Hivi umewahi kuhisi kuna upendeleo wa baadhi ya watoto kwenye familia yenu?

Nimeona nami nichangie kitu hapa
Mimi ni first born kwenye familia yetu yenye watoto wa tatu na kitu cha kipekee mimi ndio mtoto pekee wa kiume
Wadogo zangu wamekuwa na-jelaous na mimi ni kutokana na mama kunipenda zaid ya wao hii inatokana na kuwa tukipitia through a lot kwenye makuzi yangu
Tulinusurika kifo wakati nilipo zaliwa tulipata ajari ya gar na mama wakati tukitoka sehemu nilipo zaliwa tukielekea nyumban
Pili life halikuwa zuri wakati ninakuwa so ilinibidi ni msaidie bi mkubwa kwenye shughuli zake za mama lishe
Ila kwa hawa madogo now wanaishi kwenye comfort zone na kitabia wakotofauti sana na mimi kidogo huyo wa mwisho
Kitabia mimi ni mpole sio mgomvi na wala sijawahi kumbishia bi mkubwa, kwa now inafika kipindi nikiwa narud home kwa likizo utasikia madogo wanasema mtoto wa mwisho huyo karud
Hayo ndo machache kwa ufupi
 
Tunawapenda watoto wote ila ni ngumu kumpenda mmoja zaidi ya wengine ambaye hata wengine wanajua wakihitaji kitu fulani kutoka kwa mzazi anayempenda wanamtumia kama chambo ili kufanikiwa.

Watoto wa mwisho wanapendwa na wazazi wote na nguvu zote za ulezi wa kudekeza huelekezwa kwake.

Kama watoto wote ni wa kike au wote ni wa kiume Mtoto anayependwa na mama hawezi pendwa na baba hali kadharika kwa mama pia. Na hilo halikwepi.

Na kama ni mchanganyiko basi Mtoto wa kike anaegemea kwa baba na wanatengeneza bond ya kudumu mpaka mama anaweza ona wivu vivyo hivyo Mtoto wa kiume huegemea kwa mama na kuwa Mtoto wa mama.

Lakini jambo ambalo hatulijui ni kuwa upendo wetu mkubwa kwa watoto ndio hugeuka kuwa chuki na uhasama baina yetu.

Fikiria baba mwenye mtoto wa kiume ambaye anampenda mnoo na anataka afanikiwe katika maisha yake kama kiongozi wa familia ajaye. Hawezi kumuacha awe mzembmzembe na asiyetegemeka. Atata ahakikishe anakuwa mwanaume kweli atakayelinda familia yake kiuchumi, kifkra, nguvu na mengineyo. Tegemea mtoto huyo akifanya uzembe tu kwa upendo wa baba atakula fimbo au adhabu nyingine. Lakini wakati huohuo mama atambembeleza na kumpakulia tuwali kidogo jikoni na tumchuzi twa nyama. Automatically mtoto ataona baba hampendi na mama ndio anampenda. Na ndio haya matoto ya mama yaliyopo siku hizi.


Lakini pia mama kwa upendo anataka binti yake akue na kuwa mwanamke bora . Mama hatataka mzaha. Akifanya makosa au uzembe katika maswala ya nyumbani na jikoni basi atakula sana ubapa wa mwiko na kurushiwa masufuria. Akikimbilia sebuleni anapokewa na baba na kukumbatiwa. Na ikiwezekana anafoka kwa mama apunguze adhabu anasahau ya kwake na mtoto wa kiume. Ona bond inavyotengenezwa hapa na nyingine kubomolewa. Na ndio maana watoto wa kike huwaambii kitu kuhusu baba zao labda awe mwehu.


Upendo ndio umetengeneza matabaka ya upendo katika familia na si chuki. Na siku zote wapokeaji wa adhabu hawaamini kama wanapendwa kwa kupewa adhabu ni mpaka wakikua ndio hutambua kuwa wazazi waliwajenga ama kuwaharibu katika malezi.

Mimi tumekubaliana na mwenzangu nikiwa natoa adhabu kwa mtoto au yeye ndio anatoa basi tukielewa tatizo tuunge mkono na hakuna kubembeleza mmojawapo ili wajue wote wawili hatujafurahishwa na alichofanya. Lakini upendeleo hauwezi kuisha kabisa.
 
Mimi nimezaliwa wa kwanza nilipendelewa/nilidekezwa sana nikiwa mdogo lakin ikafika hatua sikupendelewa tena na upendo ukapunguzwa kabisa na nikawa mimi ndo mtoto wa kufanya kazi ngum za nyumbani, kuchimba shimo la takataka, yanaweza yakaletwa matofali/mchanga mzee akaniambia mimi ndo nihamishe kutoka sehem moja kusogeza sehem fulan na wala haina sababu ya kuyasogeza ila ni bas tu Ni vile aliamua niwe na kula kwa jasho nikiwa hapohapo nyumban had nikahisi nachukiwa kumbee laa mzee aliamua kunikomaza kiume makusudi tu maana dunia siyo nyepesinyepesi.

Mtoto ambae hajadekezwa huwa inamjenga sana kuwa mpambanaji na hata akiwa na biashara au kupata kaz n lazma aheshim alicho nacho, ila walio dekezwa anaweza akaacha kaz kisa amefokewa tu na kusahau malengo yake kwa kukatishwa tamaa na vikwazo vidogo maana uvumilivu unakuaga 0
 
Niwie radhi kwa kauli zangu ikiwa ni hivyo na bila shaka sijakukwaza Rafiki.

Mungu muumba mbingu na nchi amtunze na kumlinda binti, akue katika njia bora. Na yeye ajekua na upendo wa dhati kwa watoto wake atakaojaliwa...aendelee kuwa furaha katika maisha yenu.
Wala hujanikwaza rafiki.
Amen. Napokea baraka kwa niaba yake.
 
Amen, T.G.I.F, wale wenzangu na Mimi wapenda weekend tunaijua ile feeling ya Ijumaa,

Natumaini mpo salama, nimejikuta najiuliza hichi kitu maana ni situation ambayo nimekutana nayo sana kwa watu wengi, kuna ile namna unahisi kabisa kwamba kwenye familia yetu yenye watoto kadhaa, kuna kipenzi cha Baba na pia kuna kipenzi cha Mama, na kuna wale wanabaki wanajua kabisa Mimi siye miongoni mwao..!

Nilikuwa nazungumza na mtu wangu wa karibu siku moja, akanitamkia like 'I was not their best'...! yaani hapo si kwa Baba wala Mama, nilijiskia vibaya mno mno, na hakika ukitazama watoto waliokosa upendo wa hivyo kwa kushuhudia kabisa kuwa wenzie wanakirimiwa kuwaliko kuna namna hawako sawa kabisa kabisa tofauti na yule mtoto aliyepokea upendo wa kumtosha na kumjaziliza..!

Bado sijakuwa mzazi I don't even know how it feels, hivyo natamani nijue, unapenda watoto wote ni kweli lakini kuna yule ambaye anagusa kabisa mtima wako moja kwa moja (nimeongea na wazazi wengi na wamekiri hili), hivi hakuna namna unaweza ficha hili wenzie wasijue na wakajiskia vibaya.?

Ama umewahi pitia ile hali katika ukuaji wako ya kujua wewe ndiye unapendelewa zaidi ama ni kinyume na hapo kuliko wenzio, na ulijiskiaje.??

Natamani wajuzi wa malezi na wazazi waliweke hili sawa ili tujifunze, maana kuna kizazi chenye watu wenye tabia za ajabu sana kinazidi kutengenezwa hivi sasa na hakuna anayewaza kuhusu hili kabisa..! Kuna watu unaweza walaumu kwa tabia wanazokuonyesha ukaishia kuwalaumu na kuwachukia kumbe ni MALEZI yao tu maskiini ndiyo yamewafikisha walipo..!!

