shiumiti
JF-Expert Member
- Jun 4, 2009
- 435
- 19
Wapendwa wangu Great Thinkers...mimi katika kufuatilia sana utendaji wa hawa wawili, nimegundua kwamba Mh. Makamba ni kiongozi ambae maneno yake huwa yanamashaka sana. Kwa mfano:
Naomba kutoa hoja......
- Kuna kipindi alikuwa anahutubia wananchi kule Tarime...akisisitiza kuwa Nanukuu "SISIEM na viongozi wake wanadhamira ya dhati kuondoa umaskini kwa Watanzania, lakini kwanza lazima waondoe umaskini wao viongozi kwanza".
- Juzi juzi wakati wa uchaguzi, NEC iliamua (yeye ni mjumbe pia) kura zinapigwa na watu wenye shahada tu. Yeye kama Makamba Kama Katibu Mkuu wa SISEM alisikika akisema, nanukuu "hata mwanachama mwenye Kadi ya SISIEM (sharti iwe ni kadi hai) anaweza kupiga kura"
- Leo kwenye taarifa ya habari nimesikia pia anasema, nanukuu "SISIEM haiwezi kukaa meza moja na CHADEMA kujadili mgogoro wa Meya mjini Arusha kwa sababu Meya wa Arusha ameshinda kihalali". Wakati huo huo Makamu wa MWenyekiti wa SISIEM anasema Mkuu wa Nchi amesikitishwa sana, na inaweza pelekea Kamati Kuu ya SISIEM Kukutana na kujadili.
Naomba kutoa hoja......