Hivi unajua unaweza kutumia akili kidogo tu ukapata pesa nyingi?

Mii nilishafanya hii biashara ya kukodisha vitu tangu mwaka 2001-2003.
Karibu na pale mbezi Sasa kimejengwa kituo Cha mabasi. Niliweka mashine za kupiga matofali, vibao vya matofali, manailoni ya kufunika matofali ikija mvua.
Pia nilikuwa na welding machine 4 niliziweka hapa Sinza kwa Remmy Sasa Pana ukumbi unaitwa majestic hall. Nilikuwa nawakodisha mafundi uchomeleaji.
Nikawa na guta 2 zilikuwa zinapaki manzese.
Ic matumizi ya hivi vitu daah. Mtu akichukua kitu chako anavyokitumia yaani anakikomesha.
Hazingatii uwezo wa kitendea kazi. Mashine ndogo ya welding anataka aweke Moto mpaka mwisho ili skate chuma wakati Ile niya kuungia chuma na sio kukatia.

Baadae nilianza kukodisha screen kwaajili ya kombe la dunia Kama mtakumbuka mwaka 2002 world cup ilifanyika Japan na Korea. Jamaa walikodi mwezi mzima, lkn ilibidi wavunje mkataba kwa sababu hawakuwa na wateja maana mechi zilikuwa zinachezwa alfajili.

Ninachotaka kusema hapa unatakiwa kuwa makini Sana na kifaa chako. Matumizi ya wanaokodi huwa Ni mkomoeni. Vinginevyo kifaa chako kitachakaa kabla ya kukulipa..
Unaweza kukuta chombo kimewekwa upside down. Kipo kwenye vumbi, yaani unaweza kulia.

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeongea point ya muhimu sana hapa.Mimi nilikuwa nilinunua bodaboda used lakin ilikuwa imetumika kidogo maana mshua yule alimnunulia mtoto wake wa kiume ila dogo ubishoo wake akakataa kuwa bodaboda.Mshua akapaki mzigo hatimaye akatuuzia.
Tukatafuta kijana mmoja wa kanisani akawa bishoo akashindwa hata kupata 40 au 50 elfu kwa wiki wakti ndo bei ya kawaida kwa bodaboda alichofanya bila kukutaarifu sisi nae akawa anampa mshikaji wake ambaye wanafahamiana.Wakaanza kuikongoloa yani full kupiga pesa halafu kwetu wanaleta matatizo tu mara leo sijui blaabla tu kila wiki tena wanaleta blabla siku ya kukabidhi pesa,sasa yukawa tunajiuliza kwa nini wasiyutaalifu mapema?
Baadae mi na jamaa yangu tukachoka tukawanyang'anya pikipiki baada ya wiki kadhaa tukasikia mshikaji tuliyempa saiz kanunua yake,inamaana alikuwa anaficha hela ili aongezee anunue yake.Tukatafuta kijana mwingine ni mwaminifu na anatupa kiasi tunachotaka na kukitokea hitilafu kabla ya jumapili anatutaalifu na kwa ushahidi unaoonekana.

Kwa hiyo ukinunua, kitu kama ukampa mtu akusaidie kuendesha halafu akulipe kias kadhaa hakikisha unakuwa mfuatiliaji(management)na wakati mwingine unamwongoza(leadership)mfano kufanyia ukarabati chombo n.k.Sisi hatukufanya yote hayo kwa sababu tulikuwa wote wanafunzi mwaka wa 1 na jamaa yangu mwaka wa 3.Saiz jamaa amemaliza na yuko huru anaguatilia vizuri sana na kila hatua yuko nao.Saizi faida inapatikana.Ila ukiwa mwanafunzi au mfanyakazi kutwa kazini au chuoni basi hakikisha hata akisema amenunua sijui nini mwambie apige picha atume whatsup uone mwenyewe lakin kama yuko mbali na anauhakika humchunguzi anakuambia tu leo nimenunua helmet mpya ya abiria kumbe mwongo tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila mtu anawaza pesa, kila mtu kichwa chake ina picha ya mafanikio na asilimi 90% ya hawa watu wote wanaowaza pesa na mafanikio na maisha mazuri hufikiri pesa inapatikana kwa kufanya biashara tu, labda auze kitu fulani ndipo apate pesa.

Kuna njia nyingi za kupata pesa kwa wewe ulie na mtaji, hapo ulipo unaweza ukawa na pesa yako ila hujui uifanyie biashara gani au labda muda wa kusimamia hiyo biashara kwako ukawa mdogo hivyo unaogopa na hujui cha kufanya.

Sasa sikia leo nitakupa list ya vitu vya kufanya ujitoe na stress. Kuna watu najua hata tuongee na maturumbeta tupige ila hampo tayari kuacha kazi mnazofanya mjiajiri ila mpo tayari kuanzisha biashra ikafa, mkafungua ingine ikafa mkafungua tena na tena hamchoki ila sio eti mjiajiri najua mpo.

Sasa najua kuna watu mmeshajaribu kufungua biashara nyingi sana na mwsho kwasababu ya usimamizi biashara zote zimekufa, mmechoka na mmekata tamaa hamjui mfanye nini, hamna shida soma nitakavyoviandika leo kisha chomoka na kimoja kakifanyie kazi.

Leo naongelea biashara ya KUKODISHA VITU

Najua unaweza jiuliza utakodisha nini na kinauzwaje na kinakodishwaje,mimi leo ntawapa mfano ya ninavyovijua tu na ambavyo nina uhakika navyo, hivyo kama na wewe utapata idea usiache itoa yako ili namimi niipate nione nafanyaje.

1. VIBANDA VYA TIGO PESA
Nadhani wewe ni shahidi ya Mawakala wangapi unawakuta na miamvuli huko barabarani, nataka kukwambia kitu hao Mawakala sio kwamba wanapenda kukaa na miamvuli na meza tu ila sababu ni kwamba hana pesa ya kutengeneza kibanda,chakufanya wewe tengeneza kibanda kidogo cha wakala wa Tigo Pesa ambacho gharama yake kuanzia mabati, bomba mpaka kinakamilika ni 250,000 kwa kibanda kimoja, ina maana kama una Milioni 1 una uwezo wa kutengeneza vibanda vinne vilivyokamilika imebaki mtu kuchukua kwenda kufanyia kazi.

Kodi ya kukodisha hivi vibanda kimoja kwa mwezi ni 20,000 ina maana kwa vibanda vyako vinne una uhakika wa 80,000 kila mwezi hiyo ni uhakika yaani, sio ya kutafuta au kupigizana kelele na mtu na uchukuaji kodi wa hivi vibanda ni wa mwezi mtu akupe kodi ya mwezi tu kisha apige zake kazi.

2. BANDA LA BIASHARA
Hili banda halina utofauti na hilo banda la tigo pesa hapo juu tofauti yake ni ukubwa, kutegemea na uwezo wako ila kwa banda la ukubwa waupana futi 5 na urefu kwa futi 10 gharama ya ujenzi wa hili banda ni 500,000 hivyo ukiwa zako na 1M utaweza tengeneza mabanda mawili ambayo utayakodisha kwa wanaotaka yakodi bei yake kwa mwezi 30,000 to 50,000 kodi itategemea na wapi unaenda kumuwekea hilo banda, ukienda liweka sehemu nzuri kodi utaweza kumpa hata 60k to 100k na akalipa bila shida maana eneo hilo frem kodi ni 300k kwenda mbele. Assume una mabanda yako mawili ya kodi 50k kwa mwezi utakua unaingiza 100,000 isiyo na maelezo.

3. MASHINE YA KUCHOMELEA
Hizi mashine zipo za aina mbili kuna zile portable za kubeba halafu kuna yale transforma lake limesukwa na nyaya za aluminum, bei ya kuyanunua haya

- Portable: 400,000
- Kusuka: 300,000

Kukodisha haya ma mashine ni kwa masaaa 6 na masaa 12, kuna bei ya 6hrs na bei ya 12 hours, bei yake kwa 6hrs 20,000 na 12hours ni 30,000, ila kwa mashine portable 6hrs ni 30,000 na 12hrs 40,000.

Calculate hapo uone kwa siku utakuwa unaingiza sh ngapi, hii biashara ukijuana na mafundi welding kazi zitakuwa kila siku 5000 elfu kumi vitakuwa havikauki kwenye wallet/ pochi yako kiufupi huwezi kuwa na shida ndogondogo.

