Najaribu kutafakari, kwa mfano uchaguzi wa Rais na wabunge ungekuwa unafanyika leo, ndiyo leo! hali ingekuwaje? Uchaguzi wenyewe uwe huru, wa amani na wa haki kabisa, ninamaanisha uwe huru na wa haki kwelikweli, wenye kampeni za kistaarabu, bila vitisho, bila hisia za wizi wa kura, bila mitutu, bila ushawishi wa aina yoyote ile, yaani unaenda kupiga kura ukiwa na amani, bila shida yoyote, unadhani ingekuwaje? Nani angeshinda na nani angeshindwa vibaya?
Ingekuwaje?
Ingekuwaje?