Wana JF leo nimeshangazwa kisa hichi ndani ya gazeti la Daily News la 12/7/2019 page ya 3. Sijui kwanini tunajisahau au tunafikiri kwamba sisi wote ni kama malaika. Katika mawazo yangu nilidhani dhahabu inatunzwa chini ya usimamizi na ulinzi mkali ndani ya chumba maalumu kama "Strong Room" ambacho funguo zake hicho chumba lazima wawenazo watu wawili (2) ili kudhibiti upotevu. Sasa kama mtu moja anaweza kuwa na access na madini yote hayo unategemea kitatokea nini siku nyumbani kwake akiwa na shida ya pesa na kila siku ana madini hapo karibu ofisini?
Biblia inasema " Usinitie majaribuni" sasa naona ndo kama hayo majaribu.
Nashauri basi waende wakaulize benki wajue jinsi "Strong Room" pakutunzia pesa Benki zinavyolindwa na kuhakikisha funguo zinakaa na watu wawili ili kuweka ulinzi zaidi.
Biblia inasema " Usinitie majaribuni" sasa naona ndo kama hayo majaribu.
Nashauri basi waende wakaulize benki wajue jinsi "Strong Room" pakutunzia pesa Benki zinavyolindwa na kuhakikisha funguo zinakaa na watu wawili ili kuweka ulinzi zaidi.