4. MUZIKI SPEAKER ZILE ZA KUCHOMEKA FLASH
Hizi speaker nilijaribu kununua kwa ajili ya ki pub changu uchwara fulani hivi sikuwaza kama hizi speaker ni dili basi wateja wale wale wakawa wakija wakisikia muziki wake wananiuliza kama nakodisha nikaanzaga zikodisha kama utani kwnye visherehe vya birthday huko mitaani, bei ni 50,000 kwa event 1 kiukweli hamnaga weekend hizi speaker nakosa simu ya kuombwa watu wakizitaka maana watu n wana sherehe kila leo na miziki yao ya subwoofer haitoshelezi haja zao.

Zitafute hizi speaker zinunue usiogope hela yako itarudi bila wasi wasi, zipo size tofauti ila kwakuwa unataka ya kibiashara nunua ya 600k to 700k hapo utapata heavy weight mziki kwa shughuli za mitaani, mfano ni kama hii Ailipu hapa chini japo kampuni zipo kibao zinazotengeneza hii mispika ya hivi.


5. KABATI ZA ALUMINIUM
Umeshaenda kununua chips mahali? Umeshaona chipsi zinawekwa kwenye nini? Basi tengeneza yale makabati nakuhakikishia hamna kikwazo kikubwa kwenye biashara ya chipsi kama KABATI Zero IQ ni shahidi muulizeni awambie mtu ataweza jidunduliza anunue kila kitu ila mtihani ukaja kwenye kabati.

Sasa tengeneza makabati yako ya 200,000 tengeneza makabati manne kisha yaweke mahali andika yanakodishwa, humalizi masaa 24 tayari ushapata mteja, haya makabati bei yake kabati per day ni 2000 maana yake kabati 1 kwa mwezi litakupa 60,000 x 4 = 240,000

Unaweza amua tengeneza vikabati vidogo kwa ajili ya mtu kuweka kachumbari na vitu vidogo vidogo ambavyo bei ya kabati kutengeneza ni 150,000 kisha wewe utalikodisha kwa 1000 per day x 30 days = 30,000 x 4(idadi ya makabati) = 120,000 kwa mwezi jumlisha bei ya makabati yako yote uone utakua na kiasi gani.

6. JENERETA
Kwa Tanzania yetu hii ndugu zanguni hii ni biashara nzuri sana, sijui kama utanielewa ila hii ni biashara ambayo ataekufata/ kukupigia simu unamtajia bei huku unakula karanga zako na hawezi kataaa wateja wapo kibao tena wengi tu, vuta picha watu wamekuja kwako kukodisha zile spika plus jenereta yani hela utayoingiza hiyo siku sijui nisemeje.

Kukodi jenereta bei inapatikana kwa aina ya jenereta anachukua kubwa au dogo na linaenda kufanya kazi kwa muda gani ila bei yake kwa dogo ni 30,000 na kubwa ni 50,000 muda ni 12hours.

7. UNA KIWANJA KIPO TU
Unaogopa nini kutangaza kuwa unakodisha eneo la mtu kufuga, au kufanya chochote akipendacho kwenye kiwanja chako kisha ukampa kodi yako kwa mwezi? Huna mpango wa kujenga leo wala kesho ila una likiwanja limekaa huko lipo tu linaoteana majani (ndugu yangu ile ni pesa umeikalia) huwezi itumia wape wengine watumie kisha atakulipa.

Unaona faida gani kusema nina kiwanja changu mahali ila kipo tu hukifanyii kitu? Huo ni uchoyo wa kusaidia wengine na Roho ya kimaskini iliyo ndani yako wape watu wafanye kazi na wewe upate hela (sikulazimishi) ila hii nayo ni fursa, usisubiri kudhani wapangishaji ni wenye nyumba tu utakuwa upo ulimwengu wa Analog.

Siku hizi kuna wababa wenye vibanda, baba wenye viwanja, mama mwenye vyombo, dada mwenye ma dryer, nk nk yaani fursa juu ya fursa ila ni lazima uwe na roho ya kutoa na kusaidia wengine nawe ndipo utafanikiwa kupitia wao.

Biashara ni nyingi sana wakati mwingine huna haja ya kufanya wewe biashara ukijiona huwezi biashara sio mbaya ukawasaidia wengine kisha na wewe ukajipatia kitu kupitia kuwasaidia huko maana mwisho wa siku na wewe unahitaji pesa.

Hizi biashara hazina gharama ukinunua hivyo vifaa gharama ya kuvitunza ni wewe mwenyewe tu, yule anayekutafuta lazima anakujua na yule ndio atakuwa jicho lako huko kifaa chako kinapoenda na kwa hivi vifaa kama makabati, mabanda nk ni vitu unavyoweza vizungukia hata wewe mwenyewe kuona usalama wake upo vipi.

Una pesa unataka kufanya biashara na huoni biashara ya kufanya, Fungua jicho lako angalia pembeni yako utamuona machinga katandaza vitu chini mfuate muulize nataka kukununulia meza uweke vitu juu kwa siku unipe 1000 au 500 upo tayari? akikubali kamtengenezee.

Ukimalizana naye angalia upande huu utamkuta mama ntilie anauza sana ana wateja sana ila wateja wake wanakalia viti vibovu, mfuate mwambie unataka mnunulia viti then atakulipa 2000 per day kwa viti na meza zako, akikubali kamfuatie vitu.

Inawezekana kama ukiamua kuwaza tofauti na wengine, sio lazima wote tuwe wakulima hebu mimi na wewe tuhakikishe yule mkulima analima vizuri tumpelekee maji ya kunywa, leso ajifute jasho, ajisikie anajaliwa halafu tuone kama akivuna atakuacha bure na tuone kama maisha hayatoenda, shida yetu binadamu tuliozaliwa na mwanamke tuna roho za UMIMI tukizikemea na kuzikataa hizi roho tutafanikiwa sana.
Aseee unaakili umewaza mbali sana
Ila mimi natamani kufanya biashara tatizo naogopa kutapeliwa au kufilisika hata hivi nakabiashara ka handbags lkn kananinyima usingizi
Nadhani nahitaji mwongozo kidogo
 
Yes mkuu, kila mtu atachomoka na chake kimoja kidogo kidogo tu kisha

baadae atajikuta vyote ktk list anavifanya,muhimu "tuwe tofauti ktk utafutaji"

Dah Mkuu hivo vibanda natengeneza mwenyewe na gharama za ufundi ni hizo hizo ngoja hali ya hewa ikitulia ntafata idea zako


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kila mtu anawaza pesa, kila mtu kichwa chake ina picha ya mafanikio na asilimi 90% ya hawa watu wote wanaowaza pesa na mafanikio na maisha mazuri hufikiri pesa inapatikana kwa kufanya biashara tu, labda auze kitu fulani ndipo apate pesa.

Kuna njia nyingi za kupata pesa kwa wewe ulie na mtaji, hapo ulipo unaweza ukawa na pesa yako ila hujui uifanyie biashara gani au labda muda wa kusimamia hiyo biashara kwako ukawa mdogo hivyo unaogopa na hujui cha kufanya.

Sasa sikia leo nitakupa list ya vitu vya kufanya ujitoe na stress. Kuna watu najua hata tuongee na maturumbeta tupige ila hampo tayari kuacha kazi mnazofanya mjiajiri ila mpo tayari kuanzisha biashra ikafa, mkafungua ingine ikafa mkafungua tena na tena hamchoki ila sio eti mjiajiri najua mpo.

Sasa najua kuna watu mmeshajaribu kufungua biashara nyingi sana na mwsho kwasababu ya usimamizi biashara zote zimekufa, mmechoka na mmekata tamaa hamjui mfanye nini, hamna shida soma nitakavyoviandika leo kisha chomoka na kimoja kakifanyie kazi.

Leo naongelea biashara ya KUKODISHA VITU

Najua unaweza jiuliza utakodisha nini na kinauzwaje na kinakodishwaje,mimi leo ntawapa mfano ya ninavyovijua tu na ambavyo nina uhakika navyo, hivyo kama na wewe utapata idea usiache itoa yako ili namimi niipate nione nafanyaje.

1. VIBANDA VYA TIGO PESA
Nadhani wewe ni shahidi ya Mawakala wangapi unawakuta na miamvuli huko barabarani, nataka kukwambia kitu hao Mawakala sio kwamba wanapenda kukaa na miamvuli na meza tu ila sababu ni kwamba hana pesa ya kutengeneza kibanda,chakufanya wewe tengeneza kibanda kidogo cha wakala wa Tigo Pesa ambacho gharama yake kuanzia mabati, bomba mpaka kinakamilika ni 250,000 kwa kibanda kimoja, ina maana kama una Milioni 1 una uwezo wa kutengeneza vibanda vinne vilivyokamilika imebaki mtu kuchukua kwenda kufanyia kazi.

