Hivi wanajeshi wa kike wa JWTZ wana kazi gani?

Password

JF-Expert Member
Feb 17, 2011
777
1,082
Salaam wana JF

Muda Fulani hivi kwenye ITV walionesha wanajeshi wa kike wa JWTZ wakiwa Kongo ikasemakana kwamba wameenda kulinda amani.Dada yangu anapenda sana kuwaona wanajeshi hasahasa wa JWTZ nikamwita aje kuwaona akaja mbiombio nikamwambia hawa wameenda kulinda amani kongo. Alinijibu kwa mshangao mkubwa sana akasema wanajeshi wa kike wa JWTZ hawaendagi vitani(ingawa ile haikuwa vita ila mapigano yanahusika).

Hivi ni kweli wanajeshi wa kike hawaendagi vitani na kama ni ndiyo je kazi yao kuu ni nini wakiwa jeshini?

Karibuni mnijuze zaidi
 
Alikudanganya, wanajeshi wote wanaenda vitani bila kujali jinsia, kinaachotofautisha ni majukumu tu.. Kuna wengine wataenda kwny uwanja wa vita na wengine wanapewa shughuli nyingine..
 
f8ab2f1be9c4b3a90e80e5f8fa4d7bd6.jpg
 
Salaam wana JF

Muda Fulani hivi kwenye ITV walionesha wanajeshi wa kike wa JWTZ wakiwa Kongo ikasemakana kwamba wameenda kulinda amani.Dada yangu anapenda sana kuwaona wanajeshi hasahasa wa JWTZ nikamwita aje kuwaona akaja mbiombio nikamwambia hawa wameenda kulinda amani kongo. Alinijibu kwa mshangao mkubwa sana akasema wanajeshi wa kike wa JWTZ hawaendagi vitani(ingawa ile haikuwa vita ila mapigano yanahusika). hivi ni kweli wanajeshi wa kike hawaendagi vitani na kama ni ndiyo je kazi yao kuu ni Nini wakiwa jeshini.

Karibuni mnijuze zaidi

hivi wangeweka jeshi liwe kwa wanaume tu si mngelalamika pia, lazima mngehoji kwa nn hamna wa kike? all in all kazi ya wanajeshi wa kike ni kama zilivyo za wanajesh wa kiume
 
Alikudanganya, wanajeshi wote wanaenda vitani bila kujali jinsia, kinaachotofautisha ni majukumu tu.. Kuna wengine wataenda kwny uwanja wa vita na wengine wanapewa shughuli nyingine..
shughuli nyingine ipi mkuu!!!!!!!!!!!!!!!
 
Mtafute Mhariri wa Dira alieandika Uzushi wa Kifaru cha Jeshi kuibiwa atakupa Majibu kamili juu ya kazi ya Askari wa Kike Jeshini.

Mkuu umenikumbusha yule mzee wa "sadism is inevitable" hebu tumwombe popote alipo aje atuondolee huu utata
 
Wanajeshi kazi yao kubwa ni vita bila kujali jinsia.
kuwa mwanajeshi hapa TZ ni raha sana wengine mpaka wanastaafu jeshi hawajui hata uwanja wa vita unafananaje.ila kweli inawezekana hao wengine watakuwa wanapangiwa shughuli nyingine
 
Salaam wana JF

Muda Fulani hivi kwenye ITV walionesha wanajeshi wa kike wa JWTZ wakiwa Kongo ikasemakana kwamba wameenda kulinda amani.Dada yangu anapenda sana kuwaona wanajeshi hasahasa wa JWTZ nikamwita aje kuwaona akaja mbiombio nikamwambia hawa wameenda kulinda amani kongo. Alinijibu kwa mshangao mkubwa sana akasema wanajeshi wa kike wa JWTZ hawaendagi vitani(ingawa ile haikuwa vita ila mapigano yanahusika). hivi ni kweli wanajeshi wa kike hawaendagi vitani na kama ni ndiyo je kazi yao kuu ni Nini wakiwa jeshini.

Karibuni mnijuze zaidi

Mkuu jeshi lina mabo/kazi nyingi sana sio kushika mtutu wa bunduki tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom