Pengine tungepata uchambuzi wa neno kutoka " kwa ninavyoona mimi waliotoka ni wajumbe wa bunge la katiba wa CCM ila kwa sababu wana nguvu na ubabe uliokomaa ndio maana wameng'ang'ania mjengoni lakini kimsingi wametoka kabisaa! hawa UKAWA hawajatoka kwa maana wanaitetea Rasimu ya Mzee Warioba. Lakini CCM wana rasimu yao hilo tu linatosha kuwaomba warudi kwenye MADA sio mjengoni! Tafakari hili kama kutoka ni kwenye Mjengo wa Bunge UKAWA wametoka lakini kama kutoka ni kwenye MADA au HOJA iliyoletwa basi CCM wametoka" Bado nauliza ni nani katoka?