini siku Serikali ikisema mwezi huu hakuna mshahara?

mkubhi

JF-Expert Member
Sep 9, 2015
2,204
3,308
Najaribu kufikilia hivi sasa wapinzani, makanisa na misikiti na vyombo vya habari vipo kimya kama vile havipo Tanzania, siku serikali ikisema mwezi huu mushahara hautakuwepo mpaka mwezi ujao watumishi watalibeba vipi hili?

Wakuu naleta kwenu!
 
Tutajilipa kwa kutumia vote 20 ya bunge la bajeti maana huko ndiyo kuna kichaka cha kuchotea hela
 
Tutajilipa kwa kutumia vote 20 ya bunge la bajeti maana huko ndiyo kuna kichaka cha kuchotea hela
Mkuu jamaa anaitafuna nchi mpaka mtu wa pembeni anasikia sauti ya meno ikitafuna,, Ilitakiwa amung'unye tu sasa imekua kama anakula Muwa mixer kuvuta mchuzi na kukata fundo kwa nguvu.
 
Kwa watz ninavyowafahamu, hakuna chochote kitakachotokea. Sanasana watafungua nyuzi hapa jf za kulia na kulalamika tu.
 
"Mushahara" ukikosekana hamna shida ila mshahara ukikosekana ndio itasumbua!
 
Serikali yoyote inapokuwa madarakani elewa kuna watu waloiweka(kuiajiri) japokuwa ajira yenyewe sio ya moja kwa moja. Katika hao walioiajiri serikali wapo ambao wao ndio wanaohitaji malipo kutoka kwa serikali na wapo ambao wao ndio wanailipa serikali. Na pia serikali hiyo hiyo hiyo kuwa inaowalipa moja kwa moja na kuna inaowalipa sio moja kwa moja. Hivyo si rahisi kwa waajiriwa wa watu waliowaajiri kusema hakuna malipo dhidi ya watu ilowaajiri

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hawataweza ! kwanza ikifika tarehe 26 tu panachimbika mitandaoni ije ifike tarehe 50?

Wataanza walimu kukabidhi chaki kwa academic, wanafuata watoto kicheza bila uangalizi ndipo wazazi masikini waanza kushangilia na baada ya wiki umma wenye uelewa unaunga mkono vuguvugu na muda huo mabeberu yashajua na ndo muda wake kufanya mambo.

Soon the 6th anaapa.

angalizo:-
kama umetumwa kupima upepo mwambie asijaribu, mshauri achape mzigo mpya hadi tukienda kununua mkate tubebe hela kwenye pikapu na kurudi na msosi kwenye kikapu.
 
Najaribu kufikilia hivi sasa wapinzani , makanisa na misikiti na vyombo vya habari vipo kimya kama vile havipo Tanzania, siku serikali ikisema mwezi huu mushahara hautakuwepo mpaka mwezi ujao watumishi watalibeba vipi hili?
Hilo haliwezekani ndio maana bungeni bajeti huwa inapitishwa kwa kila wizara, sio tu kwaajiri ya maendeleo bali pia kwaajiri ya kulipa mishahara ya wafanyakazi kwa mwaka mzima.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom