DSpecial
JF-Expert Member
- Dec 18, 2011
- 480
- 158
Sikuzote kumuita msichana Demu huwa siwezi, na hili neno kulitamka kwenye kinywa changu ni zito sana kwakweli. Na kwa nilivyokuwa nikidhani hapo awali nilikuwa najua kama kunmuita msichana demu ni kama kumdhalilisha flani hivi. Ila naona linatumika sana kwakweli, lakini sijui kwa nini hili neno kwangu mimi linakuwa ni zito kulitumia. Sasa wadau na hasa kina dada wa humu JF naomba mnieleweshe vizuri kama hili neno mnakubaliana nalo kuitwa hivyo au huwa hampendi mnapoitwa mademu?