Anyways Karibuni..!
Upendo wa mzazi kwa watoto hauwez kuwa sawa hii hata nyumban nimeiona mama alikuwa anampenda sanaa kaka yangu ninaemfata kw akuzaliwa kuliko watoto wengine sababu sijui ninn maana huyo braza alikuwa mtukutu sanaaa ila baba alikuwa ananipenda sanaa mm sababu naamin nikiwa mm nilikuwa mtoto mtulivu sanaa sio mzururaji nina heshima napia nilikuwa nabidii katka masomo kuliko watoto wote
 
well
Yes it happens; you love all your kids, but you like one the most

1. Single parenting; kuna wale wazazi ambao walijikuta wanalea mtoto peke yao kwa sababu moja au nyingine; automatically mapenzi yao yanakuwa makubwa sana na huyo mtoto kuliko watoto wengine atakaowalea na mwenzie. Mtoto anaumwa, anaumia, kila function upo wewe tu; maisha yenu revolve around each other; automatically upendo utaegemea sana kwao. Ingawa kuna wengine ile chuki juu ya mzazi mwenzie aliyemuacha labda, na uchungu wa kumlea mtoto peke yake; anahamishia uchungu wote kwa mtoto, aisee mtoto atateseka hadi ajiulize kama huyu ni mzazi wangu kweli.

2. Mazingira ya kutungwa mimba, kuilea hadi kujifungua na malezi kwa ujumla. Mzazi/Couple ambayo imehangaika sana kutafuta mtoto afu ikaja kufanikiwa kumpata mtoto baada ya struggles nyingi; upendo kwa huyo mtoto wa kwanza utakuwa ni mkubwa zaidi.

-Kuna wale unakuta wakati mama ana mimba labda ikawa inamsumbua sana, kakaa bed rest, sijui kajifungua ikabidi wabaki months hospitalini na mtoto; hako katoto kanatokea kupendwa zaidi ya wenzie

-Mtoto mgonjwa au anayehitaji special need, anachukua nafasi na muda wa wenzie zaidi. Ndiyo maana kuna baadhi ya wazazi/familia, wanaamuaga kutoongeza watoto wengine ili wampe attention yote yule mwenye special need.

3. Kuna watoto ambao wanapendeka kirahisi zaidi. Mtoto mwingine akishakusalimia amemaliza, huyo anaenda kucheza; wakati mtoto mwingine akishakuona tu kashakukimbilia, mara kakuletea hiki na kile, mara kakufanyia hivi, mara kaja kukaa mkapiga story; yaani anakuonyesha upendo hadi basi. Mtoto wa hivi automatically atakuwa anapendwa zaidi na wenzie. Kuna ka-niece kangu kenyewe hakana habari na mtu yoyite zaidi ya kaka yake; hata akilia haiti mama au baba, anaita tu kaka

4. Mtoto anaye-share/serve interest za mzazi;mzazi anajikuta anampenda mtoto huyo zaidi. Mfano kuna watoto wazito na watoto wepesi wa kazi; kukiwa na kikazi tu huyo ashanyanyuka kusaidia. Mzazi anajikuta yupo karibu na huyo mwepesi zaidi. Labda mzazi anapenda kitu fulani na mtoto anakipenda pia, automatically hawa wawili wanaconnect zadi

5. Last borns wengi wanapendwa zaidi.

6. Mtoto ambaye ni wa jinsia ya pekee kwenye familia yao; mara nyingi anakuwa kipenzi cha wazazi hata na wenzie. Mfano ukute familia ambayo mtoto wa kike ni mmoja tu; huyo anakuwa kipenzi zaidi na roho ya baba yake; wa kiume wa pekee ni pumzi ya mama yake.

7. Watoto wanaopewa majina ya kurithi ya bibi/babu/kipenzi cha mzazi. Ule upendo alionao mzazi kwa yule mwenye jina, huwa unahamishiwa kwa mtoto aliyerithi jina hilo.

N:B Ingawa kupendelea mtoto ni kama kitu kisichozuilika; inabidi wazazi tuwe makini sana. Huwa inaleta chuki na madaraja kwa watoto as wale wengine wanaona kama wenyewe hawapendwi; au wengine wanajikuta wana inferiority complex; anajihisi si bora kuliko yule anayependwa zaidi. Ingawa wazazi huwa tunajitetea sana like "sio kweli, tunawapenda wote sawa".

