Hivi wanawake huwa mnasamehe kweli baada ya muda gani?

Half american

JF-Expert Member
Sep 21, 2018
25,903
67,887
Habari za wikiendi wakuu, bila kupoteza wakati niende moja kwa moja kwa linalonitatiza. Kama mnavyojua kuwa kukosea ni sehemu ya maisha na mda mwingine ni njia moja wapo ya kujifunza(sihalalishi kukosea kuwa ni sahihi). Baada ya kutambua kosa ni kuomba samahani na hapa kuna kusamehewa/kutokusamehewa.

Inakera sana mtu anakuambia amekusamehe lakini anavyoenenda ni tofauti kabisa na msamaha wake. Ni furaha kusameheka lakini inahuzunisha zaidi msamaha unakuwa nusu nusu.

Hivi unasamehe lakini husahau( sio lazima kusahau na sion ubaya kwenye hili). Kusahau imekua ngumu kuna haja gani ya kumkumbushia kila mara kuhusu lile ulilolisamehe? Mkipishana kidogo wimbo ni ule ule kwa lile ulilowahi kukosea na ni miaka imepita. Hii tabia inanikera sana wakuu .

Binafsi nikishasamehe sina muda wa kukumbuka na kumuhubiria mtu alichowahi kunikosea na sio busara kufanya hivyo. Hii tabia nimeiona kwa Ke watatu niliowahi kuwa nao.

Sasa dada zangu wazuri kabisa huwa mnasamehe kweli baada ya mda gani? Au ndio huwa hakuna msamaha?

Na hapa kama nimekosea mnisamehe na kazi iendelee.
 
~Kuna kusamehe ila sitaki mazoea,
~Kuna kusamehe na nikasahau tukaendelea poa
~Kuna kusamehe ya mdomoni tu nadhani hii inatokea kwa unmatured women, na hao 3 wanaangukia hapa

Hiyo ya kusamehe na kusahau na tukaendelea poa ndio yenyewe. Bora mtu akuambie nimekusamehe na hatak mazoea kuliko kuimba mapambio ya makosa kila mara.
 
Nachoshindwa kuelewa ni hapo tu, unafanya jambo kubwa unamuumiza mtu sana kihisia, unavunjavunja moyo wake vipande vidogo vidogo, unamsaliti mtu aliyekuamini with all her life, kisha mnataka eti, akilala akiamka kila kitu kiwe tu sawa as if jambo ulilofanya ni dogo mno..! that's next to Never,

Kusamehe siyo jambo rahisi kama unavyofikiri, unatamani kuachilia lakini unajikuta ule uchungu na maumivu viko tu pale, vinaku haunt, kila ukifikiri unashindwa kuamini hivi ni huyu kweli kanitenda haya..??

Enwei, wataalamu wanasema sometimes it takes mpaka 2 years kusamehe kabisa na kuachilia kwa makosa makubwa kama usaliti,

Endelea kubadili mwenendo wako kuonesha kuwa umebadilika kabisa, show her you're not the very same person, atasamehe ila itachukua muda, unapaswa kuvumilia, na huwa hatufanyi makusudi wala, ni unajikuta tu maumivu yanakukereketa moyoni hasa..!!
 
Hiyo inaitwa nimekusamehe ila sitasahau

Ndio katika hali ya kibinadamu kuna kosa unafanyiwa na kusahau inakuwa ngumu lakini sasa inabid uoneshe ukomavu wa fikra kwamba hutakiwi kutumia makosa ya mwenza wako kama fimbo ya kumchapia kwa sababu inaweza kuhatarisha mahusiano yenu kwani ipo siku atachoka ataona kumbe huyu hakunisamehe na anakinyongo

Mkuu niseme tu hao wanawake kuna namna wanakosea kwa kutokuacha mambo yapite
 
Mimi bwana nikitamka kwa mdomo wangu dhahiri nakuwa nimesamehe kweli na muda wa kuanza kukukumbushia sina na siwezi kufanya hivyo hata kama tukapishana tena na tena,.ila ukiniomba msamaha nikakuambia subiri kwanza au nipe muda basi nakuwa kwenye tafakuri hasa,.kwahiyo naweza kusamehe na kuachilia siku hiyo hiyo au baada ya muda fulani inategemea na moyo umelipokeaje jambo hilo..
 
Inategemea na kosa ulilofanya. Kuna makosa ambayo ukifanya, hata kama utasamehewa, mambo hayawezi kurudi kama yalivyokua "things will never be the same again".
Hiyo inaitwa nimekusamehe ila sitasahau
Ndio katika hali ya kibinadamu kuna kosa unafanyiwa na kusahau inakuwa ngumu lakini sasa inabid uoneshe ukomavu wa fikra kwamba hutakiwi kutumia makosa ya mwenza wako kama fimbo ya kumchapia kwa sababu inaweza kuhatarisha mahusiano yenu kwani ipo siku atachoka ataona kumbe huyu hakunisamehe na anakinyongo
Mkuu niseme tu hao wanawake kuna namna wanakosea kwa kutokuacha mambo yapite
 
Wanasamehe lakini hawasahau.

Mimi nilikuaga na demu wangu mmoja kumbe ilikua kila kosa nalofanya yeye ana kidaftari anaandika! Siku ya siku yamemfika hapa nikashangaa mtu katoa daftari anaanza kunisomea makosa yangu yote, siku, tarehe na muda! Aisee japo tulikua tumegombana lakini nilishindwa kujizuia nikajikuta nimeangusha bonge la kicheko mpaka yeye mwenyewe akajishtukia ikabidi twende kitandani tukasameheane tu..😂😂
 
Mkosee mama yako leo uone atakavyofukua makosa yako tangu ukiwa na sekunde 6 ndio utajua hujui. Huwa hatusahau sisi, ndio maana huwa mnaona mnatuvurugaaaa tunawacheki tu halafu fainali uzeeni.

Sent using Jamii Forums mobile app
Au unakumbuka mambo aliyokosea mwaka 1988 unamind gafla japo hausemi, na ndio hapa watu husema "wanawake wanapenda kununa bila sababu" sio kwamba hatuna sababu, zipo ila hatusemi na sababu nyingine unakuta ndio hizo za miaka ya zamani
 
Ngoja nikae hapa nipate nondo nijue wanasemehe baada ya muda gani, ili angalau niwe Nawavumilia kusubiri kusamehewa.

Yaan nmekuomba MSAMAHA kwa dhati ya moyo wangu kabisa, na nimeumia kweli kweli , alafu ipite

Wiki ya kwanza ...chafuuu

Ya pili .......chafuuuu

Yatatu...... chafuuuuu

Yanne .....Chafuuuuuuu

Et mambo ya Bado nafikiriaa, mambo ya sitaki nataka ?

Hehehehehehehe eeehhhh aiiiiiiįi

My Dear, labda Wanawake wawe wameisha Dunia hiii.

Ni ama
Usamehe na sahau ( Na usichelewe maana ni mwepesi wa 'Poa endelea na maisha yako"
Usisamehe na ueleweke ili Niendelee na Maisha mengine.

BAADHI YA MAKOSA, UKIMKOSEA MWANAMKE, LAZIMA ALIPIZE KISASI, ATAKUSAMEHE KWA MDOMO TU ,UJISAHAU ILA ATALIPA.

SASA KISASI CHA MWANAMKE NI KIBAYA.

Muwahi wewe mwenyewe KUMUACHA....

Kuna wengine mtaniambia..Ohoooo Ukikuaa utaona, ohoooo hujaoa wewe ,ohoooo ukioa utakuja kusema...ohoooo Tunza maneno

HahahaJasiri haachi Asili na Tabia ni ngozi .nasema uongo ndugu zangu

Point nikwamba, Nikikuomba msamaha, kama unakusudia kusamehe sameheee kwelikweli, mambo ya kutafutiana kuumizana ...Huo ni upotevu wa muda na nguvu...na nikiona sion dalili ya msamaha, NASEPA.
 
