Babu Kijiwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2010
- 4,762
- 4,576
Kwa wiki hizi chache niliamua kusitisha shughuli zangu za kuuza mikate stand ya Ubungo na kuanza kuzunguka mikoa mbalimbali kukusanya maoni ya raia mbalimbali kuhusu mwenendo wa nchi hususan katika awamu hii ya tano.
Niliwahoji kwenye daladala, bodaboda, vijiwe vya story, wafanya biashara wa kati, wakulima na raia wengine, ki ukweli Magufuli anakubalika kila kona ya nchi hii, nikaona ngoja niende mikoa ya kusini ambapo mpaka leo hii bado nipo huku na nimeshuka kwenye daladala muda mfupi ulio pita, huku kusini mwamba wanamkubali balaa.
Sioni kabisa future kwa CHADEMA, sioni future kwa Membe, narudia tena sioni. Na ziara hii imefanya nijiulize hivi hiyo Tanzania wanayozungumzia CHADEMA na hao wapiga kelele wengine ni hii hii au ni ile ya Kigogo2014 ambayo kuna miili kila kona imetapakaa kwa COVID-19? Nafikiri kuna Tanzania nyingine ipo Twitter na JF lakini kwa Tanzania hii ninayoishi na uhakika wapinzani hawatapata hata 10% ya kura zote zitakazopigwa.
Pole sana Lissu, umedunguliwa na risasi na unadunguliwa tena na Watanzania kwenye uchaguzi 2020
Niliwahoji kwenye daladala, bodaboda, vijiwe vya story, wafanya biashara wa kati, wakulima na raia wengine, ki ukweli Magufuli anakubalika kila kona ya nchi hii, nikaona ngoja niende mikoa ya kusini ambapo mpaka leo hii bado nipo huku na nimeshuka kwenye daladala muda mfupi ulio pita, huku kusini mwamba wanamkubali balaa.
Sioni kabisa future kwa CHADEMA, sioni future kwa Membe, narudia tena sioni. Na ziara hii imefanya nijiulize hivi hiyo Tanzania wanayozungumzia CHADEMA na hao wapiga kelele wengine ni hii hii au ni ile ya Kigogo2014 ambayo kuna miili kila kona imetapakaa kwa COVID-19? Nafikiri kuna Tanzania nyingine ipo Twitter na JF lakini kwa Tanzania hii ninayoishi na uhakika wapinzani hawatapata hata 10% ya kura zote zitakazopigwa.
Pole sana Lissu, umedunguliwa na risasi na unadunguliwa tena na Watanzania kwenye uchaguzi 2020