Changamoto niliyoi-notice haswa kwa baadhi ya wamama; ni pale ambapo favorite child wa baba anakuwa si mtoto wa mama wa kumzaa (mtoto wa nje wa mume). Huo moto utakaochochewa kati ya watoto wa nje na wa ndani mmh. Au huyo mtoto akiwa ndiyo mtoto pekee wa baba; hali ndiyo inakuwa tete zaidi . Mungu anatuona

Sent using Jamii Forums mobile app
well said mkuu
 
Ka-ugonjwa ka upendeleo Namge..??
yeah kuna mtoto mmoja kati yetu..mzee anampenda mpka ameshindwa kuficha..huwa anasema waziwazi kbsaaa..
Afu ndo kivuruge hatari..bhasi huwa tunacheka tu..tunaagiza bia tunakunywa siku zinaenda.
 
Leo niende personal maana mada imenigusa

Kuna kuona mtu flani anapendwa kitu ambacho kwangu ni kawaida ila kuna kubaguliwa

mzazi kukuchukulia kama of low class, yaani ndugu yako yoyote anaona anakumudu maana mkienda kwa mzazi ni nadra kuwa balanced na kukaa upande wako hata kama unaonewa

yaani nilibaguliwa na kuoneshwa LIVE, imagine mpo sebuleni ndugu zako wanaomba hela ya nguo wanapewa bila shaka ila wewe unaomba hela ya masomo ya ziada school tena cheaper mara hata 100 lakini unanyimwa kwa kejeli na ndugu zako wanakucheka

ilikuwa worse than that !!

Ila imenijenga kuwa mtu wa kutopenda misaada kirahisi au vitu vya bure. I fight on my own, kheri nipate buku nisonge ugali nile kuliko kumuomba mtu 100k ambayo anaweza kunipa

Kingine nampenda first born wetu, Alinionesha kunipenda sana na alikuwa karibu kuniprotect. ile Ukinigusa ujiandae kupambana nae na 90% ya kupigana kwake home sababu ni mimi 😂😂😂, Japo ni kivuruge hatari ila kama kuna mtu dunia hii najua ananipenda without a doubt bhasi ni yeye and i love him sana sana sanaaaa

nimeshakuwa emotional ngoja niishie haps 😁
Hahaa hakuna feeling tamu kama kujua you are loved! That is awesome. Mimi mama ananipenda ila Sasa changamoto siwezi kurudisha that same love. Niliondoka home nikiwa 14 years kule nilikoenda aliyenilea akanionesha upendo. Nimejikuta nimeuhamisha wote yani. Nimejitahidi kuurudisha ila wapi. Mpaka mama anajua nampenda mlezi kumzidi. Sometimes naumia ila kuna vitu vipo out of our control.
 
Kuna kutokupendwa na kubaguliwa hayo yote nimeyapitia.. sikuwa napendwa na nilibaguliwa hali ilipelekea nikakosa hata elimu kwani mimi na dada yangu tulimaliza shule ya msingi pamoja na tukafeli wote . Yeye akapelekwa shule ya kulipia mie nikaachwa nyumbani na sikuwahi kuuliza maana nilijua niko fungu gani. Yaani si kwa baba yangu wala kwa mama yangu.

Cha ajabu walianza kuonyesha upendo naweza sema ni wakinafki mara baada ya kusikia nafanya kazi. Walikuwa hawajali wala hawakuniuliza nafanya nn waliona tu natoka na kurudi basi wakasikia kwa watu kuwa nina kazi na walizidisha kuonyesha upendo nilipowaambia kuna mtu analeta barua na nikaolewa. Na mimi sasahivi ninikukumbuka yale mambo siwatafuti hata miezi sita .. nikikumbuka ni wazazi wangu napiga kiwasalimia tena tupo mji mmoja nauli hazidi 3000 kwenda na kurudi hata watoto wangu sijawahi wapelekea nikienda ni mimi tu na mtoto wa kwanza yupo darasa la kwanza na wao hawaniulizi pia... aiisseee nna mengi.. najisikia vibaya nikikumbuka.. ila wanangu nawapenda sawaaa kabisaaaa
 
Kuna kutokupendwa na kubaguliwa hayo yote nimeyapitia.. sikuwa napendwa na nilibaguliwa hali ilipelekea nikakosa hata elimu kwani mimi na dada yangu tulimaliza shule ya msingi pamoja na tukafeli wote . Yeye akapelekwa shule ya kulipia mie nikaachwa nyumbani na sikuwahi kuuliza maana nilijua niko fungu gani. Yaani si kwa baba yangu wala kwa mama yangu.

Cha ajabu walianza kuonyesha upendo naweza sema ni wakinafki mara baada ya kusikia nafanya kazi. Walikuwa hawajali wala hawakuniuliza nafanya nn waliona tu natoka na kurudi basi wakasikia kwa watu kuwa nina kazi na walizidisha kuonyesha upendo nilipowaambia kuna mtu analeta barua na nikaolewa. Na mimi sasahivi ninikukumbuka yale mambo siwatafuti hata miezi sita .. nikikumbuka ni wazazi wangu napiga kiwasalimia tena tupo mji mmoja nauli hazidi 3000 kwenda na kurudi hata watoto wangu sijawahi wapelekea nikienda ni mimi tu na mtoto wa kwanza yupo darasa la kwanza na wao hawaniulizi pia... aiisseee nna mengi.. najisikia vibaya nikikumbuka.. ila wanangu nawapenda sawaaa kabisaaaa
Pole sana dear,
Hii imeniuma jamani..!!
Mungu akutie nguvu, wasamehe na uachilie ili uishi tu kwa amani,
 
This is really bad...I was not their best either..LAKINI side effects zipo mpaka now.
vuta subira..bora mmoja asome vizuri primary school.. secondary asome kawaida na tution nzuri..afu mwingine secondary peleka private
 
Pole sana dear,
Hii imeniuma jamani..!!
Mungu akutie nguvu, wasamehe na uachilie ili uishi tu kwa amani,
Ahsante hii imenifunza na kunikomaza. Na nitawasuprise pale nitakapomaliza elimu ya juu miaka kadhaa mbele. Yani naomba wawe hai waone. Na bado mimi ndiye msaada mkubwa kwao.
 
Duu aise. We kama mimi aise. Mimi na sister tunayefatana wote tumezaa nje ya utaratibu, nimezakisha binti wa watu sister naye kazalishwa. Ila bi mkubwa mtoto wangu ameshaniambia hamtaki na asimuone kwake. Ila wa sister amemchukua na anahanhaika naye. In Short bi mkubwa ni mkoloni ila huyu sister wakati tunakua ndo alikuwa anathubutu kumtania, kumchezea muziki n.k. Hivi tunavyoongea life lake lipo ovyo ovyo.
Wa kwako haamini Kama ni wako kweli
 
upendo wa mzazi kwa mtoto huwaga hauji automatically Bali kuna sababu lakini Mara nyingi hujenga chuki kwa mtoto anayependwa zaidi mfano Mimi kwetu ni first born na tumezaliwa watatu ,mama yangu ananipenda Sana kuzidi wenzangu Ila ni kwa sababu kwenye malezi sikuwahigi kumsumbuaga kama walivokuwa wanamsumbua wadogo zangu kwa hiyo imesababisha mimi kuchukiwa na kuonekana nakuwa favoured sana.
 
Hahaa hakuna feeling tamu kama kujua you are loved! That is awesome. Mimi mama ananipenda ila Sasa changamoto siwezi kurudisha that same love. Niliondoka home nikiwa 14 years kule nilikoenda aliyenilea akanionesha upendo. Nimejikuta nimeuhamisha wote yani. Nimejitahidi kuurudisha ila wapi. Mpaka mama anajua nampenda mlezi kumzidi. Sometimes naumia ila kuna vitu vipo out of our control.

Upendo haulazimishwi lakini unaweza kujitahidi kubalance matendo yako. Mama yako pengine ana majuto ya kutokukaa na wewe muda mrefu Ila mawazo ya wewe kumpenda mtu aliyeliziba pengo lake lazma imfanye ajisikie vibaya na kumuumiza sana. Najua si rahisi lakini inawezekana kiasi mkuu ili umpunguzie maumivu maana mwisho wa siku na yeye anakupenda sana
 
Kuna kutokupendwa na kubaguliwa hayo yote nimeyapitia.. sikuwa napendwa na nilibaguliwa hali ilipelekea nikakosa hata elimu kwani mimi na dada yangu tulimaliza shule ya msingi pamoja na tukafeli wote . Yeye akapelekwa shule ya kulipia mie nikaachwa nyumbani na sikuwahi kuuliza maana nilijua niko fungu gani. Yaani si kwa baba yangu wala kwa mama yangu.

