Hivi wana CCM mnajisikiaje baada ya kuikataa Katiba ya Tume ya Warioba?

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,479
30,144
Wakati wa utawala wake wa awamu ya 4 Rais wa wakati huo, Jakaya Kikwete aliamua kuunda Tume ya kuratibu maoni ya wananchi ili Taifa lipate Katiba mpya.

Wakati anakabidhi majukumu hayo ya kuratibu maoni ya wananchi, Jakaya Kikwete alisema kuwa Katiba ya nchi yetu imepitwa na wakati kwa hiyo ilikuwa haikidhi mahitaji ya wakati huu, kwa kuwa ni Katiba ambayo tumeitumia kwa zaidi ya miaka 50 tokea tupate Uhuru, ingawa imekuwa ikiwekewa viraka mara kwa mara.

Kwa hiyo Rais mstaafu, Jakaya Kikwete alitamka wakati huo kuwa angetamani nchi yetu ipate Katiba mpya ambayo itatuvusha kwa miaka mingine 50 ijayo.

Tume ya Warioba ikakamilisha kazi yake ya kukusanya maoni ya wananchi kwa ufanisi mkubwa na ikakabidhi Rasimu hiyo ya Katiba kwa Rais huyo mstaafu Jakaya Kikwete.

Baada ya hapo likaundwa Bunge la Katiba ambalo lilikuwa na wajumbe wengi kutoka CCM na likawa na wajumbe wachache kutoka vyama vya upinzani.

Kwenye Bunge hilo la Katiba ndipo kulipotokea "sekeseke" kubwa baada ya wajumbe hao kutoka CCM kuamua "kunyofoa" vipengele vingi vyenye maslahi mapana kwa Taifa na badala yake wakareplace na vipengele ambavyo vilikuwa vimeandaliwa pale mtaa wa Lumumba chini ya uandishi wa mwanasheria wao nguli Andrew Chenge, kwa maslahi ya chama chao cha CCM!

Kutokana na hali hiyo wajumbe wa Bunge hilo kutoka vyama vya upinzani wakaamua kususia Bunge hilo kwa kutoka kwenye Bunge hilo na kuwaachia wanaccm watupu ambao walipitisha Katiba yao pendekezwa ya CCM.

Na hapo ndipo ulipokuwa mwanzo wa kuundwa kwa Umoja wa vyama vya siasa vya UKAWA.

Hata hivyo hadi leo hii hiyo Katiba pendekezwa haijaweza kupigiwa kura ya maoni na wananchi kama takwa la kisheria linavyohitaji.

Kwa maana hiyo hadi hivi sasa nchi yetu haijaweza kuwa na Katiba mpya kama yalivyokuwa matarajio ya wananchi wengi kutokana na wabunge wa Bunge la Katiba wa kutoka CCM kuweka maslahi yao binafsi na ya chama chao na hivyo kukataa vipengele muhimu vilivyokuwa kwenye Rasimu ya Tume ya Warioba ambavyo vilitokana na maoni ya wananchi yaliyokusanywa nchi nzima na Tume ya Warioba.

Kitu kingine ambacho kinatia uchungu zaidi ni kuwa mchakato mzima wa kutafuta Katiba mpya uligharimu pesa za walipa kodi kiasi cha shilingi zaidi ya bilioni 300 ambapo hatimaye Katiba hiyo ya Warioba ilitupwa kwenye "dustbin" na wabunge wa Bunge la Katiba kutoka CCM na Katiba yao waliyoipendekeza hadi hivi sasa nayo imebuma!

Tujaribu pia kuimagine hivi hizo pesa zipatazo shilingi bilioni 300 ambazo zimepotea bure kutokana na kuwa hadi hivi sasa hatijapata Katiba mpya........

Hivi pesa hizo kama zisingepotea kwenye matumizi hayo "mabovu" ya kuratibu maoni ya wananchi ambayo wanaccm waliyaona "rubbish" hivi pesa hizo zingeweza kufanya mambo mangapi muhimu kwa maslahi mapana kwa Taifa letu badala yake?

Sasa swali kubwa tunalowauliza wana CCM wanajisikiaje hivi sasa baada ya kuweka maslahi yao binafsi na ya chama chao mbele na kutojali maslahi mapana ya Taifa na hivyo kusababisha Taifa limekwama kupata Katiba mpya?
 
Hivi tunawezaje kuwa na Katiba ambayo inampa mamlaka Rais wa nchi kuwa ndiye anayemteua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi wa Taifa na makamishna wake wote wakati yeye naye ni mgombea mmojawapo wa nafasi ya Urais?

Kinachofanyika kuhusiana na Tume yetu ya uchaguzi naweza kufananisha na pambano LA mpira LA watani wa jadi wa Yanga na Simba, lakini refa wa kati na washika wake vibendera wa pembeni na makamisaa wa mchezo huo wawe wote wanataka upande mmoja wa Yanga!

