Hivi vilikuwa vitisho tu vya JK, Kwa Mawaziri.Makatibu wakuu, na wengine.

Hasara

Senior Member
Dec 29, 2006
138
9
Baada ya JK Kuukwa Urais alitoa kauli NZITO ambayo wengi waliogopa tunaona ilikuwa vitisho, na Semina Elekezi, kwa Mawaziri na ,Makatibu Wakuu, Ma-dc, na Wakuu wa Mikoa, ukweli ndiyo huu unaonekana yeye na wasaidizi wake.

mkuu huyu alitamka kwa kauli yake nina nukuu kusema JK ,kuna nitakao maliza nao miaka mitano na kuna ambao sinta malizanao wengine hawata fikisha hata mwaka au miwili na kuna ambao nita maliza nao , sasa jamani kwa mwendo huu siatamaliza na wote, nikuamishwa tu ndiyo kina chofanyika ,
Tufuatilie kauli zote alizo sema kama hii ni moja zingineni-
--Kuhusu muhafaka huko Zanzibar
--Kurudia mikataba
--Ruswa
--Madawa ya kulevya
--Majambazi
--Nyumba za serikali
--na nyingine ziwekeni hapa tuzijadili kwa pamoja.
WanaJF hili nyiye mnalionaje atamaliza na wote au hii kauli ilikuwa matisho tu?

asanteni
 
Muungwana anajua sana kucheza na Lugha,na kuuza Uzuri wake kwa Watanzania wenye Njaa na kiu kubwa ya MAENDELEO.Kila apandapo Jukwaani anakuja na ujanja mpya wa Kudanganya Wadanganyika.

Ndg Hasara haya yana mwisho!!,Huwezi kuwadanganya watu kila siku,ni miaka miwili sasa tumekuwa tunavumilia Uongo Huu wa Mtu mzima!,Si Utamaduni wetu kumwambia mkubwa Umeongopa,lakini sasa tunashindwa uvumilivu,kwani Uongo umekuwa Dhahiri na unarudiwa kila kukicha.Ni nani alijua kuwa JK atagomewa kuingia kwenye maeneo ya wananchi?(Buzwagi), au nani alijua kuwa itafika siku Viongozi watazomewa na wananchi?Huo ni uthibitisho tosha kwamba wananchi wamechoka.

Utakuja pigwa na Butwaa siku za karibuni kuona kwamba Mikutano ya Waheshimiwa inasusiwa na wananchi,au Kiongozi kushushwa Jukwaani na mawe,kwani watu wakikata tamaa uoga huondoka!!

Ndg Hasara ktk Thread yako ya Msingi unauliza kama JK atamaliza kipindi chake na hawa Wezi, Mafisadi,Wazandiki na Mafirauni waliojaa kwenye seikali yake,Jibu ni kwamba inawezekana kabisa akamaliza nao,kwa sababu inaonekana wanazungumza Lugha moja wakiwa chumbani,Lakini Muungwana akitoka nje anakuja na Lugha ya kututapeli sisi wadanganyika!,Nakuthibitishia hapa kuwa Muungwana akiendelea kwa Mwendo huu (kasi mpya),itakuwa ni Rais pekee kukaa kwenye Madaraka kwa kipindi kimoja (5yrs).

Kikwete amekuwa mchemkaji kuliko Viongozi wote waliowahi kupita ktk nafasi hiyo.Hatutaki/Tunaogopa kusema ukweli lakini ni wazi kuwa Nchi Mmemshinda.Naomba kutoa Hoja!!!
 
Hasara, naona mawazo yamegongana, maana nilikuwa napitia hotuba ya JK Ngurdoto, nikataka niibandike hapa, nashukuru umeanzisha mada hii kwani ukishaisoma hotuba hii angalia yanayosemwa na kufanywa utajua kama ile semina elekezi iliwaelekeza lolote!
 

Attachments

  • seminangurdoto.pdf
    39.7 KB · Views: 130
Mkuu Mwanakijiji
nadhani ngurudoto walienda kupongezana kwa kishindo cha ushindi. Sidhani kama kiongozi timamu anapaswa kukumbushwa wajibu wake kwani ktk ilani ya chama chake ndiyo wajibu tosha. walienda kula fungate la ushindi. Nimesoma hotuba na inashangaza sana kuona hakuna kilichotekelezwa zaidi ya kuboresha ulaji wao...
 
Hiki ni ichekesho yaani pesa ya walipa kodi inakwenda kuchezewa pale Ngurdoto halafu nasema yuko serious kukwamua matatizo ya WTZ, what a joke! Huna sababu ya kwenda mahali expensive kama pale unapotaka kuwaweka sawa watendaji wa serikali.

Limbukeni hana siri.
 
Naskia makaburi yanafukuliwa? ...tuwe makini tusije shindwa kuyafukia kwa sababu ya harufu na uvundo wake....
 
Back
Top Bottom