Kodi ya kukodisha hivi vibanda kimoja kwa mwezi ni 20,000 ina maana kwa vibanda vyako vinne una uhakika wa 80,000 kila mwezi hiyo ni uhakika yaani, sio ya kutafuta au kupigizana kelele na mtu na uchukuaji kodi wa hivi vibanda ni wa mwezi mtu akupe kodi ya mwezi tu kisha apige zake kazi.

2. BANDA LA BIASHARA
Hili banda halina utofauti na hilo banda la tigo pesa hapo juu tofauti yake ni ukubwa, kutegemea na uwezo wako ila kwa banda la ukubwa waupana futi 5 na urefu kwa futi 10 gharama ya ujenzi wa hili banda ni 500,000 hivyo ukiwa zako na 1M utaweza tengeneza mabanda mawili ambayo utayakodisha kwa wanaotaka yakodi bei yake kwa mwezi 30,000 to 50,000 kodi itategemea na wapi unaenda kumuwekea hilo banda, ukienda liweka sehemu nzuri kodi utaweza kumpa hata 60k to 100k na akalipa bila shida maana eneo hilo frem kodi ni 300k kwenda mbele. Assume una mabanda yako mawili ya kodi 50k kwa mwezi utakua unaingiza 100,000 isiyo na maelezo.

3. MASHINE YA KUCHOMELEA
Hizi mashine zipo za aina mbili kuna zile portable za kubeba halafu kuna yale transforma lake limesukwa na nyaya za aluminum, bei ya kuyanunua haya

- Portable: 400,000
- Kusuka: 300,000

Kukodisha haya ma mashine ni kwa masaaa 6 na masaa 12, kuna bei ya 6hrs na bei ya 12 hours, bei yake kwa 6hrs 20,000 na 12hours ni 30,000, ila kwa mashine portable 6hrs ni 30,000 na 12hrs 40,000.

Calculate hapo uone kwa siku utakuwa unaingiza sh ngapi, hii biashara ukijuana na mafundi welding kazi zitakuwa kila siku 5000 elfu kumi vitakuwa havikauki kwenye wallet/ pochi yako kiufupi huwezi kuwa na shida ndogondogo.

4. MUZIKI SPEAKER ZILE ZA KUCHOMEKA FLASH
Hizi speaker nilijaribu kununua kwa ajili ya ki pub changu uchwara fulani hivi sikuwaza kama hizi speaker ni dili basi wateja wale wale wakawa wakija wakisikia muziki wake wananiuliza kama nakodisha nikaanzaga zikodisha kama utani kwnye visherehe vya birthday huko mitaani, bei ni 50,000 kwa event 1 kiukweli hamnaga weekend hizi speaker nakosa simu ya kuombwa watu wakizitaka maana watu n wana sherehe kila leo na miziki yao ya subwoofer haitoshelezi haja zao.

Zitafute hizi speaker zinunue usiogope hela yako itarudi bila wasi wasi, zipo size tofauti ila kwakuwa unataka ya kibiashara nunua ya 600k to 700k hapo utapata heavy weight mziki kwa shughuli za mitaani, mfano ni kama hii Ailipu hapa chini japo kampuni zipo kibao zinazotengeneza hii mispika ya hivi.


5. KABATI ZA ALUMINIUM
Umeshaenda kununua chips mahali? Umeshaona chipsi zinawekwa kwenye nini? Basi tengeneza yale makabati nakuhakikishia hamna kikwazo kikubwa kwenye biashara ya chipsi kama KABATI Zero IQ ni shahidi muulizeni awambie mtu ataweza jidunduliza anunue kila kitu ila mtihani ukaja kwenye kabati.

Sasa tengeneza makabati yako ya 200,000 tengeneza makabati manne kisha yaweke mahali andika yanakodishwa, humalizi masaa 24 tayari ushapata mteja, haya makabati bei yake kabati per day ni 2000 maana yake kabati 1 kwa mwezi litakupa 60,000 x 4 = 240,000

Unaweza amua tengeneza vikabati vidogo kwa ajili ya mtu kuweka kachumbari na vitu vidogo vidogo ambavyo bei ya kabati kutengeneza ni 150,000 kisha wewe utalikodisha kwa 1000 per day x 30 days = 30,000 x 4(idadi ya makabati) = 120,000 kwa mwezi jumlisha bei ya makabati yako yote uone utakua na kiasi gani.

6. JENERETA
Kwa Tanzania yetu hii ndugu zanguni hii ni biashara nzuri sana, sijui kama utanielewa ila hii ni biashara ambayo ataekufata/ kukupigia simu unamtajia bei huku unakula karanga zako na hawezi kataaa wateja wapo kibao tena wengi tu, vuta picha watu wamekuja kwako kukodisha zile spika plus jenereta yani hela utayoingiza hiyo siku sijui nisemeje.

Kukodi jenereta bei inapatikana kwa aina ya jenereta anachukua kubwa au dogo na linaenda kufanya kazi kwa muda gani ila bei yake kwa dogo ni 30,000 na kubwa ni 50,000 muda ni 12hours.

7. UNA KIWANJA KIPO TU
Unaogopa nini kutangaza kuwa unakodisha eneo la mtu kufuga, au kufanya chochote akipendacho kwenye kiwanja chako kisha ukampa kodi yako kwa mwezi? Huna mpango wa kujenga leo wala kesho ila una likiwanja limekaa huko lipo tu linaoteana majani (ndugu yangu ile ni pesa umeikalia) huwezi itumia wape wengine watumie kisha atakulipa.

Unaona faida gani kusema nina kiwanja changu mahali ila kipo tu hukifanyii kitu? Huo ni uchoyo wa kusaidia wengine na Roho ya kimaskini iliyo ndani yako wape watu wafanye kazi na wewe upate hela (sikulazimishi) ila hii nayo ni fursa, usisubiri kudhani wapangishaji ni wenye nyumba tu utakuwa upo ulimwengu wa Analog.

Siku hizi kuna wababa wenye vibanda, baba wenye viwanja, mama mwenye vyombo, dada mwenye ma dryer, nk nk yaani fursa juu ya fursa ila ni lazima uwe na roho ya kutoa na kusaidia wengine nawe ndipo utafanikiwa kupitia wao.

Biashara ni nyingi sana wakati mwingine huna haja ya kufanya wewe biashara ukijiona huwezi biashara sio mbaya ukawasaidia wengine kisha na wewe ukajipatia kitu kupitia kuwasaidia huko maana mwisho wa siku na wewe unahitaji pesa.

Hizi biashara hazina gharama ukinunua hivyo vifaa gharama ya kuvitunza ni wewe mwenyewe tu, yule anayekutafuta lazima anakujua na yule ndio atakuwa jicho lako huko kifaa chako kinapoenda na kwa hivi vifaa kama makabati, mabanda nk ni vitu unavyoweza vizungukia hata wewe mwenyewe kuona usalama wake upo vipi.

Una pesa unataka kufanya biashara na huoni biashara ya kufanya, Fungua jicho lako angalia pembeni yako utamuona machinga katandaza vitu chini mfuate muulize nataka kukununulia meza uweke vitu juu kwa siku unipe 1000 au 500 upo tayari? akikubali kamtengenezee.

Ukimalizana naye angalia upande huu utamkuta mama ntilie anauza sana ana wateja sana ila wateja wake wanakalia viti vibovu, mfuate mwambie unataka mnunulia viti then atakulipa 2000 per day kwa viti na meza zako, akikubali kamfuatie vitu.

Inawezekana kama ukiamua kuwaza tofauti na wengine, sio lazima wote tuwe wakulima hebu mimi na wewe tuhakikishe yule mkulima analima vizuri tumpelekee maji ya kunywa, leso ajifute jasho, ajisikie anajaliwa halafu tuone kama akivuna atakuacha bure na tuone kama maisha hayatoenda, shida yetu binadamu tuliozaliwa na mwanamke tuna roho za UMIMI tukizikemea na kuzikataa hizi roho tutafanikiwa sana.
Thanks so much for those ideas.
Kwa sisi tuliokua tunawaza vya mamilion kumbe vipo vidogo vya kukupa pesa daily Tena bila Kodi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nilianza kwa uzuri kabisa. Mleta mada ndio kaanza dharau. Fuatilia mada tokea mwanzo utaona. Hakuna mtu anapenda mafanikio ya wengine kama mimi. Shida watu wanapenda kuambiwa maneno matamu tu. Mfano, kuambiwa utafanikiwa kwa kutumia akili kidogo sana. Kwenye biashara hakuna kutumia akili kidogo. Kama ingekuwa rahisi, kungekuwa na Reginald Mengi kibao Tz.

