Hivi unaweza kupuliza dawa ikiwa bado watu wanarandaranda mtaani?

ego

JF-Expert Member
Apr 10, 2013
1,620
1,407
Dar wametangaza kupuliza dawa mitaani jamani, jamani!

Sina uhakika na hiki wanachotaka kufanya Dar. Je, kinafanywa kwa utaratibu gani, lakini nahisi kuna shida.

Mimi sio mtaalamu wa afya lakini nahisi tunaweza kufanya vitu ambavyo tutatumia gharama lakini hatutapambana na korona.

Corona haizururi mitaani bali inasambazwa na watu, inatembea na watu na ninavyoijua Dar dawa haiwezi kupulizwa kila mtaa bali kutapulizwa maeneo fulani tu.

Lakini nahisi wale ambao wanabaini virusi vimeingia katika miji yao wanachokifanya

1. Ni kutangaza watu wakae majumbani mwao kwa siku kadhaa. maana yake unaondoa miingiliano ya watu. Kama kuna watu walikuwa na ugonjwa tayari basi ndani ya kipindi hicho watabainika na watapelekwa hospitali. Watu waliokuwa wamewazunguka watafuatiliwa kama ni familia na nyumba inaweza kupuliziwa dawa.

2. Mitani na hasa sehemu hatarishi ambazo watu wanakusanyika wengi zinapuliziwa dawa ili kama kuna sehemu virusi bado vimejibanza basi vinaangamizwa.

Ni lazima ufunge mipaka kuzuia wageni kukuletea ugonjwa tena. Inashangaza Dar bado wageni wanaingia, watu wanarandaranda mitaani, viongozi wanatuhamasisha kukusanyika kwa shughuli za ibada alafu wanatangaza kupuliza dawa.

Tusikopi vitu kwa kuwa tumeona watu wanafanya kitu fulani basi tunaiga na katika kuiga tunaonyesha jinsi gani tulivyo ama makini au tusivyo makini.

Ninatumaini upuliziaji uko well planned.
 
Wewe ndiye muingizaji no.1, fumingation inasaidia sana tena sana, na wakati wowote. Unapo ona ufa kwenye ukuta wako, basi ujue hiyo ni fursa ku,iba nyufa zote
 
Wewe ndiye muingizaji no.1, fumingation inasaidia sana tena sana, na wakati wowote. Unapo ona ufa kwenye ukuta wako, basi ujue hiyo ni fursa ku,iba nyufa zote
Hili ni tatizo la elimu zetu, hatuwazi kile tunachopambana nacho ni kitu gani tunabaki kwenye general "fumigation"

its like mtu kuamini unaweza kufanya fumigation ukatokomeza ukimwi

wapo wadudu unaweza kufanya fumigation ukawaangamiza lakini nature ya hawa wanakaa wapi na wanaenea vipi fumigation ni supporting mechanism.

uniambie ni kwa jinsi gani fumigation iliyofanyika mitaani itakavyoweza kutokomeza virusi vya korona ambavyo viko kwa watu?

kama tunatokomeza malaria mfano tunajua vector ni mbu, tunafanya fumigation kutokomeza vector ambaye anaeneza na tukisha mtokomeza huyo wale waliougua hawatapona kwa fumigation, watapona kwa dawa ila tunajua kuambukiza hakupo.

sasa unafanya fumigation mitaani, wagonjwa bado wapo uniambie ni kwa vipi fumigation hii itazuia mtu mwenye maambukizi kumuambukiza ambaye ahana maambukizi.

Nini Cha kufanya,

narudia

1. Wenzetu wanaweka karantini kwanza. ukiweka karantini ni sawa na kutokomeza mbu. yaani unazuia wanadamu kukutana maana yake unazuia njia za maambukizi ili kusitokee maambukizi mengine.

2. Nini kinatokea kwa hawa uliowaweka karantini, ni lazima mda wa karantini uwe ni mda mrefu ambao una uhakika waathirika wote wa korona watakuwa wameanza kuugua. hivyo wakiwa karantini ni lazima kuweka utaratibu wa watu kwenda hospitali wanapojisikia dalili na ikiwezekana kama public transport hazifanyi kazi basi kila mahali kuandaliwe huduma ya kuchukua wagonjwa majumbani mwao na kuwapeleka maeneo ya kupima na kupata huduma.

3. Tusisahau huduma hizi za usafiri ziwe na usafi wa hali ya juu ili zisiwe chanzo cha kusambaza. kila likipeleka mgonjwa linapuliziwa dawa ndio linarudi kuchukuwa wengine

4. Unakuwa na uhakika kuwa katika kipindi kile cha karantini, wagonjwa wote watabainika na kupelekwa sehemu za huduma na maeneo waliyokuwemo yanafanyiwa usafi ili kuua vimelea.

5. upo uwezekano kuwa kuna maeneo ya mitaani ambayo tayari yana virusi hawa, hapo sasa ndio fumigation inafanyika kutokomeza.

Fumigation as fumigation bila mikakati tangulizi haiwezi kutokomeza corona iliyoko kwa mtu fulani ambaye anayo katika jamii na haiwezi kuzuia mtu huyo kuambukiza wengine isipokuwa tu hawezi kuambukiza kupitia kitu kilichofanyiwa fumigation.
 
Back
Top Bottom