Hivi watengeneza sera wanajua vijana wanaofeli kidato cha 4 siku hizi wanakwenda wapi?

Wazo uli
Naanza kwa kuunga mkono hoja.

Nashauri serikali ipanue vyuo vya ufundi stadi (VETA) na kujiunga huko isiwe tena hiari iwe LAZIMA kwa vijana wanaomaliza form 4 na kupata division sifuri au four.

Nikiwa na maana baada ya vijana kumaliza form 4 serikali ichuje, wakwenda form 5, wakwenda vyuo vya taaluma na wale wanaobaki wapangiwe vituo vya VETA kwenda huko.

Hii haitaacha kijana mzururaji na itatoa hamasa kwa wazazi kupeleka watoto wao huko.

Mfumo huu unaweza kuwekwa na kuunganishwa kuanzia pale kijana anapoingia form 4 achague yeye mwenyewe ikitokea anakwenda VETA angependa kusomea nini.

Ifikie hatua tutambue kufeli shule haimaanishi mtu hafai au hawezi kufanya makubwa.

Kuna vijana wengi wenye vipaji wanapotea kutokana na mifumo yetu kumuona hana thamani tena baada ya kufeli shule.

Naomba kuwasilisha.
Wazo ulilotoa naliunga mkono asilia 100, hakuna haja ya wanafunzi wote kwenda form six na vyuo vikuu ,wanafunzi wote wanaofeli na kupata wastni wa chini waende vyuo vya ufundi kwa maana hilo Tanaka ndilo linalo jenga uchumi was nchi.
 
Sera bora hutegemea yafuatayo;

1. Nini uhitaji wa hiyo SERA kwa jamii?

2. Ushirikishwaji wa wadau (wanajamii, wanasiasa, dini, & watekelezaji/implementors wa hiyo sera ili kupata maoni sahihi

3. Mchango wa tafiti kadhaa kuhusu hiyo SERA

4. Utekelezaji bora wa SERA husika

SIASA

Najua kuna kundi la kutetea chama tawala,lakini kundi sahihi kwa nchi ni lile linalotoa ninikifanyike.

Hii dhana ya shule ni upotezaji wa muda imewaingia hawa vijana kwa kasi. Yani betting na kampani hawaoni kama inapoteza muda (kiume), na wa (kike )hawaoni engage yao kwenye drama za dating na fashion trends kama upotezaji wa muda.

Policy makers +Teknolojia = hapa kazi tunayo

Mr Mkiki.
Graduate kibao wanasota mtaani.
Anayefanya mamuzi ni meko
 
Dawa pekee hapo ni kuirudisha tu mezani ile sera ya Elimu ya Mwl. Nyerere ya enzi za Ujamaa! Education For Self Reliance.

Kitendo cha Serikali kwa sasa kuwakaririsha wanafunzi mambo yasiyo na tija na pia yasiyo na uhusiano na mazingira wanayotokea, ni matumizi yasiyofaa ya raslimali watu.

Vyuo vya Ufundi stadi VETA viimarishwe kwenye kila KATA Nchini. Zile shule za Ufundi mfano Tanga Tech, Arusha tech, Moshi tech, nk ziboreshwe ili kuzalisha wataalamu wa ngazi ya diploma.

Mitaala kuanzia shule za msingi mpaka vyuo ibadilishwe na hivyo Wanafunzi kuandaliwa kwa lengo kuu la kujiajiri badala ya ilivyo sasa ambapo wanaandaliwa kwa lengo la kuajiriwa.

Kiufupi kwenye suala zima la sera ya ajira, Serikali yetu inaleta utani. Madhara ya huu utani yatakuja tu kutokea siku moja pale hili kundi la vijana wasio na ajira litakapo amua kudai hizo ajira kwa nguvu.
 
Unajua hili ni suala nyeti na la muhimu sana ambalo serikali ilipaswa iliangalie kwa umakini sana.

Huwa najiuliza sana wanafunzi wanaopata zero kwenye matokeo ya IV serikali ina mpango gani nao, VETA inawatosha? Bodaboda mtaani zitawatosha? Viwanda vipo vya kuwatosha?

Dah,

Yaani serikali hao ‘graduates’ tu haina mpango nao, itakuwa sisi tuliopata zero.!
 
Naunga mkono hoja ya mtoa mada,

Form four awe ana cheti au hana lkn akishakosa form 5 na vyuo vya taaluma tayari anakuwa hana kazi, hana utaalam wowote sawa na aliyeishia la4C...

Nini kifanyike?

1. Tuwe serious kidogo kwenye content inayofundishwa darasani, yaan mtu aliyesoma soil profile, poultry farming nk nk awe na ujuzi au stadi za kazi, tuone kama kweli ni muhimu vijana hawa kuendelea kukariri Kinjekitile kafa lini...,

2. Kuongezwe vyuo vya veta ( serikali na private) kama walivyosema wengine, Ingawa hili halitokei tuu, hata sahv vyuo vinaongezeka with needs..., ukienda Arusha na dar utakuta vyuo vingi vya utalii, hotelia na lugha kutokana na mahitaji ya sehem ile.
So hapa cha kufanya ni kuongeza mahitaji, kama ambavyo tumesema TZ ya viwanda, mana yake kwenye entire chain watahitajika veta wengi kuliko hata professionals..

-Panua bandari, improve miundombinu kwenda nchi jirani, punguza kodi kwa makampuni ya usafirishaji, Ila lazima waajiri madereva waTZ...., Yaani tuwe busy Kwa wingi wetu kuhudumu nchi zingine
-empower makampuni ya ndani ya utalii yafanye Hadi nchi zingine, yaan mtalii aanzie hapa kwenda kwingine, siyo anakuja kupitia Kenya, mfano
-tafuta masoko ya bidhaa mbalimbali zinazolimwa nchini, hata soko likiyumba kuwe na bima za kusaidia, ili kilimo kiwe kitu kinacholipa, watu watajikuta wapo humo. Kwa sasa betting inalipa kuliko kulima mahindi.
KWA UJUMLA, TENGENEZA MAHITAJI, WATANZANIA WATACHANGAMKIA FURSA NAAMINI

3. JKT ni muhimu na lazima, nafikiri zingeongezwa, afu ziwezeshwe, baada ya yale mafunzo ya awali, kunakuwa na section ya ufundi stadi, wazalishe bidhaa zote zinazohitajika serikalini..., Afu serikali inawalipa ujira mdogo wakati wa kujifunza, akipata cheti anabaki Kwa ajira au anatembea mbele..
-Kwann tununue chaki
-Kwann serikali inunue mahindi ya kuweka kwenye ghala la taifa wakati mashamba ya jkt yamelala Tu pale
- shule hazina madawati
-ofisi hazina samani
- chaki za kuagiza China
- toothpick za Indiana
-viberiti sijui vya wapi


Nitaendelea
Asante!! Tuendelee kutuoa mawazo
 
Back
Top Bottom