Sajenti
JF-Expert Member
- Apr 24, 2008
- 3,651
- 412
Siku ya jumamosi wiki iliyopita rafiki yangu wa karibu sana alinipa mualiko wa ghafla ambao sikuutaraji. Pamoja na hali hiyo niliitikia wito. Pale nyumbani kwake tulikuwa wageni takribani 50 wake kwa waume. Sikujua undani wa mwaliko ule. Lakini baada ya sintofahamu ya muda mfupi baadae mwenyeji wetu alitupa undani wa mkusanyiko ule.
Kwa wengi waliokuwepo pale ilionekana kama ni kitu kipya ingawa mimi niliona ni aina ya mapinduzi tunayotakiwa kuyatarajia katika jamii yetu ya kitanzania. Yule mwenyeji alitueleza kuwa nia ya kutualika pale licha ya kula na kunywa lakini alitaka kupata msaada kutoka kwetu sisi ambao alituona ni watu wake wa karibu, tulioshibana nae hivyo tungemsaidia. Mtoto wake wa kiume ambae ni wa kwanza kuzaliwa amepata nafasi ya chuo nchini Scotland. Hii ina maana kuwa mzazi kwa nafasi yake hakuwa na uwezo sana kugharamia masomo ya kijana yule. na kwa maelezo yake alijaribu kupita hata katika taasisi za serikali e.g wizara na idara za serikali lakini bila mafanikio ili kupata msaada wa ufadhili hata ikibidi kwa mkopo. So tulitakiwa kumchangia ili kuongezea pale penye upungufu kwani alishakuwa na kiasi cha fedha lizoweza kupata.
Minong'ono niliyosikia ikienda chini kwa chini ilinishangaza sana, kwani mtu alihoji kuwa kama ni kuchangia ada ya mtoto kusoma nje ni jukumu la mzazi sio kuita watu eti na kuwapotezea muda wao???!! Watu tumekuwa wepesi sana wa kuchangia harusi kwa michango ya pesa nyingi tu, vipi elimu. Kwa kuwa tu kwenye harusi utahudhuria na kujilipa kwa njia ya vinywaji na maubwabwa basi?? Kifupi kikao hakikwenda vizuri mwisho wa kikao pledge zilizotoka pale Mmmmh!! Nashauri tuwe na harambee za kuchangia elimu sio miharusi tu..
Kwa wengi waliokuwepo pale ilionekana kama ni kitu kipya ingawa mimi niliona ni aina ya mapinduzi tunayotakiwa kuyatarajia katika jamii yetu ya kitanzania. Yule mwenyeji alitueleza kuwa nia ya kutualika pale licha ya kula na kunywa lakini alitaka kupata msaada kutoka kwetu sisi ambao alituona ni watu wake wa karibu, tulioshibana nae hivyo tungemsaidia. Mtoto wake wa kiume ambae ni wa kwanza kuzaliwa amepata nafasi ya chuo nchini Scotland. Hii ina maana kuwa mzazi kwa nafasi yake hakuwa na uwezo sana kugharamia masomo ya kijana yule. na kwa maelezo yake alijaribu kupita hata katika taasisi za serikali e.g wizara na idara za serikali lakini bila mafanikio ili kupata msaada wa ufadhili hata ikibidi kwa mkopo. So tulitakiwa kumchangia ili kuongezea pale penye upungufu kwani alishakuwa na kiasi cha fedha lizoweza kupata.
Minong'ono niliyosikia ikienda chini kwa chini ilinishangaza sana, kwani mtu alihoji kuwa kama ni kuchangia ada ya mtoto kusoma nje ni jukumu la mzazi sio kuita watu eti na kuwapotezea muda wao???!! Watu tumekuwa wepesi sana wa kuchangia harusi kwa michango ya pesa nyingi tu, vipi elimu. Kwa kuwa tu kwenye harusi utahudhuria na kujilipa kwa njia ya vinywaji na maubwabwa basi?? Kifupi kikao hakikwenda vizuri mwisho wa kikao pledge zilizotoka pale Mmmmh!! Nashauri tuwe na harambee za kuchangia elimu sio miharusi tu..