Hivi Waislamu " original" wako Israel ( Palestina) au Saudi Arabia?

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
82,754
139,558
Nauliza tu kwa wanazuoni na wabobezi wa maswala haya ya imani za kuabudu na kumtumikia Mungu.

Kwa mfano hapa Tanzania hizi dini tuliletewa tu kutoka huko zilikoanzia, ndio maana nauliza Uislam wa " ukweli " ni ule wa Palestina, Saudi Arabia au Iran?

Kuuliza siyo ujinga.

Ramadhan kareem!
 
Bwashee uislamu ulianzishwa na mtume.

Mtume alizaliwa Mecca Saudi Arabia kwa iyo asili ya uislam ni Saudia.

Hao waislamu wa israeli ni wavamizi ndo mana wanashurutishwa waondoke kwenye nchi ya ahadi.
Nimekuelewa kiasi bwashee!
 
Sasa kama unaamini Tanzania dini tuliletewa, hudhani swali lilitakiwa kuwa chimbuko la Uislamu ni wapi badala ya kuhoji Uislamu wa kweli?!

Uislamu ni mmoja tu, kama unaamini kuna Uislamu wa uongo basi huo sio Uislamu!!

Wapo Waislamu wa uongo lakini hakuna Uislamu wa uongo ingawaje yanaweza kuwepo madhehebu ya uongo ; kama ambavyo uwepo wa Wakristo wa uongo lakini hapawezi kuwepo na Ukristo wa uongo, at least, as per christianity faith ingawaje huko pia yanaweza kuwepo madhehebu ya uongo!!

Ni kutokana na ukweli huo, ndo maana hata Yesu hakupata kuzungumzia suala la Ukristo wa uongo bali Manabii wa Uongo wanaotokana na Wakristo waongo, na hatimae kuanzisha madehebu ya uongo!!

Mkristo/Mwislamu muongo ni kama Mtanzania anayejifanya ni Mtanzania wakati sio Mtanzania na kwahiyo anakuwa Mtanzania wa uongo lakini hakuna Tanzania ya uongo!!

So, kama swali ni chimbuko basi ni Saudi Arabia kwa sababu ndiko Mtume Muhammad alizaliwa na kupata utume wake akiwa huko, kama ilivyo kwa Ukristo ambapo Yesu alizaliwa Israel, na kuanza mafundisho yake huko!!
 
Sasa kama unaamini Tanzania dini tuliletewa, hudhani swali lilitakiwa kuwa chimbuko la Uislamu ni wapi badala ya kuhoji Uislamu wa kweli?!

Uislamu ni mmoja tu, kama unaamini kuna Uislamu wa uongo basi huo sio Uislamu!!

Wapo Waislamu wa uongo lakini hakuna Uislamu wa uongo ingawaje yanaweza kuwepo madhehebu ya uongo ; kama ambavyo uwepo wa Wakristo wa uongo lakini hapawezi kuwepo na Ukristo wa uongo, at least, as per christianity faith ingawaje huko pia yanaweza kuwepo madhehebu ya uongo!!

Ni kutokana na ukweli huo, ndo maana hata Yesu hakupata kuzungumzia suala la Ukristo wa uongo bali Manabii wa Uongo wanaotokana na Wakristo waongo, na hatimae kuanzisha madehebu ya uongo!!

Mkristo/Mwislamu muongo ni kama Mtanzania anayejifanya ni Mtanzania wakati sio Mtanzania na kwahiyo anakuwa Mtanzania wa uongo lakini hakuna Tanzania ya uongo!!

So, kama swali ni chimbuko basi ni Saudi Arabia kwa sababu ndiko Mtume Muhammad alizaliwa na kupata utume wake akiwa huko, kama ilivyo kwa Ukristo ambapo Yesu alizaliwa Israel, na kufanya mafundisho yake huko!!
Ahsante bwashee!
 
Dini ungekuwa ni mpango wa Mungu, Basi alipoumwa Adam palepale angepewa dini. Lakini alipewa ardhi, wanyama, na kila kitu. Dini ikaja baadaye Sana. Ukristo Leo una miaka 2028 na uislamu ulikuja miaka 400-600 baada ya Ukristo.
Siku zote hizo kwanini Mungu hakuwa amezileta hizo dini feki?
Hata Biblia yenyewe inathibisha kuwa hizo mnazodhani kuwa ni dini Bora si lolote wala chochote, ila dini Bora ni hi:-

Yakobo 1:27
Neno: Bibilia Takatifu

27 Dini iliyo safi, isiyo na uchafu mbele za Mungu Baba, ndio hii: kuwasaidia yatima na wajane katika dhiki zao, na kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu.
 
Bwashee uislamu ulianzishwa na mtume.

Mtume alizaliwa Mecca Saudi Arabia kwa iyo asili ya uislam ni Saudia.

Hao waislamu wa israeli ni wavamizi ndo mana wanashurutishwa waondoke kwenye nchi ya ahadi.
Hahaaa
Kumbe Israel ndo wavamizi I see! Vice versa is true
 
Dini ungekuwa ni mpango wa Mungu, Basi alipoumwa Adam palepale angepewa dini. Lakini alipewa ardhi, wanyama, na kila kitu. Dini ikaja baadaye Sana. Ukristo Leo una miaka 2028 na uislamu ulikuja miaka 400-600 baada ya Ukristo.
Siku zote hizo kwanini Mungu hakuwa amezileta hizo dini feki?
Hata Biblia yenyewe inathibisha kuwa hizo mnazodhani kuwa ni dini Bora si lolote wala chochote, ila dini Bora ni hi:-

Yakobo 1:27
Neno: Bibilia Takatifu

27 Dini iliyo safi, isiyo na uchafu mbele za Mungu Baba, ndio hii: kuwasaidia yatima na wajane katika dhiki zao, na kujilinda mwenyewe usichafuliwe na ulimwengu.
tatizo hujui hata maana ya dini ni nn
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom