hivi uaminifu ktk ndoa ni jukumu la mwanamke peke yake au??

arnolds

Senior Member
Oct 10, 2009
105
57
Amani kwenu wadau!
hivi hii imetulia kweli?, Kama ikitokea mwanaume ameenda nje ya ndoa ishu inaonekana ni simple tofauti na mwanamke akitoka nje ya ndoa! Naomba mnisaidie kwanini mwanamke akikosa uaminifu ishu inakua ni kubwa mno ukilinganisha na mwanaume?!!

big up fellas!.
 
hapo unatumika mfumo dume kumkandamiza mwanamke na majina kibao malaya fujo kwakwenda mbele sijawahi kusikia mwanaume akiitwa malaya ikawa na nguvu kama kwa mwanamke
 
Mbona wanaume nao wanaitwa VIWEMBE, KICHECHE AU NANIHII MKONONI?????
 
nadhani hapa tatizo ni jinsi jamii inavyoamini kuwa katika suala la ngono mwanaume siku zote yuko sahihi kulinganisha na mwanamke. chukulia hata jinsi ambavyo mwanaume akifumaniwa mwanamke atalazimishwa kusamehe kuwa ni shetani lakini tofauti na mwanamke akifumaniwa ujuwe uwezekano mkubwa ni kuachika na majina kibao yatafuatia. So lazima jamii ibadirike kuhusu haya mambo. Kama kosa limefanyika basi lionekane pande zote.
 
Mapokeo hayo tuliyonayo,kutoka kwa MABABU ZETU hata kwenye VITABU vyetu vitakatifu mwanamke anaonekana hana haki kama ya mwenzi wake mwanaume. Ni ngumu sana hii issue,sababu tulipokuwa wadogo na mpaka sasa bado nasikia watoto wa kiume wakiambiwa au tukiwaambia eti unalialia nini kama mwanamke, au usiwe lazy km mwanamke, au mambo yake kama ya kike, hapa kichwani mwa mtoto wa kiume inamjenga kuwa OK kumbe mwanamke ni mtu asiye na uwezo kama mwanamme, katika shughuli nyingi mwanamke anatengwa anaonekana kama hafai kuwepo huko ingawa akipewa nafasi anaweza akafanya zaidi ya hata huyo mwanamme. Hii ndo inapelekea hata ndani ya NYUMBA mwanaume anaweza akachinja mtu akiibiwa mke wake wakati yeye MWANAUME anaweza akawa kazaa nje ya ndoa au hata ana VIMADA kibao tuu. Nakumbuka wakati naishi Morogoro miaka ya 1987-1989 kuna Mwalimu wetu alifumaniwa live kitaani akimegwa na mme wa mtu, yule mwalim aibu alihama na shule, lkn yule mme wa mtu watu walimsifia sana tuu dah jamaa mkali kala yule ticha, maana ticha alikuwa kifaa kweli kweli, mke wa yule jamaa mzinzi na yeye akaishia kufarijiwa na watu tu na mmewe kumuomba samahani yakaisha. ILA yule baba ndo angemfumania mkewe anamegwa sidhani km yule mwanamke angerudi salama kwao hahahahaha.Wengine wana sema kutokana na maumbile yalivyo tofauti mwanaume anaingia na kutoka lkn mwanamke anaingiliwa na kuachiwa *****. hii ndo inamfanya mwanaume asipende katu KUMEGEWA. HATA MIMI NTAUA MTU JAMANI. lkn simegi nje kwa heshima ya MAMSAP
 
Wengine wana sema kutokana na maumbile yalivyo tofauti mwanaume anaingia na kutoka lkn mwanamke anaingiliwa na kuachiwa *****. hii ndo inamfanya mwanaume asipende katu KUMEGEWA. HATA MIMI NTAUA MTU JAMANI. lkn simegi nje kwa heshima ya MAMSAP

Hii kali..... kama ni kweli basi kazi ipo! Na je kama kuna sox anaachiwaje? ASHAKUM SI..M.....SI!
 
Amani kwenu wadau!
hivi hii imetulia kweli?, Kama ikitokea mwanaume ameenda nje ya ndoa ishu inaonekana ni simple tofauti na mwanamke akitoka nje ya ndoa! Naomba mnisaidie kwanini mwanamke akikosa uaminifu ishu inakua ni kubwa mno ukilinganisha na mwanaume?!!

big up fellas!.

Ni kwa sababu ya inflated male ego. Sio haki lakini ndivyo jinsi mambo yalivyo...
 
Amani kwenu wadau!
hivi hii imetulia kweli?, Kama ikitokea mwanaume ameenda nje ya ndoa ishu inaonekana ni simple tofauti na mwanamke akitoka nje ya ndoa! Naomba mnisaidie kwanini mwanamke akikosa uaminifu ishu inakua ni kubwa mno ukilinganisha na mwanaume?!!

big up fellas!.

siku zote, mapenzi ni socially defined na sio biologically defined. hivyo hayo yote ni mambo ya kijamii na nisehemu ya mapenzi, ni romance kamili. hakuna matatizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom