Hivi ukali huu ni wa nini hasa? Inasikitisha sana!

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
1571650996427.png
Yaani kwa kama si mkosi basi ni balaaa.

Unakuta mtu anatoa ushauri tu, achilia mbali kukusoa lakini anayeshauriwa anavyokuwa mkali mpaka unashangaa. Sijui shida inakuwa ni nini. Na hii ipo kwa karibu vyama vyote. Viongozi, wanachama na Wadau wa vyama vya siasa husika; wakishauriwa bila kujali ubora, manufaa na msingi wa ushauri husika, wanawageuza watoa ushauri kama maadui badala ya kuwachukulia kama marafiki.

Yaani mtu anatoa ushauri tu (achilia mbali kukosoa) lakini utakavyokimbizwa huku ukipopolewa mawe; atatamani ni bora ungeweka mkono kwenye mzinga wa nyuki. Sijui shida hasa inakuwa ni nini?

Ukitaka kundi unalotaka kulishauri muende sawa (Isipokuwa wachache ambao wana utulivu wa akili), basi lisifu (Hata kama linafanya kitu cha hatari). Ukitaka mwende sawa zaidi, liahidi kwamba litaenda mbinguni na una uhakika huo;hapo sawa ila ukishauri tu bila kujali ubora wa unachoshauri, umekwisha. Yaani sijui tumekuwa watu wa namna gani.

Cha ajabu hao hao ambao wakishauriwa wanakuwa wakali kama pilipili,nao wanalaumu wenye mamlaka kwamba hawataki kushauriwa ;sasa unajiuliza kama wao wala hawana mamlaka makubwa kwa sasa ila hawasikii la kuambiwa je wakiwa na mamlaka makubwa itakuwaje?

Na hoja zinazotolewa huwa zinakuwa ni dhaifu mpaka unajiuliza ni nini hiki? Yaani inakuwa ni kama mtoto anaambiwa “hauwezi kusoma vizuri, ni vizuri kujifunza kusoma ABC kwa sababu itakusaidia kwenye XYZ”. Anayeshauriwa jibu lake ni “wewe umeniona mimi tu? Mbona huwaambii kina fulani? Mbona fulani pia hawezi kusoma ina maana yeye humuoni? N.k

Lakusikitisha zaidi, hao ndio wanategemewa waoneshe njia wengine. Ni muhimu kubadilika vinginevyo ni changamoto kubwa.

Kuna siasa fulani hivi zinazofanywa na baadhi ya vyama ambazo ni “siasa za aibu”. Tujisahihishe !
 
Hakuna anayependa kushauriwa jambo ambalo anaona yeye yupo sahihi na hakuna kabisa anayependa kukosolewa.
Leo nimepigwa block na shangazi fatma karume kule tweeter kisa tu kumshauri aache kuchukua habari za uongo, alafu ndio wa kwanza kujifanya ooh freedom of speech. Pumbaavu kabisa
 
Hakuna anayependa kushauriwa jambo ambalo anaona yeye yupo sahihi na hakuna kabisa anayependa kukosolewa.
Leo nimepigwa block na shangazi fatma karume kule tweeter kisa tu kumshauri aache kuchukua habari za uongo, alafu ndio wa kwanza kujifanya ooh freedom of speech. Pumbaavu kabisa

Yaani inabidi tuelewe kwamba kuna vitu vinauma na kukera lakini ni muhimu. Na moja ya vitu hivyo ni kukosolewa. Ila pia nashindwa kuelewa shida inatoka wapi maana kama tunakubaliana kwamba binadamu hatujakamilika na tunakosea, iweje tukubali principal hii kwa wengine ila inaponitokea mimi kwa mfano sikubali?

Halafu ushauri una shida gani kwa mfano?

Anyway, basi let say ushauri na kukosoana ni kitu kibaya na hakifai, kwa maana hiyo anayeshauriwa anapaswa kukapiliana na washauri maana hawamtakii mema; basi tusilaumu yeyote anaye behave the same. Iwe hiyo ndio principle tuliyoamua kuchagua na ifahamike hivyo.

Vinginevyo ni aibu ya watu wote na mwiso wake sijui itakuwa nini?
 
JPM anatakiwa akaze zaid
ya hapo, mtu amekuonyeshea chuki ya waz waz, tena anakuombea ufe alaf bado unamlea, huyo hata akipata chance ya kukupoteza anakupoteza, cha kufanya ni kumchinjilia mbali , na hakuna cha ushaur hapo mi unafki mtupu
 
Kuna siasa fulani hivi zinazofanywa na baadhi ya vyama ambazo ni “siasa za aibu”. Tujisahihishe
Ulimaanisha nini?
Matukio tunayoyaona yanafanywa na wanasiasa kila siku katika ubora wake au ubaya wake; ni matokeo ya tabia na utamaduni unaojengeka kwa muda mrefu. Ukiona matukio mabaya, ni matokeo ya utamaduni mbaya na kinyume chake.

kama tungekuwa na utaratibu wa kukubali kushauriana na kuheshimu ushauri, tungesahihishana lakini kwa kuwa kila mmoja anaamini yeye hakosei wanaokosea wenzake tu, hakuna ambaye anataka kushauriwa (isipokuwa watu wachache sana) achilia mbali kukosolewa au kujisahihisha. Hii ndio yangamoto ambayo mleta mada anajaribu kui address
 
JPM anatakiwa akaze zaid
ya hapo, mtu amekuonyeshea chuki ya waz waz, tena anakuombea ufe alaf bado unamlea, huyo hata akipata chance ya kukupoteza anakupoteza, cha kufanya ni kumchinjilia mbali , na hakuna cha ushaur hapo mi unafki mtupu
Na wewe hapa unachofanya ni kuchochea chuki isiyo na sababu yoyote.

Kabla hujafanya au kusema kitu chochote serious, Jiulize faida na hasara ya unachotaka kusema. Jiulize mnufaika ni nani na atanufaikaje, ukibaini kwamba hakuna mnufaika achana nacho.

Kauli kama hii unayotoa hapa mnufaika wake ni nani?
 
Hakuna anayependa kushauriwa jambo ambalo anaona yeye yupo sahihi na hakuna kabisa anayependa kukosolewa.
Leo nimepigwa block na shangazi fatma karume kule tweeter kisa tu kumshauri aache kuchukua habari za uongo, alafu ndio wa kwanza kujifanya ooh freedom of speech. Pumbaavu kabisa
mbulula tu wote hao, ni wachumia tumbo, mirija yao imeziba ndio maana unaona povu, wakati wajo vitengoni hukusikia hizo povu!
 
JPM anatakiwa akaze zaid
ya hapo, mtu amekuonyeshea chuki ya waz waz, tena anakuombea ufe alaf bado unamlea, huyo hata akipata chance ya kukupoteza anakupoteza, cha kufanya ni kumchinjilia mbali , na hakuna cha ushaur hapo mi unafki mtupu
Anao ubavu wa kukaza?Mtu mwenyewe kawa kama gari la mkaa, trip moja mwituni likirudi garage!
 
Na wewe kama kiongozi (hata kwa kutoa hoja tu hapa tayari wewe ni kiongozi kwa sababu kuna watu wanakusoma na maamuzi yao kuathiriwa kwa namna flani na unachoandika), kabla ya kuamua kuji "behave" kwa namna flani, jiulize kama kila mtu akiamua kuji 'behave the same!' nini kitatokea?

Baada ya hapo ukijiridhisha kwamba kitakachotokea ni kitu kizuri, basi endelea lakini kama sio, acha hata kama unachotaka kukifanya unakitamani.
 
Hakuna anayependa kushauriwa jambo ambalo anaona yeye yupo sahihi na hakuna kabisa anayependa kukosolewa.
Leo nimepigwa block na shangazi fatma karume kule tweeter kisa tu kumshauri aache kuchukua habari za uongo, alafu ndio wa kwanza kujifanya ooh freedom of speech. Pumbaavu kabisa

Tuonyeshe ulimshauri nini, maana hata hapa unacholazimisha ni wapinzani wafanyiwe ukatili kisa wamefurahia uvumi kumuhusu rais.
 
Tuonyeshe ulimshauri nini, maana hata hapa unacholazimisha ni wapinzani wafanyiwe ukatili kisa wamefurahia uvumi kumuhusu rais.
Ukatili katika ujumla wake bila kujali anayefanya ni nani ana anayefanyiwa ni nani ni kitu kisichokubalika katika ujumla wake. Kufanya, kuchochea au kushabikia siasa zenye muelekeo huo ni moja ya hiki tunachoweza kukiita kushadidia siasa za aibu.

Kwa hiyo hilo ni tatizo kama yalivyomatatizo mengine, tatizo ni pale linapotokea tatizo watu wanaanza kuangalia mfanyaji ni nani na mwathirika ni nani badala ya kuangalia kama suala lenyewe ni sawa au si sawa. Hapo ndipo tunapojikuta tunapoteza moral authority na kugeuka kuwa watu wa ajabu.
 
Back
Top Bottom