Mindi
JF-Expert Member
- Apr 5, 2008
- 3,523
- 4,991
CCM pamoja na historia ndefu ya kutokea TANU, Pamoja na kwamba ipo madarakani miongo kadhaa, haijui maisha nje ya utawala, bado ni chama dhaifu sana kiasi kwamba hakiwezi kusimama chenyewe bila kubebwa na baiskeli ya wagonjwa ya Polisi, msukumaji usalama wa taifa. Haiwezi kufanya chochote bila mkono mmoja upo daima kwenye fuko la Hazina.
Angalia wanaume wa shoka pale ufipa. Daima wanatafutiwa kesi za kubambikizwa, viongozi wake mara wanafilisiwa na akaunti zao kufungwa na TRA. Mara miradi yao inavurugwa. Yaani ni mpambano muda wote.
Kiongozi wa CCM usipoangalia, hata mjumbe utapigiwa saluti na polisi. Viongozi wa CCM ni mayai mayai. Mambo mteremko.
Wala huhitaji kuhangaika kujua vyama wafuasi wa CCM. utaona chama cha upinzani lakini kinabebwa na polisi. Fedha ya ruzuku nje nje. Hakuna kesi wala mikwaruzo.
Katika mazingira haya, CCM wala siyo chama cha siasa. Ikijitenga na na madaraka tu, inakufa. Haifui dafu hata chembe kwa CHADEMA
Angalia wanaume wa shoka pale ufipa. Daima wanatafutiwa kesi za kubambikizwa, viongozi wake mara wanafilisiwa na akaunti zao kufungwa na TRA. Mara miradi yao inavurugwa. Yaani ni mpambano muda wote.
Kiongozi wa CCM usipoangalia, hata mjumbe utapigiwa saluti na polisi. Viongozi wa CCM ni mayai mayai. Mambo mteremko.
Wala huhitaji kuhangaika kujua vyama wafuasi wa CCM. utaona chama cha upinzani lakini kinabebwa na polisi. Fedha ya ruzuku nje nje. Hakuna kesi wala mikwaruzo.
Katika mazingira haya, CCM wala siyo chama cha siasa. Ikijitenga na na madaraka tu, inakufa. Haifui dafu hata chembe kwa CHADEMA