Hivi Twiga cement nao ni wezi?

mikimba

Member
Oct 20, 2010
6
0
Jamani Ndugu zangu wana JF sijui nikimbilie wapi.Nilinunua Hisa za Tanga cement mwaka 2003 ,niliweza kupata Gawio mara tatu baada ya hapo sikupata tena.Mwanzoni ulikuwa unatakiwa kutoa acount yako ya bank baadaye wakabadilisha wakawa wanatuma posta na unalipiwa huko.Baada ya hapo sijui ni kitu gani kinachoendelea.Nimewaandikia kutupitia anuani yao ya barua pepe simbacement@infor.co.tz mara mbili lakini hawajibu.tangu mwaka 2007 sijapata gawio lolote na bahati mbaya nimepata barua inayoonyesha gawio la mwaka 2003 la Tsh 200,000 nilipoenda posta wakaniambia niwaandikie Tanga cement maana kitu hiki ni cha zamani sana.Nikawandikia e-mail tangu tarehe 1/9/2011 mpaka leo sijajibiwa.
Nilinunua hisa 2,500 za NICO sijawahi kupata kitu,sikulalamika sana nikitarajia Tanga cement watanikomboa kumbe na wenyewe ni walewale.Naomba mwenye kunisaidia nifanyeje.Naumia
 
nico umeliwa , bali binasfsi nawatetea hao tanga cement. jaribu kufuatilia ama kama uliwahi kubadilisha anuani . pia ikibidi waendee kiwandani, kama unaona mawasiliano yote uliofanya bado hakuna manufaa, nakuhakikishia haki yako utapata.
 
Back
Top Bottom