Hivi ulaya Trafiki huwa nao wanakaa barabarani kusimamisha magari?

Kwanza nchi nyingi za Ulaya polisi anawashughulikia wote, wenye magari na wengineo. Hawasimami barabarani ila wanakuwa kwenye magari yao maalum wanafanya patrol almost kila mtaa/barabara hadi vijijini.
Gari zao ziko fitted na system inaitwa ANPR yaani Automatic Number Plate Recognition. Humo kuna data za madereva na gari zote, gari yako ikipita system yao inasoma namba ya gari yako ndani ya sekunde inawapa jibu kama gari halina vibali au dereva hana leseni, anadaiwa au ana kosa lingine la jinai.
Mara nyingine huwa wanatega sehemu ambayo wanajua wahalifu wanapenda kutorokea. Hawakusimamishi bila kosa,aidha gari ina kasoro,wewe una kasoro au umeendesha vibaya.
Hii system sasa hivi polisi wetu wanaitumia kukamata wale wasiolipa faini, wangekuwa na magari ya kisasa ingekuwa ndani ya patrol car badala ya kukaa nayo kibandani.
Mdau Prondo hii kitu itawasaidia sana by the way niliiona hii pia unapoingia parking area ya Ubungo plaza number plate inakuwa recognised haraka sana, badala ya tochi lukuki waweke hii
 
trafiki wa huku wanajificha kabisa ili usimuone ufanye mambo yako akukamate
 
Sio nchi za ulaya tu hapa hapa Africa kusini huwezi kuta polisi wa trafiki barabarani kama huku kwetu.Jijini Joburg na karibu na uwanja wa Oliver Tambo kila mahali kuna sensors ukifanya kosa sensors zinakuona na namba ya gari imejirekodi utakutanana risiti yako huko mbele.Kule kuna line hata kuendesha gari speed ndogo ni kosa unachelewesha wenzako.Trafick utamkuta tu mahali ajali imetokea umeme kule haukatiki mara kwa mara kama huku.Ni suala la technologia tu hata wao walikuwa hawako hivo na sisi tutafika huko
Africa kusini mbali hivyo, hapo Nairobi tu tayari kuna cameras barabarani
 
Bora technology ije dar waondoke barabalani
Ikija hio mtalia....kila siku italetewa barua ya notification unaambiwa tu chagua kulipa fine au mahakamani. Watanzania hawapendi kufuata sheria wataumia sana! Hio system ni nzuri kwa mfuata sheria utaifurahia ila kwa wengu hapa Tz mtalia kwasababu mtakosa pa kukimbilia!
Zile buku 5 zinawasaidia kwasababu itakuja point system on your license kila kosa points zibaongezeka ikifika 12(UK) unapoteza leseni ila kwa bongo unachagua buku 5 au points, ila ikija system automatic hutakuwa na nafasi ya kutoa buku 5...makosa manne leseni inafungiwa mtaweza?
 
Mi naomba tu kuuliza kwa anayejua au aliefika huko ulaya, hivi huko nako mapolice /trafik huwa wanasimama kando kando ya barabara na kusimamisha magari, na kama ni hivo je nao wanakuwa na vitabu vya risiti vya faini.
Mi sijui hii tabia naiona kama ni kitu cha ajabu yaani trafiki hamna mbinu nyingine zaidi ya kukaa chini ya mti pembeni ya barabara.
Na je nashindwa kuelewa hizo pesa za rushwa ambazo ni nyingi zaidi ya hizo zinazoandikwa huwa wanakula na nani, maana ni nyingi sana, je huwa wanapeleka mgao kwa wakubwa wao au?
Halaf kwanini trafiki wengi wanaroho mbaya sana, je wanakuwa trained kuwa na roho mbaya au ndo walivozaliwa
Ulaya hamna kitu kama hicho. Haya mambo yako huku ushenzini tu.
 
* Yes wanasimama kando kando ya barabara kwenye maeneo yaliyo na msongamano mkubwa wa watu, kwa ajili ya patrol.

* Yes magari yanayokiuka taratibu na sheria za usalama wa barabarani husimamishwa, dereva huhojiwa,kuelekezwa au hata kupigwa faini...

* Vitabu vya risiti sidhani, ila unapewa ticket inayoonesha aina ya kosa na kiasi cha faini ya kulipia.

* Alisimia kubwa ya waendesha magari, hawazingatii sheria na taratibu. Mfano Dar, zebra haziheshimiwi kabisa. Mwenda kwa miguu anavuka kwenye zebra ati dereva anamtolea maneno makali mwenda kwa miguu, "utagongwa wewe" badala ya yeye kusimama watu wapite...

Cc: @nahondaw
 
Sio nchi za ulaya tu hapa hapa Africa kusini huwezi kuta polisi wa trafiki barabarani kama huku kwetu.Jijini Joburg na karibu na uwanja wa Oliver Tambo kila mahali kuna sensors ukifanya kosa sensors zinakuona na namba ya gari imejirekodi utakutanana risiti yako huko mbele.Kule kuna line hata kuendesha gari speed ndogo ni kosa unachelewesha wenzako.Trafick utamkuta tu mahali ajali imetokea umeme kule haukatiki mara kwa mara kama huku.Ni suala la technologia tu hata wao walikuwa hawako hivo na sisi tutafika huko
In shaa Allah, karibuni tu Tuko njiani. Tanzania ya viwanda itatupeleka pazuri tu.
 
Pambana na hari yako mambo mengine yatakusumbua bure akiri yako na kukupunguzia sikuzako za kuishi.
 
Kule Sweden hakuna trafiki barabarani hata kidogo. Lakini kila mwendesha chombo cha anafuata sharia. Ukivunja sharia za usalama barabarani unapelekewa faini yako ikiwa na picha na eneo ulilotenda kosa kwenye address yako au hata nyumbani.
 
Back
Top Bottom