ukiuza vitu mtandaoni bila kuwa na ofisi unaweza pata leseni ya biashara?
Shukrani sana
- Ndio
- Unaweza pata leseni ya biashara.
Biashara mtandaoni kwa sasa ni rasmi inatambulika.
Je nini unatakiwa kuwa nacho ili upate leseni ya biashara kwa shughuli unayofanya mtandaoni.
#1. Hakikisha unakuwa na TIN number
#2. Hakikisha unakuwa na anwani yako ( fika posta wakupe Box number yako, utakayotumia kujaza kwenye docs. mablimbali )
#3. Hakikisha unakuwa na Jina la biashara yako
Kwa msaada zaidi muone Afisa biashara wa wilaya uliyopo.