Hivi ulitumia simu gani wakati unajiunga JF kwa mara ya kwanza?

Ligaba

JF-Expert Member
Oct 12, 2018
1,045
2,821
Habari zenu wakuu.

Leo nimekumbuka nyuma wakati najiunga na JF kwa mara ya kwanza. Kwa kweli technology inakimbia kwa speed kubwa sana. Nikikumbuka aina ya simu niliykuwa nafungulia threads za humu ndani na magumu yake naduwaa kidogo.

Kwa ufupi Mimi ID yangu ya kwanza JF niliifungua 2011 wakati ule nilikuwa mtumiaji sana wa Facebook na kule kuna page ya JF nililike na ikawa naona story za humu ndani, nilipo jaribu kuingia ndani nikawa naona member wa wakati huo nakumbuka Mzizi Mkavu, na maligends wengine waliokuwa katika pick.

Kinacho nichekesha Leo ni aina ya simu huo mwaka nilikuwa natumia simu fulani za Nokia X-01 kama sikosei wengine walikuwa wanaziita Asha. Nawaza kama simu hii nikipewa Leo nitumie KuGoogle itakuwaje?

Je, wenzangu mnazikumbuka simu zilizotuunga JF kwa mara ya kwanza? Nasikia kuna wakongwe zaidi hao hawakutumia simu badala yake walitumia PC ili kuingia JF.

Screenshot_20201130-150214_1606737899758.jpeg
 
Niliijua JF 2012 Ilikuwa natumia sumsung GF sijui ngapi ngapi. Kadogodogo ka touch ila kalikuwa kanatumia Java. Hata hivyo nilikuja kujiunga na Vodafone 2015.
 
niliijua jf mwaka 2015 nikajiungia kwenye simu ya mshikaj wangu ilikua huwawei hapo ikawa kuingia ni tizi maana mpk ni mtafute msela kitendo kilichopelekea ni sahau password

Mwaka 2017 ndo nilijiunga Rasmi kwenye Tecno F5 hapo bado ilikua kwenye piki now nina simu nyingne.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom