G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Mbunge umehamia CCM tena unawatukana waliokupa ridhaa ya chama kugombea. Unatukana sana huku unajisahau kuwa unaenda kugombea ubunge kwa tiketi ya chama ambacho umehamia juzi. Chama ambacho unaenda kukutana na magwiji ha propaganda chafu yaliyojipanga tangia 2016.
Nawaambieni mtapata tabu sana. Kwanza mtatukanwa matusi haya haya mnayotukana sasa! Mtachambwa na mwisho hamtapita hata mmoja wenu kwenye kura za maoni.
Mnajisahau sana, mnapata kiburi sana ila muda utaongea. Nyie ni mazuzu yasiyoona mbele na kwa hakika mtakuja kujikuta mnamlalamikia tena huyu huyu anayewaita kwake ila kwa wakati huo hakuna wa kuwasikilizeni maana kila mtu atakuwa anapambana na hali yake. Kwa sasa nyie jitoeni ufahamu vya kutosha kabisa!
Na ikiwa kamati kuu itajifanya ubabe na kuwapa ugombea kinguvu basi yatakayofuatia yatafurahisha sana.
Nimwambie tu Rais Magufuli kuwa anachokijenga sasa na kwa miaka minne iliyopita ndicho atakachokiona kwenye uchaguzi mkuu na kuanzia mwaka 2021. Hapo ndipo atajua kuwa kumbe ubabe si kitu chochote mbele ya siasa! Tukutane ulingoni palipojaa umamluki, fitina, uchawi, uuwaji na kila aina ya takataka linalojulikana.
Ulingoni si mbali kutoka sasa.
Nawaambieni mtapata tabu sana. Kwanza mtatukanwa matusi haya haya mnayotukana sasa! Mtachambwa na mwisho hamtapita hata mmoja wenu kwenye kura za maoni.
Mnajisahau sana, mnapata kiburi sana ila muda utaongea. Nyie ni mazuzu yasiyoona mbele na kwa hakika mtakuja kujikuta mnamlalamikia tena huyu huyu anayewaita kwake ila kwa wakati huo hakuna wa kuwasikilizeni maana kila mtu atakuwa anapambana na hali yake. Kwa sasa nyie jitoeni ufahamu vya kutosha kabisa!
Na ikiwa kamati kuu itajifanya ubabe na kuwapa ugombea kinguvu basi yatakayofuatia yatafurahisha sana.
Nimwambie tu Rais Magufuli kuwa anachokijenga sasa na kwa miaka minne iliyopita ndicho atakachokiona kwenye uchaguzi mkuu na kuanzia mwaka 2021. Hapo ndipo atajua kuwa kumbe ubabe si kitu chochote mbele ya siasa! Tukutane ulingoni palipojaa umamluki, fitina, uchawi, uuwaji na kila aina ya takataka linalojulikana.
Ulingoni si mbali kutoka sasa.