Hivi unategemea kwenye mchezo huo hao wachezeshaji wafanye fairness?

Jibu liko wazi kuwa hao waamuzi ni lazima watafanya upendeleo kwa Yanga ambako ndiko walikotoka.....
 
Tena tunamlaani lowassa baada ya kufikiri kuwa atakuwa rais ili alindwe na hii katiba mbovu!
Ndiyo maana Mkuu "kipara kipya" tunasema kuwa Katiba yetu ni "Bomu" bila kuangalia ni nani inamlinda.......

Whether awe anatoka chama tawala au kutoka upinzani.........
 
Kwa suala la Katiba ya bchi, jirani zetu Kenya wanatizidi kwa mbali sans kwa ubora wa Katiba yao.

Tumeshuhudia Kiongozi mkuu wa upinzani nchini humo Raila Odinga wa Muungano wa vyama vya NASA akifungua kesi kwenye supreme court ya nchi hiyo kupiga matokeo ya Rais.

Hebu Fanya comparison ya Katiba yetu ambayo inasema kuwa Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi anapomtangaza mgombea wa Urais aliyedhinda , hakuna mahakama yoyote hapa nchini itakayokuwa,na uwezo wa kusikiliza shauri lolote LA kilalamikia matokeo hayo.

At the same time anayeteua kuanzia Mwenyekiti wa Tume na makamishna wote wa Time hiyo ni Rais wa nchi ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa chama tawala, ambaye pia ni miongoni ya wagombea waliopigiwa kura ya Ufaid , ambayo Tune hiyo anapaswa kutoa matokeo yake......

What do you expect to happen??????
 
Katiba ni bonge la bomu.......la muda tu litalipuka na itakuja kuleta fujo sanaaa hasa hii tunayojidanganya amani!!!
 
Lakini nasikia kuwa aliyebariki mchakato ndiye aliyeharibu pia mchakato mzima kwa maelekezo yake mwenyewe yaliyokuwa yakitolewa mara kwa mara kwenye vikao vyao vya chama.
Madhumuni ya kuvuruga mchakato mzima ni kwa sababu katika katiba pendekezwa ilikuwa ikimbana hata yeye mwenyewe kama alifanya madhambi "ofisini" alistahili kuwajibishwa.
Kwa hiyo akapiga kampeni na vitisho kwa wajumbe ili kuivuruga.
Hii ndiyo taswira ya viongozi wengi wa kiAfrika.
Suala hilo likisimamiwa kwa sasa linaweza likaenda vizuri.
Lakini iwe kwa kutumia "mapendekezo ya Warioba" na kuundwa bunge jioya la katiba. Hapi tunaweza kuja na muafaka mzuri.
 
Ndiyo maana Mkuu "kipara kipya" tunasema kuwa Katiba yetu ni "Bomu" bila kuangalia ni nani inamlinda.......

Whether awe anatoka chama tawala au kutoka upinzani.........
mimi niliongezea nyama tu sababu tunapiga kelele yeye tuliyenaye hana moyo wa dhati kuiondoa hiyo bomu!
 
mimi niliongezea nyama tu sababu tunapiga kelele yeye tuliyenaye hana moyo wa dhati kuiondoa hiyo bomu!
Very true, na alishawahi kutamka kuwa suala la Katiba ya nchi siyo kipaumbele chake bali yeye priority no 1_kwake ni kuinyoosha nchi!
 
Kutumika billion 300 sio kigezo cha kukubali katiba hata ingekuwa trillion.
Halafu hivi unakumbuka ni watu gani waliochangia maoni yao? Namna ya kuwapata unaikumbuka?
Ninavyojua mfumo uliotumika kuchukua maoni ulikuwa very fair....

Taabu ilianza baada ya Bunge la Katiba kuanza vikao vyake ambapo wabunge wa Bunge hilo kutoka upande wa CCM walianza kuijadii Katiba hiyo kuangalia zaidi maslahi ya Chama chao badala ya kutanguliza maslahi mapana ya Taifa letu.
 
Lakini nasikia kuwa aliyebariki mchakato ndiye aliyeharibu pia mchakato mzima kwa maelekezo yake mwenyewe yaliyokuwa yakitolewa mara kwa mara kwenye vikao vyao vya chama.
Madhumuni ya kuvuruga mchakato mzima ni kwa sababu katika katiba pendekezwa ilikuwa ikimbana hata yeye mwenyewe kama alifanya madhambi "ofisini" alistahili kuwajibishwa.
Kwa hiyo akapiga kampeni na vitisho kwa wajumbe ili kuivuruga.
Hii ndiyo taswira ya viongozi wengi wa kiAfrika.
Suala hilo likisimamiwa kwa sasa linaweza likaenda vizuri.
Lakini iwe kwa kutumia "mapendekezo ya Warioba" na kuundwa bunge jioya la katiba. Hapi tunaweza kuja na muafaka mzuri.
Naweza kukubaliana na maoni yako kwa kiasi Fulani.

Kwa kuongezea tu, ninachohisi kilichotokea ni kuwa wakati JK anateua wajumbe wale wa Tume ya kuratibu maoni ya wananchi na kumpa uenyekiti wa Tume hiyo mwanaccm mwenzao Jaji Joseph Warioba, nadhani matarajio yake na ya wanaccme wenzake yalikuwa, baada ya kukusanya maoni hayo atafanyia "editing" maoni hayo na kuyakata maoni yote ambayo siyo ya maslahi kwa chama chao.......

Sasa shida ilianza baada ya Jaji Warioba kijivua unafiki na kuyaweka maoni yote ya wananchi kama walivyoyapokea na Tume ya Warioba kukabidhi Rasimu ya Katiba hiyo kwa JK na alipoipitia na kuisoma.......

JK akaona baadhi ya vipengele "vinamchefua" na akaona havikustahili kuwemo kwenye Rasimu hiyo.........

Vipengele kama uundwaji wa Tume huru ya uchahuzi ......

Kipengele cha wagombea wa nafasi ya Urais kuweza kufikisha malakamiko yako ya kipinga matokeo hayo mahakamani.......

Na kipengele cha kuondoa kinga ya Rais aliyeko madarakani na ambaye keshaondoka madarakani kuweza kushitakiwa mahakamani iwapo watafanya makosa makubwa Kama ya "abuse of power" nadhani ndiyo yaliyomfanya JK kupiga U turn na kuigomea Katiba na kuona ni heri tuendelee na Katiba yatu ya hivi sasa milele!
 
inavyoonekana Lowasa anakutesa sana moyoni! kilichoongelewa hapa ni katiba,wewe unmsemaLowasa ,au ndiyo uwezo wako huo kiakili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mawazo yake usiyabeze saaana kiivyo.
Iko hivii? Baada ya kuamini kabisa kuwa EL anakubalika na kujipa matumaini ya kushika kijiti toka kwa JK, alitumia uwezo wake wote pamoja na mshirika wake wa karibu JK kuivuruga kabisa katiba pendekezwa.
Katiba ya uTanganyika ilikuwa inampunguzia "ujogoo" rais wa muungano kitu ambacho EL hakukubaliana nacho hata chembe, ndiyo maana serikali3 ilipigwa vita vya kufa mtu.
Pia JK ilikuwa inambana mwenyewe, baada ya kukabidhi kijiti na akionekana kama alifanya madhambi madarakani kuwajibishwa.
Siyo kwamba kila kitu wanachokisema watu ni wajinga na ni kibaya kwako kwa ajili tu ya mahaba na ushabiki wa kisiasa.
Jifunze pia kutafakari na mawazo ya watu wengine na si kukimbilia kubeza kilakitu kwa kujivisha upofu.
 
Mawazo yake usiyabeze saaana kiivyo.
Iko hivii? Baada ya kuamini kabisa kuwa EL anakubalika na kujipa matumaini ya kushika kijiti toka kwa JK, alitumia uwezo wake wote pamoja na mshirika wake wa karibu JK kuivuruga kabisa katiba pendekezwa.
Katiba ya uTanganyika ilikuwa inampunguzia "ujogoo" rais wa muungano kitu ambacho EL hakukubaliana nacho hata chembe, ndiyo maana serikali3 ilipigwa vita vya kufa mtu.
Pia JK ilikuwa inambana mwenyewe, baada ya kukabidhi kijiti na akionekana kama alifanya madhambi madarakani kuwajibishwa.
Siyo kwamba kila kitu wanachokisema watu ni wajinga na ni kibaya kwako kwa ajili tu ya mahaba na ushabiki wa kisiasa.
Jifunze pia kutafakari na mawazo ya watu wengine na si kukimbilia kubeza kilakitu kwa kujivisha upofu.
That is very true.

Let's allow freedom of expression
 
Miongoni ya vitu vibovu kabisa kwenye Katiba yetu ya sasa ni kumpa mamlaka Rais aliyeko madarakani ambaye pia ndiye Mwenyekiti wa Chama tawala kuwa ndiye amayeteua Mwenyekiti wa Tume ya uchaguzi na makamishna wake wote.

Hivi unategemea kwa muundo huo wa Tume iweze kuwa fair kwa vyama vya upinzani?

Swala lingine bovu kabisa kwenye Katiba yetu ya sasa ni kumpa impunity Rais wa nchi hii.....

Mbaya zaidi ni pale Katiba hiyo inaposema kuwa Rais hataweza kushitakiwa kwenye mahakama yoyote hapa nchini kwa kosa lolote atakalofanya atakuwepo madarakani na hata atakapotoka madarakani!

Hivi wananchi tukisema kwa Katiba hiyo Rais amapewa madaraka ya ki-mungu-mtu mtatuita wachochezi?
 
Back
Top Bottom