Mimi sijakuzuia, nilishasema uko huru kufuata maelezo ya mtoaji mada. Naomba tafadhali maneno yangu yote usiyazingatie kabisa. Ni dunia huru.

Lengo langu lilikuwa jema kabisa nilitaka kujenga mada vizuri zaidi ili iweze kusaidia watu kwa undani zaidi. Kwa kuwapatia watu njia za kufanikiwa wakishaanza biashara na kumudu vikwazo. Watu wajifunze kuchukua critics vizuri. Ila mtoa mada akaanza kinishambulia tu wakati mimi malengo yangu yalikuwa mazuri. Na ndio ikawa ugomvi ambao binafsi siupendi kabisa.
Mawazo yako yalikuwa mazuri kuijenga mada kwa upande mwingine, biashara yoyote ina pande mbili ambazo zinatakiwa kuzingatiwa kabla haijaanzishwa (ulikuwa sawa) ila approach pengine haikuwa nzuri sana ndio maana mtoa mada aka react negative.
 
Shukurani sana na ubarikiwe sana kwa kuwa na moyo mkunjufu wa kushare na wengine fikra chanya juu ya biashara kwahilo tunakushuru
 
Kiukweli katika kujifunza mambo ya biashara kwa vitendo na research za mtaani nimegundua kwamba watu wengi huwa tunafeli kwa kuwaza mavitu makubwa(projects kubwa) na kuzidharau projects ndogo ambazo ukizipatia ziko very consistent.
Wakati kumbe kuna viprojects vidogo vidogo ukiwa navyo vitatu unaishi mjini.

Kwa mfano maeneo ya nyumbani dar kuna vijana fulani wameungana wakaanzisha project ya kutengeneza maandazi na chapati jioni maeneo karibu na stendi.
Wanapika machapati/maandazi makubwa moja linauzwa kwa shilingi 500.

Basi wanauza sana,wako vijana wanne na wako bize muda wote yaani ni kama kiwanda lakini wamekodi eneo tu wakapanga meza zao wala hakuna cha fremu wala nini.
Sasa hapo mahali kuna kijiwe cha bodaboda wananunua sana wakichukua michapati miwili ndio kama dinner yao ndio imetoka hiyo.

Na projects ya aina hii nimeiona sehemu mbili tofauti maeneo ya nyumbani ni vijana wa kichaga na kihaya kundi lingine.
Ndio maana mtoa mada nimemuelewa vizuri sana.
 
Ninachokiona hapa haya yote yapo hata huyu anaebisha asionekane kama chama cha upinzani tu mkumbuke kuna Jambo alilowakumbusha na ni kubwa pia mfano mtu angeenda kununua pikipiki na kumpa MTU anayedhani ataleta hela, pasipo tahadhari matokeo Jamaa siku akijikwaruza kweny mishe za kawaida anaeenda uiuza pikipiki anakuja na kusema wamenikaba na kunipora! Hi mpingaji anakukumbusha ufanye kitu kuzuia Hilo labda kufunga ma GPS na kila unaloona linaweza saidia kuhakikisha unakuwa salamander kweny biashara na mbaya kwakuwa utakuwa ndo umeianzisha

Ola muanzisha maada unajua kutupanga madini kina language hapa nitakafanyia KAZI
 
Umesema mafanikio kwa kutumia akili kidogo! Vipi ulimwengu wa roho hata kama hujaenda shule pesa unabeba kwa kapu??
 
Kuna sehemu huwa napita asubuhi naona kina mama wauza mboga wa kutosha wanaweza kuwa hata 300 ,na huwa wanskaa pale Kama masaa 2 wanaondoka...huwa narafakari Hawa niwape huduma gani,na Mimi nipate riziki ,sijapata jibu Hadi Sasa!
Misaada please!
 
Back
Top Bottom