Cha ajabu walianza kuonyesha upendo naweza sema ni wakinafki mara baada ya kusikia nafanya kazi. Walikuwa hawajali wala hawakuniuliza nafanya nn waliona tu natoka na kurudi basi wakasikia kwa watu kuwa nina kazi na walizidisha kuonyesha upendo nilipowaambia kuna mtu analeta barua na nikaolewa. Na mimi sasahivi ninikukumbuka yale mambo siwatafuti hata miezi sita .. nikikumbuka ni wazazi wangu napiga kiwasalimia tena tupo mji mmoja nauli hazidi 3000 kwenda na kurudi hata watoto wangu sijawahi wapelekea nikienda ni mimi tu na mtoto wa kwanza yupo darasa la kwanza na wao hawaniulizi pia... aiisseee nna mengi.. najisikia vibaya nikikumbuka.. ila wanangu nawapenda sawaaa kabisaaaa
Pole mkuu lakini chuki uliyoibeba lazma ikuathiri kwa kiasi flani, kama itawezekana wekeza nuvu kwa wanao na uiachilie
 
Amen, T.G.I.F, wale wenzangu na Mimi wapenda weekend tunaijua ile feeling ya Ijumaa,

Natumaini mpo salama, nimejikuta najiuliza hichi kitu maana ni situation ambayo nimekutana nayo sana kwa watu wengi, kuna ile namna unahisi kabisa kwamba kwenye familia yetu yenye watoto kadhaa, kuna kipenzi cha Baba na pia kuna kipenzi cha Mama, na kuna wale wanabaki wanajua kabisa Mimi siye miongoni mwao..!

Nilikuwa nazungumza na mtu wangu wa karibu siku moja, akanitamkia like 'I was not their best'...! yaani hapo si kwa Baba wala Mama, nilijiskia vibaya mno mno, na hakika ukitazama watoto waliokosa upendo wa hivyo kwa kushuhudia kabisa kuwa wenzie wanakirimiwa kuwaliko kuna namna hawako sawa kabisa kabisa tofauti na yule mtoto aliyepokea upendo wa kumtosha na kumjaziliza..!

Bado sijakuwa mzazi I don't even know how it feels, hivyo natamani nijue, unapenda watoto wote ni kweli lakini kuna yule ambaye anagusa kabisa mtima wako moja kwa moja (nimeongea na wazazi wengi na wamekiri hili), hivi hakuna namna unaweza ficha hili wenzie wasijue na wakajiskia vibaya.?

Ama umewahi pitia ile hali katika ukuaji wako ya kujua wewe ndiye unapendelewa zaidi ama ni kinyume na hapo kuliko wenzio, na ulijiskiaje.??

Natamani wajuzi wa malezi na wazazi waliweke hili sawa ili tujifunze, maana kuna kizazi chenye watu wenye tabia za ajabu sana kinazidi kutengenezwa hivi sasa na hakuna anayewaza kuhusu hili kabisa..! Kuna watu unaweza walaumu kwa tabia wanazokuonyesha ukaishia kuwalaumu na kuwachukia kumbe ni MALEZI yao tu maskiini ndiyo yamewafikisha walipo..!!

Anyways Karibuni..!
Unakuta labda mtu ni rebel kwenye familia, wazazi kila wakitaka kumnyoosha yeye anakuwa anahisi hawampendi. Halafu kuna yule ambaye wanahisi anafuata njia sahihi so wanakuwa wanampongeza huyu rebel anajihisi kama anatengea.
Na the more rebelious kid unavyozidi jaribu kumnyoosha the more anavyokuchukia na kuzidi kiwa rebelious.
Mara nyingi kunakuwaga kuna shida sema unakuta mzazi haijui. Uwa mtoto kuwa rebelious anakuwa kama vile ana fight back anafanya yale anayojua kuwa hampendi makusudi tu kama kuwakomoa
 
Back
Top Bottom