Hivi wafuasi wa CUF na NCCR walirudi CCM baada ya vyama vyao kupotea?

radika

JF-Expert Member
Jul 15, 2014
20,427
32,196
Kuna jambo ambalo wana ccm wanajifariji na kulifurahia kwamba upinzani hasa chadema na cuf ukipotea basi ndio nafuu ya ccm swali dogo tujiulize toka mfumo wa vyama vingi uanzishwe wamewahi kusikia wafuasi wa vyama vya upinzani baada ya nccr na cuf kupoteza nguvu na mvuto hivyo vyama vikakosa wafuasi kiasi kwamba wakarudi ccm kwa mapenzi yao?

Huo mpambano ktk chaguzi mbalimbali ambao ccm inaupata hao wapiga kura wanatoka wapi? Hapa lazima akili ya ziada inahitajika kujua kwamba upinzani si vyama vya upinzani bali dhamira iliyopo mioyoni mwa baadhi ya watu ambao hawaridhishwi na ccm hii ina maana hata kama chadema na cuf vitapotea hili kundi litaendelea kuwepo ambalo baadae litakuja kuwa na nguvu za ajabu.

Endapo vyama vya upinzani vikatoweka hili kundi ambalo tayari linachembechembe za kutaka mabadiliko litakwenda wapi? Je mtawalazimisha wawe wanachama wa ccm kinguvu? Hapa mwenyekiti wa ccm,katibu na ndugu polepole wanacheza kamari kitu wanachokizalisha baadae watakilipa kwa gharama yoyote ile.

Kwa sasa hamna kumuunga mkono wamekuja na slogan mpya wanapita bila kupingwa huu ni mchezo wa kitoto sana unaofanywa na watu wenye viwango vya udaktari na uprofesa kwa kushabikia hili jambo.

Nguvu kubwa inatumika kurubuni madiwani na wabunge wahamie chama kikuu kweli wengine wanakubali lakini hata ukiwaangalia kwa muonekano wa taswira zao ni watu waliokosa kujiamini na hawana amani kabisa.

Muda ni hakimu mzuri haki ya mtu haipotei ila hucheleweshwa tu.
 
Ccm hawajawahi kuwa na fikra firikishi wanaishi katika fikra mkumbo maana wananchi wenye vyama vyao ni asilimia ndogo sana kulinganisha na wale wasio na vyama vya siasa ambao ndio huwa waamuzi wa chaguzi mbalimbali za kisiasa nchini
 
Ccm hawajawahi kuwa na fikra firikishi wanaishi katika fikra mkumbo maana wananchi wenye vyama vyao ni asilimia ndogo sana kulinganisha na wale wasio na vyama vya siasa ambao ndio huwa waamuzi wa chaguzi mbalimbali za kisiasa nchini
Mkuu hawa jamaa wanashangaza mtu anacoment chadema kinakufa kwa furaha sana sasa unajiuliza chadema kikifa huyo mwanachadema ataenda ccm na kuwa mwanachama mtiifu?
 
Mkuu hawa jamaa wanashangaza mtu anacoment chadema kinakufa kwa furaha sana sasa unajiuliza chadema kikifa huyo mwanachadema ataenda ccm na kuwa mwanachama mtiifu?
Historia ya chaguzi zetu mbalimbali toka kurudishwa kwa mfumo wa vyama vingi vya kisiasa 1992 na 1995 kukafanyika uchaguzi wake wa kwanza na ccm kupata upinzani mkubwa sana, hivyo toka 1995 hadi 2015 ccm hawajawahi kuwa na uchaguzi rahisi pamoja na baadhi ya vyama kuua nguzu zake
 
downloadfile-3.gif

Tunabomoa ngome.:D
 
NCCR-Mageuzi, CUF na NLD waliuzwa wakiwa ndani ya gunia. The trio are numbly done. The killer, Chadema, is also on the death roll. Think on new strategic plans to launch credible foresighted opposition in Tanzania.
 
Back
Top Bottom