Hivi viongozi wetu wa awamu ya 5 wana watoto kweli?

Jimmy George

JF-Expert Member
Nov 28, 2016
1,733
1,643
Habari za asubuhi wana JF,

Mi nakaa najiuliza hawa viongozi wetu wa awamu hii ni kweli wana watoto wa kuzaa wenyewe? Swali langu linatokana na haya yafuatayo;

1. Mwaka mzima watu wanasubiri ajira hata hawana mpango wa kutoa zaidi ya kutoa sababu kibao.
2. Kutoa matamko mengi ambayo mengi yana athari kwa wananchi lakini wao hawajali.
3. Wanafunzi kukosa mikopo.
4. Kumjali faru John kuliko miili saba ya watu kule Ruvu.
5. Kutotoa fedha za maafa kule Kagera.
6. Kutumbua watu hata kwa makosa yanayohitaji kuonya.
7. Kukamata watu kama Mr Melo na kuwaweka ndani eti kisa wanaonekana. kwenda kinyume na serikali.
8. Bomoabomoa nyumba za wananchi ambazo hazikustahili kubomolewa lakini viongozi hawaonyeshi kushtuka.

Na kama watakuwa na watoto basi mi naweza kusema;
1. Hawana upendo.
2. Wana ubinafsi.
3. Siyo watu wa kujali shida za wengine.
4. Wapo kimaslahi.
5. Wanafki.
 
Watoto wanao mbona yupo j! halafu umesema kama wanao...?
 
Ajira Mara baada ya kukamilika kwa uhakiki nafikir serikali yetu iko makin na niwaelewa, xo ajira Nina iman watatoa 2 kuwa na subira
 
Habari za asubuhi wana JF mi nakaa najiuliza hawa viongozi wetu wa awamu hii ni kweli wana watoto wa kuzaa wenyewe ? Swali langu linatokana na haya yafuatayo;
1. Mwaka mzima watu wanasubiri ajira hata hawana mpango wa kutoa zaidi ya kutoa sababu kibao
2. Kutoa matamko mengi ambayo mengi yana athari kwa wananchi lakini wao hawajali
3. Wanafunzi kukosa mikopo
4. Kumjali faru John kuliko miili saba ya watu kule Ruvu
5. Kutotoa fedha za maafa kule Kagera
6. Kutumbua watu hata kwa makosa yanayohitaji kuonya
7. Kukamata watu kama Mr Melo na kuwaweka ndani eti kisa wanaonekana kwenda kinyume na serikali
8. Bomoabomoa nyumba za wananchi ambazo hazikustahili kubomolewa lakini viongozi hawaonyeshi kushtuka



Na kama watakuwa na watoto basi mi naweza kusema
1. Hawana upendo
2. Wana ubinafsi
3. Siyo watu wa kujali shida za wengine
4. Wapo kimaslahi
5. Wanafki
zingatia na uufanyie kazi ushauri huu hapa --> [HASHTAG]#usirudiekosa2020[/HASHTAG]
 
Ajira Mara baada ya kukamilika kwa uhakiki nafikir serikali yetu iko makin na niwaelewa, xo ajira Nina iman watatoa 2 kuwa na subira
Mi naona ni danadana wanatupiga
1. Mwezi wa 5 walisema ajira zitatoka bajeti ikipita July
2. Kabla ya mwezi wa 7 wakasema tunahakiki watumishi hewa na Mhe. Rais akasema itadumu miezi miwili tu
3. Mwezi wa 9 wakasema wanahakiki vyeti feki ndiyo sielewi cjui wanahakiki mpaka leo

Kwa waalimu tarajali ndiyo hao wameambiwa sayansi na hisabati watume vyeti wahakiki ambapo najua mpaka mwezi wa pili watasema wanahakiki tu
 
Ajira Mara baada ya kukamilika kwa uhakiki nafikir serikali yetu iko makin na niwaelewa, xo ajira Nina iman watatoa 2 kuwa na subira
Hiyo subira unaijua? Mbona mnajitoa ufahamu sana. Kwenye mambo mazito mnatoa majibu mepes kbsa. Aliyeshiba hamkumbuki mwenye njaa
 
Sio kwamba wanapenda! Usiwalaumu sana ukipata muda ukaongea nao utawasikia ya moyoni mwao na utawaonea Huruma pia
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom