Jibuni swali ndiyo maana huwa mnafeli. Rais Trump amekosea kwa kukiuka makubaliano yaliyopitishwa na Umoja wa Mataifa na kukubaliwa pia na Jumuiya ya Kimataifa. Ilikubaliwa na kupitishwa jiji la Jerusalem lisifanywe kuwa mji mkuu wa I utawala wa Israel kama njia mojawapo ya kutatua migogoro inayojitokeza mara kwa mara kati ya Waisrael na Waparestina. Bali jiji hili lisalie kuwa 'mji mtakatifu' kwa dini za kiyahudi, kiislamu, na kikristo. Sasa Waisrael wao wanadai Jerusalem ni capital city yao na inapaswa kuwa hivyo kwa vyovyote iwavyo. Rais Trump ni kama katumia 'ubabe', labda. Anyway, suala la mgogoro wa Mashariki ya Kati linatatanisha sana na hasa ukitilia maana limejichanganya na kubebwa na IMANI ZA KIDINI kwa pande zote mbili. Tuwaombee Amani. Hawajawahi furaia amani wenzetu wale, ni kuuana tu! Hebu fikiria mtu anakuwa na silaha ubafuni mwake hata awapo kwenye starehe.