Nachoshindwa kuelewa ni hapo tu, unafanya jambo kubwa unamuumiza mtu sana kihisia, unavunjavunja moyo wake vipande vidogo vidogo, unamsaliti mtu aliyekuamini with all her life, kisha mnataka eti, akilala akiamka kila kitu kiwe tu sawa as if jambo ulilofanya ni dogo mno..! that's next to Never,

Kusamehe siyo jambo rahisi kama unavyofikiri, unatamani kuachilia lakini unajikuta ule uchungu na maumivu viko tu pale, vinaku haunt, kila ukifikiri unashindwa kuamini hivi ni huyu kweli kanitenda haya..??

Enwei, wataalamu wanasema sometimes it takes mpaka 2 years kusamehe kabisa na kuachilia kwa makosa makubwa kama usaliti,

Endelea kubadili mwenendo wako kuonesha kuwa umebadilika kabisa, show her you're not the very same person, atasamehe ila itachukua muda, unapaswa kuvumilia, na huwa hatufanyi makusudi wala, ni unajikuta tu maumivu yanakukereketa moyoni hasa..!!

Mabadiliko ndio ya muhimu hasa na ndio chachu ya samahani yako kuwa na maana kwake. Sipingi sio rahisi kusamehe na sio jambo linalochukua siku chache kufanikiwa ila sidhani kama ni busara useme umesamehe alafu unaendelea kutembea nalo moyoni.

Ukitembea nalo usiligusie kila mara maana kama mkosaji nilishatambua nilikosea na kuomba samahani haifai kunihubiria kila mara as if sijatambua kosa langu.
 
Hiyo inaitwa nimekusamehe ila sitasahau

Ndio katika hali ya kibinadamu kuna kosa unafanyiwa na kusahau inakuwa ngumu lakini sasa inabid uoneshe ukomavu wa fikra kwamba hutakiwi kutumia makosa ya mwenza wako kama fimbo ya kumchapia kwa sababu inaweza kuhatarisha mahusiano yenu kwani ipo siku atachoka ataona kumbe huyu hakunisamehe na anakinyongo

Mkuu niseme tu hao wanawake kuna namna wanakosea kwa kutokuacha mambo yapite

Nmekuelewa sana mkuu, kuna mda inabidi ukubali yaishe ili maisha mengine yaendelee. Kosea kidogo tu reference ni kosa lile hadi kuna mda anajishtukia anaomba samahani kuwa haitojirudia lakini haachi, majuzi ananiambia ishu sio kusamehe bali ni kusahau ndio ngumu nikamuuliza kuna haja gani ya kunitamkia kosa lile kila mara majibu yakawa ni kuwa hatorudia tena nmsamehe.
 
Mimi bwana nikitamka kwa mdomo wangu dhahiri nakuwa nimesamehe kweli na muda wa kuanza kukukumbushia sina na siwezi kufanya hivyo hata kama tukapishana tena na tena,.ila ukiniomba msamaha nikakuambia subiri kwanza au nipe muda basi nakuwa kwenye tafakuri hasa,.kwahiyo naweza kusamehe na kuachilia siku hiyo hiyo au baada ya muda fulani inategemea na moyo umelipokeaje jambo hilo..
Natamani angekuwa kama wewe maana inakera sana ni haki yake kunihukumu kwa sababu nilikosea kweli sikatai lakini sio kusema amesame alafu ananihubiria kila mara.

Mkosee mama yako leo uone atakavyofukua makosa yako tangu ukiwa na sekunde 6 ndio utajua hujui. Huwa hatusahau sisi, ndio maana huwa mnaona mnatuvurugaaaa tunawacheki tu halafu fainali uzeeni.

Kwa ufupi mnajua kulipa kisasi vizuri 100%. Sasa hiyo ina faida gani ikiwa unasababisha maumivu kwa mwngine tena unayempenda? Kama kusahau haiwezekani kwanini usisamehe na kukaa nalo kimya?
 
Back
Top Bottom