Hivi Vita vya Kuupinga Ufisadi Vipo au Myth?

Zakumi

JF-Expert Member
Sep 24, 2008
5,063
2,471
Baada ya kuwa mwangaliaji wa muda mrefu kuhusu masuala ya ufisadi, ningependa kusema kuwa hakuna kitu kinachoitwa vita dhidi ya ufisadi.

Haya ni maoni yangu binafsi na sina nia ya kuwakatisha tamaa wapiganaji au kuwafagilia mafisadi. Na maoni yangu yanatokana na ukweli kuwa vita vyovyote ni lazima viwe na viongozi, wapiganaji, mbinu za upiganaji na malengo ya kupigana vita hivyo.

Sasa tukija katika vita vya ufisadi, sioni viongozi wowote ambao wanaweza kuunganisha umma na wapiganaji hili kufikia malengo hayo. Mpaka sasa sijaona kiongozi yoyote anayekubalika.

Kuhusu wapiganaji. Hiki pia ni kikwazo. Wapiganaji wengi wanapigana vita vya mtu mmoja mmoja. Kwa maana kwamba kila mtu yupo tayari kutoa mawazo yake kwa kupitia waandishi wa habari, internet forums, blogs lakini hakuna nguvu ya pamoja. Hivyo muda mwingi unatumika kutoa new big ideas katika vyombo vya kutoa habari.

Mbinu zinazotumika ni zilezile wanazotumia mafisadi. Tena mafisadi wanazitumia kwa ufanisi mkubwa. Kwa mfano propaganda ni mbinu ambazo zinamlenga mlalahoi na sio profesa wa UDSM, au mchangiaji wa JF. Hivyo Makamba anaposema wanaopinga Serikali wanaona wivu kwa kukosa madaraka, anayemlenga ni mlalahoi ambaye siku ya uchaguzi ataipigia kura CCM. Hivyo wapiganaji walipo JF kuuliza elimu ya Makamba kutokana na kile alichosema ni kutojua uwanja wa mapambano huko wapi.

Malengo ya vita dhidi ya ufisadi ni finyu. Na kutokana na ufinyu huo, hata mbinu za kupiga vita vyenyewe zinakuwa na matatizo. Ufisadi unatokana na ukweli kuwa binadamu ni Greedy. Na njia pekee ya kupunguza greed ni kuwa na jumuia au taasisi zilizo transparent, zenye ku-check and balance uongozaji wa jumuia na zenye kufuata sheria.

Wenu

Z10
 
Mbinu zinazotumika ni zilezile wanazotumia mafisadi. Tena mafisadi wanazitumia kwa ufanisi mkubwa. Kwa mfano propaganda ni mbinu ambazo zinamlenga mlalahoi na sio profesa wa UDSM, au mchangiaji wa JF. Hivyo Makamba anaposema wanaopinga Serikali wanaona wivu kwa kukosa madaraka, anayemlenga ni mlalahoi ambaye siku ya uchaguzi ataipigia kura CCM. Hivyo wapiganaji walipo JF kuuliza elimu ya Makamba kutokana na kile alichosema ni kutojua uwanja wa mapambano huko wapi.

Malengo ya vita dhidi ya ufisadi ni finyu. Na kutokana na ufinyu huo, hata mbinu za kupiga vita vyenyewe zinakuwa na matatizo.

Wenu

Z10

Mh,

Kama ulivyosema on the first paragraph of the quote, personally i do side with ur argument totally. Kitu ambacho umeacha na kwa opinion yangu ni kwamba CCM inawasomi na waelevu wengi they know, who matters and what to say. Hivyo siku zote wapo ahead of the game.

Angalia the amount of people turning up whenever a senior CCM official goes at their political rallies. Na tazama hawa jamaa wapinzani au hata wapiganaji wa CCM, target yao sio welfare ya wananchi bali daily attacks on hao so called mafisadi.

Umewahi hata siku moja kusikia mpiganaji akisema hela iliyoibiwa secta fulani ilikua na uwezo wa kusaidia wananchi kwa kiasi fulani na kuelezea vitu ambavyo vingeweza fanywa na hiyo hela kwenye maisha ya hao walalahoi. But you always here individual names ambao wapo involved na huo wizi. If anything this clarifies to us Makamba is right, ni wivu tu rather than real battle.

Kwa sababu lets face it asilimia kubwa ya hawa wapiganaji awako directly affected na consequences za upotevu wa hela i.e their kids still attend or attended better schools, wanakula vizuri na Tanesco wanapo leta giza wana majenereta ya kuleta mwanga, hivyo tabu za mtanzania kwa kweli sidhani kama wana zielewa. Na hu-sikii hi vita ikipelekwa kwa watanznaia, ni vita ya magazetini na bungeni lakini si vita ya kuhutubia watu hata elfu kumi pale mnazi mmoja. Sasa hii ni vita au wivu tu kama wanavyosema?

Mfano wa karibu majuzi tuliletewa post, ya hao waandishi walio fanyiwa huko loliondo na wanawake walioambiwa si watanzania, kisa pressure waliokua wanawaletea officials na abuse of human rights iliyotokea huko. Umeona hata post moja kutoka kwa wapambe wao walio ja humu ndani ya JF wakisema nini au hata kuwatetea hao waliokabwa na serikali. Ndio ujue ina make sense wanaposema ni wivu tu na wala si wapiganaji kama wanavyojidai its a fact and i will stand the ground until prove otherwise.
 
JC:

Kwa bahati tu kuna posti yenye kichwa:Rais Kikwete ndiye anayefaa kuongoza – Dk. Mwakyembe.

Labda hii ndio mikakati yenyewe. Lakini kama ulivyosema wengi wa wapiganaji wana nafasi zao. Hivyo kusema kuwa wanapigania maslahi ya wananchi ni kutowatendea walalahoi haki.

Kimbinu hakuna jitihada za pamoja na hakuna mission statement. Watu wanajihita wapiganaji lakini hakuna direction yoyote hile. Na hii inawakatisha tamaa wale ambao wako tayari kufanya mabadiliko.

Ningependa kusikiliza kutoka kwa wapiganaji wenyewe. Labda wakitambua matatizo yanayowakabili katika kambi zao wanaweza kutafuta mbinu mpya huku wakielewa mapungufu yao.

Kwa hapa JF ninachokiona ni intellectual discussions zisizoisha. Na wapiganaji wengine wako tayari kubadili majina hili ku-promote thread wanazoziona kuwa ni muhimu.
 
Vita ipo!
Lakini kutokana na nguvu za mafisadi, hata rafiki yangu Pinda anasema ni vigumu sana kuwamudu hawa watu!

Hapa JF vita dhidi ya Ufisadi ni kali sana, ndo maana wanapandikizwa mawakala wa MAFISADI kila mara kujaribu kupotosha mwelekeo...Lakini mi naamini katika WAKATI..na iko siku tutaibuka kidedea!
 
Vita ipo!
Lakini kutokana na nguvu za mafisadi, hata rafiki yangu Pinda anasema ni vigumu sana kuwamudu hawa watu!

Hapa JF vita dhidi ya Ufisadi ni kali sana, ndo maana wanapandikizwa mawakala wa MAFISADI kila mara kujaribu kupotosha mwelekeo...Lakini mi naamini katika WAKATI..na iko siku tutaibuka kidedea!

Maana ya vita si maneno mmjomba, ingekua hivo mpaka leo marekani na Iraq wangekua wanajibizana ina fika muda action has to be taken.

Sasa hawa wapiganaji kwa kweli wanachosha na maneno yao, sawa tumekubali hawapendezewi na muongozo wa sasa na tabia za viongozi wetu OK what next.

Yaani hata hilo kanisa katoliki lime-waonesha mfano, ingawa imeleta sokomoko la dini along the way, lakini imewapa mfano wa bure hii vita ni ya kumuelimisha mtanzania kwa lugha atakayo ielewa sasa hawa jamaa wanafanya nini kutwa walio CCM kujibizana na Makamba. Na walio CHADEMA ni Zitto, Zitto and Zitto. What about the people ambao wanadai wanataka kuwatendea haki, hapa ndio kama mtu huna akili timamu kwa kweli unaona ni mchezo tu.

Ukiangalia uchaguzi umebakia miezi tu wanampango gani, ndio kushinda labda ni too much asking lakini sidhani hata kama wana nia ya kuongeza idadi ya wabunge huko bungeni wapate sauti. Yaani they dont sell their policies enough to attract new members or potential scholars wajiunge kutwa Zitto,Zitto and more of the Zitto duh. What about chadema?

Zakumi

Kuhusu kubalisha mbinu hapo usitegeme mkuu kwani the motive ni bandia its obvious now, penye nia pana njia unaona kweli hawa jamaa wanataka mabadiliko ni wasomi hao wanajua vyanzo vya matatizo wangekua na nia ya kubadilisaha uongozi (CCM) wangeangaika kuwaelimisha watu kwanini CCM haifai kama kanisa lilivyojaribu.

Na wangekua na nia ya kuwadhibiti akina mafisadi wange angaika kuua nguvu zao, sheria za ajabu zinazo wafanye walinge nazo hao mafisadi, ambazo wanajua wazi so long the head of state is their man, hao wachukia ufisadi wanajisumbua tu. Je unaona hata siku moja hawa wakilia na sheria ambazo zina walinda no, lakini always wanalia na mafisadi kwa upande wangu ni wivu tu more than anything else.
 
Zakumi,

..mimi niliwashtukia 'wapiganaji' wa CCM pale walipoanza kudai ati JK naye anapinga ufisadi.

..wanaojiita 'wapiganaji' ni wana CCM walionyimwa madaraka na wanamtandao. sasa na wao wameanza kujipanga ili wawanyanganye tonge wanamtandao 2010 au 2015.

NB:

..kuna mambo mengi sana yanakwenda kombo nchi hii lakini watu wameng'ang'ana na ufisadi peke yake.
 
Bravo bravismo my brother from another mother aka Zakumi. You have said it better than I could have said it.
 
Baada ya kuwa mwangaliaji wa muda mrefu kuhusu masuala ya ufisadi, ningependa kusema kuwa hakuna kitu kinachoitwa vita dhidi ya ufisadi.

Haya ni maoni yangu binafsi na sina nia ya kuwakatisha tamaa wapiganaji au kuwafagilia mafisadi. Na maoni yangu yanatokana na ukweli kuwa vita vyovyote ni lazima viwe na viongozi, wapiganaji, mbinu za upiganaji na malengo ya kupigana vita hivyo.

Sasa tukija katika vita vya ufisadi, sioni viongozi wowote ambao wanaweza kuunganisha umma na wapiganaji hili kufikia malengo hayo. Mpaka sasa sijaona kiongozi yoyote anayekubalika.

Kuhusu wapiganaji. Hiki pia ni kikwazo. Wapiganaji wengi wanapigana vita vya mtu mmoja mmoja. Kwa maana kwamba kila mtu yupo tayari kutoa mawazo yake kwa kupitia waandishi wa habari, internet forums, blogs lakini hakuna nguvu ya pamoja. Hivyo muda mwingi unatumika kutoa new big ideas katika vyombo vya kutoa habari.

Mbinu zinazotumika ni zilezile wanazotumia mafisadi. Tena mafisadi wanazitumia kwa ufanisi mkubwa. Kwa mfano propaganda ni mbinu ambazo zinamlenga mlalahoi na sio profesa wa UDSM, au mchangiaji wa JF. Hivyo Makamba anaposema wanaopinga Serikali wanaona wivu kwa kukosa madaraka, anayemlenga ni mlalahoi ambaye siku ya uchaguzi ataipigia kura CCM. Hivyo wapiganaji walipo JF kuuliza elimu ya Makamba kutokana na kile alichosema ni kutojua uwanja wa mapambano huko wapi.

Malengo ya vita dhidi ya ufisadi ni finyu. Na kutokana na ufinyu huo, hata mbinu za kupiga vita vyenyewe zinakuwa na matatizo. Ufisadi unatokana na ukweli kuwa binadamu ni Greedy. Na njia pekee ya kupunguza greed ni kuwa na jumuia au taasisi zilizo transparent, zenye ku-check and balance uongozaji wa jumuia na zenye kufuata sheria.

Wenu

Z10

On paper all our institutions are very transparent, tatizo ni watendaji. Watendaji ni waoga na wala rushwa. Kuteteana na Uenzetu ni wingi sana, part of it nafikiri ni asili ya uafrika, kumkoma nyani ni vigumu.
 
Vita ipo!
Lakini kutokana na nguvu za mafisadi, hata rafiki yangu Pinda anasema ni vigumu sana kuwamudu hawa watu!

Hapa JF vita dhidi ya Ufisadi ni kali sana, ndo maana wanapandikizwa mawakala wa MAFISADI kila mara kujaribu kupotosha mwelekeo...Lakini mi naamini katika WAKATI..na iko siku tutaibuka kidedea!

PakaJimmy:

Unaposema kuwa vita vipo ni lazima kuwe na pande zaidi ya mbili zenye kupigana na zenye wapiganaji.

Ikifika point kuwa wapiganaji au majenerali wa vita wa pande zinazopingana ni walewale ujue hivyo sio vita tena.
 
Bravo bravismo my brother from another mother aka Zakumi. You have said it better than I could have said it.

Bro Juli:

Inspiration sio lazima itoke mbali. That slogan Miafrika Ndivyo Ilivyo has inspired me.

Nimeshahamua kutofautisha quests, commitments na longolongo. Mambo mengi yanayoendeshwa na watanzania ni longolongo na wakati ukipita wanatafuta longolongo jingine.
 
Bro Juli:

Inspiration sio lazima itoke mbali. That slogan Miafrika Ndivyo Ilivyo has inspired me.

That's the dirty little secret about that slogan, to inspire folks to do better, to go above and beyond, and in the process we all benefit. Let's face it, who likes to be known as loser? I sure don't as do many other people. I often thrive in adversity. I like it when people doubt me. Doubters motivate me to prove them wrong which in turn brings the best out of me. If I as a person can use my haters as my motivators, Africans as a whole and Tanzanians in particular can use that slogan as their motivator too.
 
Zakumi,

..mimi niliwashtukia 'wapiganaji' wa CCM pale walipoanza kudai ati JK naye anapinga ufisadi.

..wanaojiita 'wapiganaji' ni wana CCM walionyimwa madaraka na wanamtandao. sasa na wao wameanza kujipanga ili wawanyanganye tonge wanamtandao 2010 au 2015.

NB:

..kuna mambo mengi sana yanakwenda kombo nchi hii lakini watu wameng'ang'ana na ufisadi peke yake.


JKuu:

Nilikuwa naelekea huko. Na hii inatokana na kikao cha NEC kilichopita ambacho mwenyekiti alihamua kuwaachia watu watoe yaliyomo moyoni.

Kwa sisi wa kawaida zilionekana pumba. Lakini ukichukulia maanani kwamba Mkapa alisimama na kupigia makofi mjumbe mmoja aliyesimama kutoa pumba zake basi hapo kuna mambo ambayo yanaendelea ambayo sisi wakawaida hatuyajuhi.

Na kongamano la Mwalimu linaonyesha kuna mgawanyiko ndani ya CCM. Na mgawanyiko huo unawafanya watu wawe wapiganaji. Lakini wangekuwa madarakani wangekuwa wanampigia propaganda JK.
 
Baada ya kuwa mwangaliaji wa muda mrefu kuhusu masuala ya ufisadi, ningependa kusema kuwa hakuna kitu kinachoitwa vita dhidi ya ufisadi.

Haya ni maoni yangu binafsi na sina nia ya kuwakatisha tamaa wapiganaji au kuwafagilia mafisadi. Na maoni yangu yanatokana na ukweli kuwa vita vyovyote ni lazima viwe na viongozi, wapiganaji, mbinu za upiganaji na malengo ya kupigana vita hivyo.

Sasa tukija katika vita vya ufisadi, sioni viongozi wowote ambao wanaweza kuunganisha umma na wapiganaji hili kufikia malengo hayo. Mpaka sasa sijaona kiongozi yoyote anayekubalika.

Kuhusu wapiganaji. Hiki pia ni kikwazo. Wapiganaji wengi wanapigana vita vya mtu mmoja mmoja. Kwa maana kwamba kila mtu yupo tayari kutoa mawazo yake kwa kupitia waandishi wa habari, internet forums, blogs lakini hakuna nguvu ya pamoja. Hivyo muda mwingi unatumika kutoa new big ideas katika vyombo vya kutoa habari.

Mbinu zinazotumika ni zilezile wanazotumia mafisadi. Tena mafisadi wanazitumia kwa ufanisi mkubwa. Kwa mfano propaganda ni mbinu ambazo zinamlenga mlalahoi na sio profesa wa UDSM, au mchangiaji wa JF. Hivyo Makamba anaposema wanaopinga Serikali wanaona wivu kwa kukosa madaraka, anayemlenga ni mlalahoi ambaye siku ya uchaguzi ataipigia kura CCM. Hivyo wapiganaji walipo JF kuuliza elimu ya Makamba kutokana na kile alichosema ni kutojua uwanja wa mapambano huko wapi.

Malengo ya vita dhidi ya ufisadi ni finyu. Na kutokana na ufinyu huo, hata mbinu za kupiga vita vyenyewe zinakuwa na matatizo. Ufisadi unatokana na ukweli kuwa binadamu ni Greedy. Na njia pekee ya kupunguza greed ni kuwa na jumuia au taasisi zilizo transparent, zenye ku-check and balance uongozaji wa jumuia na zenye kufuata sheria.

Wenu

Z10

Thinker Z10,

I am not sure kama siasa ni njia nzuri ya kukabiliana na ufisadi. Kwa upande wangu nadhani kuwategemea wanasiasa kuisafisha nchi yetu na madhila ya ufisadi na udhalimu mwingine wa watawala, ni sawa na kupanda chelewa na kutarajia utachipua mnazi. This is just not happening.

I don't know about many things, but I know one thing I know for sure ni kuwa ufisadi ni criminal offence, na hakuna siasa hapo. Jawabu pekee la tatizo la ufisadi kama ulivyoelezea mwishoni, ni kuwa na system nzuri ya judiciary ambayo ni competitive, independent, inayoji-self check, ambayo ni msumeno kwa yeyote regardless, etc..Ukiwa na system kama hiyo, ika-balance na system nyingine nzuri ya executives, civil societies, pressure groups na legislation.
 
On paper all our institutions are very transparent, tatizo ni watendaji. Watendaji ni waoga na wala rushwa. Kuteteana na Uenzetu ni wingi sana, part of it nafikiri ni asili ya uafrika, kumkoma nyani ni vigumu.

I am not sure if they are transparent. But we should note that transparency or excellency doesnt fall from outer space. Therefore, in any community or country, one generation has to set standards that others would follow and perfect. Unfortunately, I am ashamed to say, we have settled for mediocrity.
 
Thinker Z10,

I am not sure kama siasa ni njia nzuri ya kukabiliana na ufisadi. Kwa upande wangu nadhani kuwategemea wanasiasa kuisafisha nchi yetu na madhila ya ufisadi na udhalimu mwingine wa watawala, ni sawa na kupanda chelewa na kutarajia utachipua mnazi. This is just not happening.

I don't know about many things, but I know one thing I know for sure ni kuwa ufisadi ni criminal offence, na hakuna siasa hapo. Jawabu pekee la tatizo la ufisadi kama ulivyoelezea mwishoni, ni kuwa na system nzuri ya judiciary ambayo ni competitive, independent, inayoji-self check, ambayo ni msumeno kwa yeyote regardless, etc..Ukiwa na system kama hiyo, ika-balance na system nyingine nzuri ya executives, civil societies, pressure groups na legislation.


Nakusikia Mkuu:

Nilisoma shule alizoacha mkoloni. Hivyo tulikuwa na maktaba shuleni. Kuna kitabu kimoja cha hadithi kinasema kuwa kipofu alipewa zawadi ya kuona kwa dakika moja. Katika dakika hiyo moja mnyama mkubwa aliyemuona alikuwa Punda. Hivyo kila watu wakizungumza kuhusu wanyawa, kipofu huyo ataleta ubishi kama wanyama hao wanamzidi ukubwa punda.

Siasa na watanzania ni sawa na kipofu wangu na ukubwa wa punda. Toka tomepata uhuru, siasa is the best thing we have ever learned.

Juhusi za kumwambia mtanzania kuwa kuna vyombo vingine vinavyoweza kutusaidia katika matatizo ya ufisadi kuliko siasa ni sawa kujaribu kumshawishi kipofu wangu kuwa tembo ni mkubwa kuliko punda.

Kuna siku Kikwete alitoa ahadi kuwa hawezi kubadilisha sheria za uchaguzi wakati uchaguzi umeshapita. Lakini kwenye uchaguzi unaokuja, sheria zitabadilika hili watu wasichanganye biashara na siasa. Tungembana hapa ingekuwa ize. Lakini tumesahau na kuendeleza ushabiki.
 
Back
Top Bottom